Oti Kate
Member
- Dec 20, 2011
- 58
- 59
Wana JF
Kwa kweli huyu mwigulu anatuaibisha sana sisi wote ambao tumesoma chuo kikuu sehemu ya mlimani. Niliposikia kwa mara ya kwanza akijisifu kuwa yeye ni mchumi wa daraja la kwanza kutokea mlimani then BoT, nilisema ayamkini kijana
ameteleza ulimi, so sikutegemea kusikia tena akijinasibu kwa maneno hayo!
Cha ajabu jana akiwa TBC katika mdahalo, alirudia maneno hayo tena na zaidi. Sasa wewe Mheshimiwa (wa kuiba wake za watu) wach huo utoto, hayo mambo ya kijisifia elimu na uwezo wako, hebu waachie watoto wa std. 7 na form one, wewe angalia nini wana-Iramba magharibi wamekutuma au wamekosa kule jimboni ili uwawakilishie kwa wahusika hapo mjengoni.
Kama kila mtu angeamua kujisifu hapo bungeni kuhusu shule yake, nadhani muda wa bunge la bajeti usingetosha......kumbuka kuna maprofesa humo humo ndani ya CCM ingawa Mchungaji Msingwa alituthibitishia kuwa wanafikiri kama watoto wa darasa la pili, lakini kumbuka wameenda shule.
Hebu wacha huo utoto, fanya kilichokupeleka bungeni........................unatuabisha wenzako tuliopitia mlimani, tutaonekana kichwa maji kaka wewe!
Kwa kweli huyu mwigulu anatuaibisha sana sisi wote ambao tumesoma chuo kikuu sehemu ya mlimani. Niliposikia kwa mara ya kwanza akijisifu kuwa yeye ni mchumi wa daraja la kwanza kutokea mlimani then BoT, nilisema ayamkini kijana
ameteleza ulimi, so sikutegemea kusikia tena akijinasibu kwa maneno hayo!
Cha ajabu jana akiwa TBC katika mdahalo, alirudia maneno hayo tena na zaidi. Sasa wewe Mheshimiwa (wa kuiba wake za watu) wach huo utoto, hayo mambo ya kijisifia elimu na uwezo wako, hebu waachie watoto wa std. 7 na form one, wewe angalia nini wana-Iramba magharibi wamekutuma au wamekosa kule jimboni ili uwawakilishie kwa wahusika hapo mjengoni.
Kama kila mtu angeamua kujisifu hapo bungeni kuhusu shule yake, nadhani muda wa bunge la bajeti usingetosha......kumbuka kuna maprofesa humo humo ndani ya CCM ingawa Mchungaji Msingwa alituthibitishia kuwa wanafikiri kama watoto wa darasa la pili, lakini kumbuka wameenda shule.
Hebu wacha huo utoto, fanya kilichokupeleka bungeni........................unatuabisha wenzako tuliopitia mlimani, tutaonekana kichwa maji kaka wewe!