Mwigulu serikali kuuingiza 5t kwenye uchumi ila hajatuambia prediction ya inflation rate, itakua je? Hili ndo dawa ya tozo ya miamala ya simu

mulwanaka

JF-Expert Member
Feb 19, 2017
5,262
12,835
Waziri wa Fedha na Mipango Dr Mwigulu Nchemba Amesema Serikali itaingiza zaidi Tsh 5 Trilioni Kwenye Mzunguko wa Fedha Hatua hiyo itawafanya Wananchi Kutosikia Machungu ya Tozo Mpya za Uzalendo Kwenye Miamala ya Simu.

Akizungumza Katika Uzinduzi wa Benki ya Biashara (TCB BANK) Dr Mwigulu Amesema Tozo Mpya za Miamala ya Simu zitaonekana Changamoto mwanzo lakini Mzunguko wa Fedha ukiongezeka na Fedha zikawa zinafikia Watu kwa Haraka Changamoto hiyo itaisha na Wananchi watazoea.

"Tumejipanga kuhakikisha tunatoa Fedha ya kutosha kwa Watoa huduma wa Serikali, Ikienda hivyo tulivyopanga tumedhamiria kutoa sio chini ya Tsh Trilioni 1 kwaajili ya Madeni tunayodaiwa na wazabuni wa Ndani ili kuibua wale Ambao Shughuli zao zilianza kupoa kwa Kuwa Fedha zimeshikiliwa Serikalini" Waziri Mwigulu Nchemba

Source Mwananchi
Screenshot_20210716-111611_Facebook.jpg
 
Ila mkuu wa mkoa wa dodoma nimeanza kumwelewa kumbe hao watuga sera hizi sera haziwahusu mtoto wachekechea analipa ada ya 16m Feza school kweli kiongozi kama huyu atajali raia wa kawaida vijijini.
 
Kabla ya kuchagua mtu kushika nyadhifa nyeti serikalini ni vema tusiishie kwenye vyeti vya shule bali tutazame na historia za maisha yao na exposure zao.

Maana wengi walipitia shida katika makuzi yao na shida zimewageuza kuwa ma''Sadists'.
 
Ila mkuu wa mkoa wa dodoma nimeanza kumwelewa kumbe hao watuga sera hizi sera haziwahusu mtoto wachekechea analipa ada ya 16m Feza school kweli kiongozi kama huyu atajali raia wa kawaida vijijini.
Fala sana haya majitu......
 
Back
Top Bottom