Mwigulu Nchemba: Wafanyabiashara msiogope kuweka fedha benki hazitachukuliwa

Wapi jack pemba na wenzie, nadhani sasa watarudi bongo baada ya jiwe kufa, watu wamepitia maisha magumu sana kisa kuwapa urais watu washamba yaani yeye kwa mtazamo wake mtu akiwa na maisha mazuri kidogo tu ni mwizi, amehangaisha sana matajiri huyo mzee aende tu salama.
 
Mwigulu: Mlioficha Pesa Nyumbani Ziwekeni Benki, Zitaliwa na Panya

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba amewataka wafanyabiashara wanaoficha fedha majumbani kuacha kufanya hivyo na badala yake wahifadhi benki kwa sababu haziwezi kuchukuliwa.

Aidha, Dkt. Mwigulu amesisitiza watendaji wa Wizara hiyo kutekeleza maagizo ya Rais Samia Suluhu kuhusu kupanua wigo wa kodi kwa kuongeza walipakodi wapya huku waliopo wakitakiwa kulindwa ili kukuza uchumi wa nchi.

“Kwa wale Wafanyabiashara ambao walishaanza kuona nikiweka hela yangu ikaonekana mtandaoni labda itachukuliwa yote, nitoe rai warudishe fedha kwenye mabenki, zitaliwa mchwa huko na panya bila sababu.

“Mojawapo ya mambo yanayojitokeza hata katika mijadala mingi bungeni ni ukadiriaji wetu tunaoufanya wa kodi zetu tuufanye kwa kuzingatia sheria na weledi katika sekta hiyo ya ukusanyaji mapato.

“Kuna maeneo ambayo yamekuwa yakijitokeza yanaleta mkanganyiko tuyaache mfano anatokea mtu ameshakadiriwa miaka yote kodi na amepewa ‘clearance’ kwamba huyu tumemkadiria na amelipa inapita miaka kumi anaenda kukadiriwa tena anapigiwa hesabu ya miaka kumi au kumi na tano ambayo katika miaka hiyo yote alipewa certificate.

“Kuna wale ambao wao mara zote wanabadilisha maelekezo nadhani niwape angalizo mapema tu maana yake wakati msisitizo umetolewa kuwa tukusanye kodi wale wengine walikuwa wanaenda wanavamia tu wanasema tumeambiwa tukusanye kodi mpaka mtakoma.

“Sasa hivi watu wataambiwa kusanyeni kwa weledi halafu wataenda waseme sasa hivi ni kula kuku tu nchi hii tutaijenga sisi wenyewe na tutaijenga kwa kodi,” Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba.
 
images (22).jpeg
 
Suala kama hili linatakiwa kuwa la kisheria na sio discretion ya waziri. Bunge lingesema wazi kwa kuwa na sheria, kwambaserikali inaweza kuchukua hela zako benki wakati wowote ikitaka, au lisema serikali haiwezi kuchukua hela zako. Uamuzi wa watu kuficha hela majumbani mwao, au kuweka nje ya nchi itategemea uwazi huo.

Inawezekana serikali inajua kitu fulani, ndio maana ilifanya hivyo. Sidhani kama serikali ina lengo tu la kuonea wafanyabiashara.
 
Warudishe kwanza zilizochukuliwa ikiwemo na za wa maduka ya bureau de change ya Arusha na Dar.Ccctv camera si zipo na waliochukua si wanajulikana waeleze walizipeleka wapi maana kama ni uhakiki sio kwa zaidi ya miaka hio 3
 
Kumbe wapinzani walikuwa wanasema kweli. Mataga yanaaibika kila siku. Na JPM wao amekataliwa mbinguni na toharani sasah8vi anachomeka kwa Lucifer.
 
Taarifa hii ni kwa mujibu wa Waziri wa Fedha Dkt Mwigulu Lameck Nchemba akiongoza kikao kazi cha kuchakata maagizo ya Rais Samia kwa Wizara hiyo.

Waziri amewaambia Wafanyabiashara nchini kote na Watanzania kwa ujumla wasiogope kuweka fedha zao Benki kwani zitakuwa salama na hazitachukuliwa.

Dkt. Mwigulu ameteuliwa hivi karibuni na Mhesh Rais Samia kuongoza Wizara ya Fedha akitokea Wizara ya Sheria na Katiba.

Hapa kazi tu & Zege halilali

MCL

=============

Waziri wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dk Mwigulu Nchemba amewataka wafanyabiashara wanaoficha fedha majumbani kuacha tabia hiyo kwa maelezo kuwa fedha zao haziwezi kuchukuliwa.

Dk Mwigulu ameeleza hayo leo Jumamosi Aprili 3, 2021 katika kikao na watendaji wa wizara hiyo na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) na Msajili wa Hazina (TR).

“Kwa wale wafanyabiashara walioona wakiweka fedha zao zitaonekana mtandaoni labda zitachukuliwa zote nitoe rai warudishe fedha kwenye mabenki zitaliwa mchwa au panya bila sababu, uchumi wa kisasa sio wa kuweka fedha kwenye boksi.”

“Kodi itatozwa tu kwa sehemu ya fedha inayotakiwa kukusanywa na sisi tujenge utaratibu wa kutii sheria kulipa kodi na kuwa wazalendo kwa nchi yetu.” Amesema Mwigulu.
Apeleke muswada bungeni kuifuta ile sheria iliyoruhusu. Maneno matupu hayavunji mfup
 
Hili tamko waandikiwe kabisa mabenki waandikiwe kabisa TRA wamedsababisha shida kwa wafanyabiashara mfano unadaiwa kodi umepewa order ya mzigo mteja anaweka pesa kwenye Akaunti ili umtumie mzigo au umnunulie TRA wabazibeba !!!

St Jude secondary Arusha walibeba ada za wanafunzi na ni shule ambayo wafadhili ndio hulipia wanafunzi wanaotoka familia maskini

Benki madalali wa mazao hadi wanaziogopa sababu unapewa mzigo uuze kisha umpe tajiripesa yake ukiuza umpe wakikuta pesa benki wanasomba unaonekana mtakatisha pesa au mkwepa kodi
Income badala ya kuangalia business wanaangalia hela zinazoingia kwenye account na ku zi treat kama income wakati pesa ni za customer unayemuwekea kama dalali au aliyekutumia umnunjlie mzigo
Hili la kuangalia deposts na kuziona kama business income na kudai maelezo na ku zi treat kama money laundering si sahihi zina scare depositors
Acha unafiki wewe fala, kipindi Cha nyuma wakati tunalalamikia haya si mlikuwa mnatutukana?
 
Back
Top Bottom