OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 48,772
- 102,128
Tusikilizane wanajukwaa
Wachambuzi wa mambo ya siasa na uchumi wameeleza sababu kubwa ya "kuloa'' mapema kwa serikali ya awamu ya tano ni washauri wa rais kushindwa kumshauri namna bora ya kuendesha nchi hususani uchumi wa nchi.
Wachambuzi wameeleza kuwa baraza la mawaziri linafanya kazi kwa hofu ya kutumbuliwa na hivyo kupelekea kuogopa kumwambia rais ukweli bado anapofanya kinyume.
Mbunge na waziri Luhanga Mpina kupitia vyombo vya habari alikanusha kwamba wao hawamuogopi Rais Magufuli bali wanamuheshimu Lakini ukweli unabaki palepale kwamba WANAMUOGOPA KWELI KWELI
Mhe.Mwigulu Nchemba waziri mbunge wa kuchaguliwa na aliyekuwa naibu waziri wa fedha awamu ya nne huku akiwa mchumi mwandamizi pale BOT anaonekana kuwa kiranja wa mawaziri wanaomuogopa rais.....nitaeleza
Waziri huyu alikuwa waziri wa fedha awamu ya NNE huku akionekana kinara zaidi ya Saada Mkuya...anafahamu vyema Sera na kanuni za uchumi na namna walivyoendesha wizara awamu ya nne,lakini haonekani kushauri mazuri hayo katika vikao vya baraza.
Mh.Mwigulu akiwa naibu waziri wa fedha katika awamu ambayo fixed deposit haikuonekana kuwa tatizo.Mh.Mwigulu akiwa waziri katika awamu ambayo halmashauri zilikuwa katika hali at least nzuri kiasi cha kuweza kujiendesha lakini haonekani kumshauri rais juu ya hali mbaya kabisa katika halmashauri zetu.
Mwigulu ameshindwa kumshauri rais kulipa madeni ya ndani kwa wazabuni na wakandarasi ambao bank zinakwenda kuwafilisi kutokana na kushindwa kulipa madeni
Tunamtaka Mh.Mwigulu kama mjumbe wa Jamiiforums aje hapa atuambie kwa nini anamuogopa rais?Na je,ni kweli kwamba wao ndio wanaoshauriwa na rais badala ya wao kumshauri rais?
Updates,................
Mh.Mwigulu amejibu kuwa yeye hamuogopi Rais na wanamshuri katika baraza.Lakini katika majibu take hajaonesha wala kujibu maswala tuliyoibua kuonyesha kwa nini tunasema wanamuogopa.
Tunamuomba sasa ajibu hayo pamoja na mambo mengine yanayoulizwa na wanajukwaa hususani kuonekana mganganyiko na contradictions kati ya matamko ya rais na mawaziri wake
Wachambuzi wa mambo ya siasa na uchumi wameeleza sababu kubwa ya "kuloa'' mapema kwa serikali ya awamu ya tano ni washauri wa rais kushindwa kumshauri namna bora ya kuendesha nchi hususani uchumi wa nchi.
Wachambuzi wameeleza kuwa baraza la mawaziri linafanya kazi kwa hofu ya kutumbuliwa na hivyo kupelekea kuogopa kumwambia rais ukweli bado anapofanya kinyume.
Mbunge na waziri Luhanga Mpina kupitia vyombo vya habari alikanusha kwamba wao hawamuogopi Rais Magufuli bali wanamuheshimu Lakini ukweli unabaki palepale kwamba WANAMUOGOPA KWELI KWELI
Mhe.Mwigulu Nchemba waziri mbunge wa kuchaguliwa na aliyekuwa naibu waziri wa fedha awamu ya nne huku akiwa mchumi mwandamizi pale BOT anaonekana kuwa kiranja wa mawaziri wanaomuogopa rais.....nitaeleza
Waziri huyu alikuwa waziri wa fedha awamu ya NNE huku akionekana kinara zaidi ya Saada Mkuya...anafahamu vyema Sera na kanuni za uchumi na namna walivyoendesha wizara awamu ya nne,lakini haonekani kushauri mazuri hayo katika vikao vya baraza.
Mh.Mwigulu akiwa naibu waziri wa fedha katika awamu ambayo fixed deposit haikuonekana kuwa tatizo.Mh.Mwigulu akiwa waziri katika awamu ambayo halmashauri zilikuwa katika hali at least nzuri kiasi cha kuweza kujiendesha lakini haonekani kumshauri rais juu ya hali mbaya kabisa katika halmashauri zetu.
Mwigulu ameshindwa kumshauri rais kulipa madeni ya ndani kwa wazabuni na wakandarasi ambao bank zinakwenda kuwafilisi kutokana na kushindwa kulipa madeni
Tunamtaka Mh.Mwigulu kama mjumbe wa Jamiiforums aje hapa atuambie kwa nini anamuogopa rais?Na je,ni kweli kwamba wao ndio wanaoshauriwa na rais badala ya wao kumshauri rais?
Nimeona thread ya kuwa Mawaziri wanamwogopa Rais, jambo hili HALINA UKWELI. Mawaziri wote tuko huru kushauri, Rais anatupa nafasi ya kushauri, kujadili na tunaamua kama Baraza, Kila mwezi tunafanya Baraza na mawaziri tunakwenda na agenda. Rais hutoa nafasi kwa kila Waziri kuongea, tena wakati Mwingine Rais huita mpk Naibu Mawaziri wote kwenye Baraza ili watoe ushauri kwenye mambo ya Nchi. Hivyo kauli ya kwamba mawaziri wanaogopa sio za kweli
Mwigulu
Updates,................
Mh.Mwigulu amejibu kuwa yeye hamuogopi Rais na wanamshuri katika baraza.Lakini katika majibu take hajaonesha wala kujibu maswala tuliyoibua kuonyesha kwa nini tunasema wanamuogopa.
Tunamuomba sasa ajibu hayo pamoja na mambo mengine yanayoulizwa na wanajukwaa hususani kuonekana mganganyiko na contradictions kati ya matamko ya rais na mawaziri wake