Interest
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 3,432
- 7,055
Kiongozi na Muwakilishi wa Wananchi wa jimbo la Iramba mkoani Singida, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amefunguka kuwa ni rahisi kumnadi Rais Magufuli kuendelea na awamu nyingine 2020 kwa sababu kazi alizozifanya zinaonekana.
Mwigulu ambaye muda wote anaonekana kuwa positive na Serikali/Chama chake tofauti na viongozi wengine, ameitaja miradi ya umeme vijijini, SGR, Nyerere Power Station ya Rufiji, Ndege, Vivuko, Meli na Madaraja kama vielelezo tosha vitakavyosaidia kumnadi kirahisi Dkt. John Magufuli mwaka 2020.
Hayo yote ameyasema wakati akijibu hoja ya kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo, Ndg. Zitto Kabwe ambaye aliandika:
#MwagaPombe2020 #VoodooEconomy
Magufuli amezuia USD Bilioni 52.8 ( TZS 121 Trilioni ) za FDI kuingia nchini na kuzuia Ajira zaidi ya Milioni 1. Mwezi Oktoba, 2015 Tanzania ilikuwa na miradi yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 52.8 yenye Fedha tayari na inayosubiri utekelezaji tu. Miradi hiyo ni pamoja na - Mradi wa Gesi Asilia Lindi ( LNG ) USD Bilioni 30: Mradi ungeifanya Tanzania kuwa mzalishaji wa 4 wa Gesi asilia Afrika na kuingizia Nchi Fedha za kigeni USD Bilioni 6 kwa mwaka.
- Mradi Eneo la Kiuchumi la Bagamoyo USD Bilioni 10: Mradi ungeifanya Tanzania kuwa Kituo kikuu cha Usafirishaji Afrika. Bagamoyo ingekuwa bandari ya 3 kwa ukubwa duniani.
- Mradi wa Reli ya Kati na Matawi yake yote kuunganisha Tanzania na DRC USD Bilioni 7.5 - Mradi wa Chuma cha Liganga na Makaa y Mawe ya Mchuchuma USD Bilioni 3.3: Mradi ungeifanya Tanzania kuwa Nchi ya 2 Afrika kuzalisha Chuma na ungeingiza Mapato ya Fedha za kigeni USD Bilioni 4 kwa mwaka
- Mradi wa Magadi Soda Engaruka USD Bilioni 2: Mradi ungeifanya Tanzania kuwa Nchi ya 3 duniani kuzalisha magadi soda baada ya Marekani na Uturuki na ingeingiza Mapato ya Fedha za kigeni USD Milioni 400 kwa mwaka.
Miradi yote hii ingekuwa ni Fedha zinazoingia nchini ( INFLOWS ) na Serikali isingetumia Fedha yake ya Kodi.
Badala yake Serikali ya CCM ya Awamu ya 5 imeamua kutoa nje Fedha za Nchi ( OUTFLOW ) ili kutekeleza baadhi ya miradi.
Matokeo yake;
- VYUMA VIMEKAZA kwa wananchi kutokuwa na Fedha kwa sababu ya Fedha kuondolewa kwenye mzunguko - Deni la Taifa kupaa kutoka Deni la Nje la USD Bilioni 15 mwezi Oktoba 2015 mpaka USD Bilioni 22 mwezi Juni 2019 na Deni la Ndani kutoka TZS Trilioni 8 mwezi Disemba 2015 mpaka TZS Trilioni 16 mwezi Juni 2019.
Wachumi wanaita hii ni voodoo economics! Unaacha kuingiza Fedha kwenye Uchumi na badala yake unazitoa na kuongeza Madeni kwenye Taifa.
#MwagaPombe2020 #KaziNaBata
Katika kile kinachoonekana ni kujibu hoja hizo, Dkt. Nchemba akaandika:
Bwana ZITTO, elewa, Rais MAGUFULI ametekeleza Ilani kwa kiwango cha juu Sana, Umeme zaidi ya Vijiji 7,100 mpaka sasa na kazi inaendelea, Hospitali zaidi ya Tarafa 350 na Kazi inaendelea, Lami imefungua mikoa ya Singida, Tabora, simiyu, na sasa mpaka Kigoma usikoona, Maji zaidi ya asilimia za kwenye ilani, Mabweni Kazi inaendelea.
Haya Ni ya jamii tu, Njoo miradi ya Kihistoria, kama SGR, Nyerere power Station ya Rufiji, Ndege, Vivuko, Meli na Madaraja ambavyo hata usipovisemea vizuri wewe, Watoto wako na wajukuu watakuja kusema kuwa alikwepo Rais mmoja akiitwa MAGUFULI alifanya mambo haya ya kizalendo.
Hivyo UPINZANI uwe na mgombea moja watashindwa, wawe wawili watashindwa, iwe wengi watashindwa, iwe NUSU MGOMBEA WATASHINDWA. Bila hata kubadili sentence moja ya Sheria . HAKUNA KAZI NYEPESI KAMA KUMNADI MAGUFULI, kwani KAZI ALIZOFANYA ZINAONGEA KULIKO MANENO. Tunayajua mnayojiandaa kuyasema, TUTAWAJIBU MUDA UKIFIKA YAANI Itakuwa hivi!!!! "CHAGUA MAGUFULI KAZI IENDELEE".
Hii sio mara ya kwanza kwa Dkt. Mwigulu Nchemba kujibu hoja za Zitto Kabwe hususani zile zinazoelezea masuala ya kiuchumi ambayo ni taaluma yake kwa ngazi ya Uzamivu.
Mwigulu ambaye muda wote anaonekana kuwa positive na Serikali/Chama chake tofauti na viongozi wengine, ameitaja miradi ya umeme vijijini, SGR, Nyerere Power Station ya Rufiji, Ndege, Vivuko, Meli na Madaraja kama vielelezo tosha vitakavyosaidia kumnadi kirahisi Dkt. John Magufuli mwaka 2020.
Hayo yote ameyasema wakati akijibu hoja ya kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo, Ndg. Zitto Kabwe ambaye aliandika:
#MwagaPombe2020 #VoodooEconomy
Magufuli amezuia USD Bilioni 52.8 ( TZS 121 Trilioni ) za FDI kuingia nchini na kuzuia Ajira zaidi ya Milioni 1. Mwezi Oktoba, 2015 Tanzania ilikuwa na miradi yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 52.8 yenye Fedha tayari na inayosubiri utekelezaji tu. Miradi hiyo ni pamoja na - Mradi wa Gesi Asilia Lindi ( LNG ) USD Bilioni 30: Mradi ungeifanya Tanzania kuwa mzalishaji wa 4 wa Gesi asilia Afrika na kuingizia Nchi Fedha za kigeni USD Bilioni 6 kwa mwaka.
- Mradi Eneo la Kiuchumi la Bagamoyo USD Bilioni 10: Mradi ungeifanya Tanzania kuwa Kituo kikuu cha Usafirishaji Afrika. Bagamoyo ingekuwa bandari ya 3 kwa ukubwa duniani.
- Mradi wa Reli ya Kati na Matawi yake yote kuunganisha Tanzania na DRC USD Bilioni 7.5 - Mradi wa Chuma cha Liganga na Makaa y Mawe ya Mchuchuma USD Bilioni 3.3: Mradi ungeifanya Tanzania kuwa Nchi ya 2 Afrika kuzalisha Chuma na ungeingiza Mapato ya Fedha za kigeni USD Bilioni 4 kwa mwaka
- Mradi wa Magadi Soda Engaruka USD Bilioni 2: Mradi ungeifanya Tanzania kuwa Nchi ya 3 duniani kuzalisha magadi soda baada ya Marekani na Uturuki na ingeingiza Mapato ya Fedha za kigeni USD Milioni 400 kwa mwaka.
Miradi yote hii ingekuwa ni Fedha zinazoingia nchini ( INFLOWS ) na Serikali isingetumia Fedha yake ya Kodi.
Badala yake Serikali ya CCM ya Awamu ya 5 imeamua kutoa nje Fedha za Nchi ( OUTFLOW ) ili kutekeleza baadhi ya miradi.
Matokeo yake;
- VYUMA VIMEKAZA kwa wananchi kutokuwa na Fedha kwa sababu ya Fedha kuondolewa kwenye mzunguko - Deni la Taifa kupaa kutoka Deni la Nje la USD Bilioni 15 mwezi Oktoba 2015 mpaka USD Bilioni 22 mwezi Juni 2019 na Deni la Ndani kutoka TZS Trilioni 8 mwezi Disemba 2015 mpaka TZS Trilioni 16 mwezi Juni 2019.
Wachumi wanaita hii ni voodoo economics! Unaacha kuingiza Fedha kwenye Uchumi na badala yake unazitoa na kuongeza Madeni kwenye Taifa.
#MwagaPombe2020 #KaziNaBata
Katika kile kinachoonekana ni kujibu hoja hizo, Dkt. Nchemba akaandika:
Bwana ZITTO, elewa, Rais MAGUFULI ametekeleza Ilani kwa kiwango cha juu Sana, Umeme zaidi ya Vijiji 7,100 mpaka sasa na kazi inaendelea, Hospitali zaidi ya Tarafa 350 na Kazi inaendelea, Lami imefungua mikoa ya Singida, Tabora, simiyu, na sasa mpaka Kigoma usikoona, Maji zaidi ya asilimia za kwenye ilani, Mabweni Kazi inaendelea.
Haya Ni ya jamii tu, Njoo miradi ya Kihistoria, kama SGR, Nyerere power Station ya Rufiji, Ndege, Vivuko, Meli na Madaraja ambavyo hata usipovisemea vizuri wewe, Watoto wako na wajukuu watakuja kusema kuwa alikwepo Rais mmoja akiitwa MAGUFULI alifanya mambo haya ya kizalendo.
Hivyo UPINZANI uwe na mgombea moja watashindwa, wawe wawili watashindwa, iwe wengi watashindwa, iwe NUSU MGOMBEA WATASHINDWA. Bila hata kubadili sentence moja ya Sheria . HAKUNA KAZI NYEPESI KAMA KUMNADI MAGUFULI, kwani KAZI ALIZOFANYA ZINAONGEA KULIKO MANENO. Tunayajua mnayojiandaa kuyasema, TUTAWAJIBU MUDA UKIFIKA YAANI Itakuwa hivi!!!! "CHAGUA MAGUFULI KAZI IENDELEE".
Hii sio mara ya kwanza kwa Dkt. Mwigulu Nchemba kujibu hoja za Zitto Kabwe hususani zile zinazoelezea masuala ya kiuchumi ambayo ni taaluma yake kwa ngazi ya Uzamivu.