Moshe Dayan
JF-Expert Member
- Feb 10, 2008
- 815
- 698
its called tactical combat deployment
Ukimuuliza ni kwanini kambi ya Vifaru iko Kibaha si ajabu akakujibu kuwa ni kutokana na kuwa karibu na bandari hivyo gharama za usafiri ni rahisi zaidi, ukimuuliza swali la pili mbona mabomu ya vifaru hayapo Kibaha atakwambia yamepelekwa mbali na mjini.........Mchumi wetu bana duhh.....its called tactical combat deployment
Nilikua najua kwani masuala ya ulinzi hasa ya jeshi huwezi kuanzisha kambi kama alivyofanya Lyatonga na vituo vya polisi vya kata......kuuliza sio ujinga,we ulikuwa unajua hivyo??
Yalipolipuka mabomu mbagala akina Slaa na mbowe walikuwa wakwanza kuhoji kwanini kambi za kijeshi zinawekwa mjini wakaonekana majiniazi
Kahoji mwigulu the same thing anaonekana taahira.........,..what a double standard
Mapenzi ya vyama vyetu yasitupofushe upeo wetu wa fikra
Hata Navy alitaka iwe kwenye mto mmojawapo huko Iramba .......Kwahiyo ulitaka KAMBI ya jeshi ya kulinda uwanja wa ndege wa kimataifa wa Tanzania ipelekwe IRAMBA?
Mwenye wivu naye nani Nahodha aliyemwambia kuanzisha kambi ya JWTZ sio sawa na kuanzisha shamba darasa au nani hasa? Maana kama Naibu katibu mkuu wa chama kinachotawala hajui maana ya kuanzisha kambi za jeshi kuwa ni suala la kimkakati huyu si ni mzigo hata kwa hicho chama na waliomteua?
Pia ukilitazama jibu la Nahonda kwa umakini utajua kuwa hamheshimu huyu jamaa hapa punje kwani angekuwa na punje ya heshima kwake walau angemjibu kuwa wazo halitekelezeki na kuishia hapo na sio kumpa vidonge kiasi kile
Hata Navy alitaka iwe kwenye mto mmojawapo huko Iramba .......
Mnambua wa mpi uwe na sikuyona ka nsoni.Huoni Tunaaibika wanyiramba kwa shallow thinking ya huyu mwenzetu.
Inamaana wote hawajui kuwa kambi za JESHI zinaanzia mbali na makazi ya watu ila miji inapanuka na mwisho wa siku watu wanawafikia.kamwe JESHI halianzishi kambi zake mjini chunguza kambi ya gongo la mboto ilianza lini utapata jibu kuwa pale lilikuwa ni pori na hawaishi watu.Slaa na Mbowe waliuliza kwa nini kambi za jeshi zinawekwa mijini karibu na makazi ya watu?
Kwa nini isekwae mwabepande, pugu ambapo hakuna msongamano wa watu.
Kwahiyo ulitaka KAMBI ya jeshi ya kulinda uwanja wa ndege wa kimataifa wa Tanzania ipelekwe IRAMBA?
Katika kipindi cha maswali na majibu leo asubuhi lilikuwepo swali la MBunge Mariam Msabaha wa CHADEMA aliyetaka kujua hatma ya mgogoro wa wanajeshi na wananchi huko Znz kuhusu ardhi, likafuatia la nyongeza la Ester Bulaya aliyetaka kujua hatima ya mgogoro wa wananjeshi na wananchi Kunduchi , baada ya majibu ndipo Mhe. Mwigulu aliuliza
'Ni kwanini serikali isihamishe kambi zote za jeshi maeneo ya mijini na kuzipeleka vijijini ambako kuna maeneo makubwa na hivyo migogoro itakuwa imeisha ......na alitaja eneo moja huko kwao Iramba kuwa linafaa kuwekwa kambi ya JWTZ '
Nahodha katika majibu yake alimjibu kuwa kambi za jeshi huwa hazianzishwi tu bila utaratibu bali hufanyika utafiti wa kina na wa kimkakakti katika maswala ya ulinzi kabla ya kufanya uamuzi wa kambi iwekwe wapi na iwe ni ya aina gani akimaanisha ya Vifaru, Kikoso cha anga ama ardhii na majini,
Hii ilikuwa aibu kubwa sana kwa mchumi namba moja ambaye ametoka JKT juzi hajui kuwa masuala ya ulinzi sio sawa na kuanzisha shhamba darasa Iramba kuwa unaangalia eneo lililopo theni unaanzisha shamba darasa .
Nimeona aibu sana kwa naibu katibu mkuu wa CCM ambaye hajui kuwa kambi za jeshi ni suala la kimkakati na hakuna nchi duniani eti mijini hakuna wanajeshi kwenye kambi .......Hao ndio viongozi wa CCM ya leo tutarajie nini kama sio maafa kwa taifa....