Mwigulu Nchemba acha kutuchonganisha na Rais Samia, umeanza kumshauri vibaya

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,735
6,291
Waziri wa Fedha na Mipango mnachokifanya hivi sasa ni kama vile mna shida sana ya pesa na mmeishiwa ubunifu na sasa mnataka kutuvika Mizigo ya madeni na matatizo ya Serikali kwa gharama yeyote ile.

1. Mmetuongezea kodi ya katika mawasiliano ya simu kwa vocha na vifurushi wakati tunalipa VAT. Uliposemwa semwa unadai mikopo ya SGR na Bwawa la Nyerere ni mikubwa itatuumiza so mnataka mzibezibe humo.

2. Mkatuongezea kodi nyingine ktk mafuta mkidai mnataka kumalizia barabara zilizoaki.

3. Sasa mnakuja tena na kodi ya Majengo kulipiwa kwenye Luku, Yaani unampunguzia Mpangaji idadi ya Token zake ili amlipie mwenye nyumba kodi ya Majengo. Hapo ameshalipa Maji, Kodi ya pango, bado ana maisha yake pia.

Hilo mmeona halitoshi mumpunguzie na Unit alipe kodi ya Jengo yeye halafu aende akamdai mwenye nyumba ambaye hata nyinyi Serikali kulipana naye hiyo kodi ya Jengo ni mpaka kizaazaa na vitisho vingi. Siyo bomu hili mnaenda kupika la kesi za madai na dhuluma?

Mahakama gani inayomaliza kesi ya madai ndani ya mwezi mmoja?

NARUDIA TENA, BWANA MWIGULU NCHEMBA UNATAKA KUTUCHONGANISHA NA MAMA YETU NA UNATURUDISHA UNYONGENI. MBONA SHUJAA MMEANZA KUMZIDI SHUJAA KATIKA KUTUBANA?
 
Kuna mkoa na mkoa ukiishi nao utawajua nitakuwa nimeeleka samahani Kwa watakokwazika ukweli utabaki kuwa ukweli
 
Sioni kama utaratibu wa kulipa kodi ya nyumba kwa luku ni mbaya kama watu mnavyodai

Hiv kweli wew mtu mzima 25+ years unashindwa kuongea na mwenye nyumba wako ili kuweka sawa suala la hii kodi ya nyumba? Kwamba unashindwa kusema mzee badala ya kukupa 50,000/- kwa mwezi sasa mimi nitakupa 49,000/- mana 1000/- nalipia na kodi ya nyumba?

Kama ni kweli watanzania wanashindwa hilo basi tuna taifa la watu wazembe wanaoitegemea serikali ambao hawawezi kufanya chochote wala kunegotiate chochote mpaka serikali iingilie kati na hivyo kuitwa wanyonge itakuwa haki yao
 
Kitendo cha kumsifia huyo dhalimu hapo mwisho nimejua wewe ni muhuni kama wahuni wengine. dhalimu hakuwabana wakati ndio alikuwa anapora hela za watu na kubambikia kodi.
 
Sioni kama utaratibu wa kulipa kodi ya nyumba kwa luku ni mbaya kama watu mnavyodai

Hiv kweli wew mtu mzima 25+ years unashindwa kuongea na mwenye nyumba wako ili kuweka sawa suala la hii kodi ya nyumba ? Kwamba unashindwa kusema mzee badala ya kukupa 50,000/- kwa mwezi sasa mimi nitakupa 49,000/- mana 1000/- nalipia na kodi ya nyumba....

Una uhakika wenye nyumba watakubaliana na hilo wazo?
 
Utaratibu wa kulipa shilingi elfu kavu za kodi ya nyumba haukupokelewa vizuri na umma. Zile foleni ndefu zinawapotezea watu muda wa kufanya shughuli zao nyingine.

Miradi ya treni ni mikubwa sana lakini itachagiza ukuaji wa uchumi ikikamilika.
 
Sioni kama utaratibu wa kulipa kodi ya nyumba kwa luku ni mbaya kama watu mnavyodai

Hiv kweli wew mtu mzima 25+ years unashindwa kuongea na mwenye nyumba wako ili kuweka sawa suala la hii kodi ya nyumba ? Kwamba unashindwa kusema mzee badala ya kukupa 50,000/- kwa mwezi sasa mimi nitakupa 49,000/- mana 1000/- nalipia na kodi ya nyumba...
Hawa wenye nyumba wanaolipwa kodi kwa njia ya simu wanadai na ya kutolea au unawazungumzia wengine?
 
Hii nchi ukisikiliza kila wapanua Domo hakuna kitu kitaenda maana watu wamejaa ulalamishi,lawama bila kuja na suluhisho
 
Sioni kama utaratibu wa kulipa kodi ya nyumba kwa luku ni mbaya kama watu mnavyodai

Hiv kweli wew mtu mzima 25+ years unashindwa kuongea na mwenye nyumba wako ili kuweka sawa suala la hii kodi ya nyumba ? Kwamba unashindwa kusema mzee badala ya kukupa 50,000/- kwa mwezi sasa mimi nitakupa 49,000/- mana 1000/- nalipia na kodi ya nyumba...
Watu wengi watagombana na wenye nyumba, labda wapangaji watulie bila kumdai mwenye nyumba hiyo kodi.

Vinginevyo wengi watapewa notice kila siku.

Na ukijidai kihereher unapandishiwa kodi unaulaza mwenyewe.
 
Kitendo cha kumsifia huyo dhalimu hapo mwisho nimejua wewe ni muhuni kama wahuni wengine. dhalimu hakuwabana wakati ndio alikuwa anapora hela za watu na kubambikia kodi.
Dhalimu wako hayupo mkuu!

Sasa mambo ni safi!
 
Waziri wa Fedha na Mipango mnachokifanya hivi sasa ni kama vile mna shida sana ya pesa na mmeishiwa ubunifu na sasa mnataka kutuvika Mizigo ya madeni na matatizo ya Serikali kwa gharama yeyote ile....
Shujaa ndio nani?

Jinga kabisa wewe.
 
Sioni kama utaratibu wa kulipa kodi ya nyumba kwa luku ni mbaya kama watu mnavyodai

Hiv kweli wew mtu mzima 25+ years unashindwa kuongea na mwenye nyumba wako ili kuweka sawa suala la hii kodi ya nyumba ? Kwamba unashindwa kusema mzee badala ya kukupa 50,000/- kwa mwezi sasa mimi nitakupa 49,000/- mana 1000/- nalipia na kodi ya nyumba...
Hutaki kupanga wewe.

Nyumba za mjini unazijua?
 
Waziri wa Fedha na Mipango mnachokifanya hivi sasa ni kama vile mna shida sana ya pesa na mmeishiwa ubunifu na sasa mnataka kutuvika Mizigo ya madeni na matatizo ya Serikali kwa gharama yeyote ile...
Magufuli si alisema hilo bwawa tunatengeneza kwa fedha zetu?
 
Back
Top Bottom