Mwigulu: Miradi ya Airport, SGR, e-passport na Ununuzi wa Ndege imepitia kwenye Baraza la Mawaziri, ipo kwenye Bajeti na imepitishwa Bungeni

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,432
7,055
Dkt. Mwigulu Nchemba, amejibu hoja ya Zitto Kabwe: Tangu lini Rais anaheshimu Bunge? Kosa la Lugola ni kufanya dili kwa kumzunguka Rais, hoja ya Bunge ni kisingizio tu

Ameandika:

Bwana zitto, jifunze kutafakari kabla hujaandika. Rais ameongelea "Mradi wa hovyo" na anasema mradi huu hauko kwenye bajeti, wala haukupitishwa kwenye baraza la mawaziri na bunge.

Sasa vinginevyo na unavyovisema, miradi kama Airport, SGR, e-passport, ununuzi wa ndege na mingine ni miradi iliyopo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, imepitiwa na Baraza la Mawaziri, ipo kwenye Bajeti na imepitishwa bungeni.

Acha kupotosha watu, mikataba huwa haisainiwi bungeni, wala hakuna siku bunge litajadili mkataba wa mradi labda maazimio na taarifa ya mkataba.

Kwa mikopo, kila mwaka serikali inaleta mapendekezo ya kukopa kwenye bajeti kuu na tunapitisha., sasa mantiki ya unachokisema iko wapi? Kama kawaida yako unapotosha kwa makusudi, kisiasa na kirafiki.

Nani asiyejua ulikuwa kamati moja na kangi na wengine uliwatumia sana kwa maslahi binafsi? Watanzania wanakumbuka urafiki wenu ule na kwa maslahi yenu binafsi.
 
Sijui kwa nini munapoteza muda kujadili post za Zitto. Zitto aliyesoma namba kwenye vioo vya ndege na kutangaza kwamba ni used? Namuona ni mtu ambaye ana matatizo ya ufahamu. Kila jambo anataka awe wa kwanza kulitangaza.

Zitto alizoea kushangiliwa na watu waliochoka mfumo uliopita. Akishangiliwa, anakuwa kama mcheza mpira wa sekondari anayeshangiliwa na mabinti, anaanza kujirusha tu!
 
Bwana ZITTO, Jifunze kutafakari kabla hujaandika, RAIS ameongelea "MRADI WA HOVYO" na anasema mradi huu hauko kwenye BAJETI,wala haukupitishwa kwenye Baraza la Mawaziri na Bunge.
Sasa miradi kama Airport, SGR, e PASSPORT, Ununuzi wa Ndege na vinginevyo unavyovisema ni miradi ILIYOPO KWENYE ILANI YA UCHAGUZI YA CCM, IMEPITIWA na BARAZA LA MAWAZIRI, IPO KWENYE BAJETI NA IMEPITISHWA BUNGENI.

ACHA KUPOTOSHA WATU, Mikataba huwa HAISAINIWI BUNGENI, wala hakuna siku Bunge litajadili Mkataba wa Mradi labda maazimio na taarifa ya Mkataba.
KWA MIKOPO, Kila Mwaka serikali inaleta mapendekezo ya kukopa kwenye Bajeti kuu na tunapitisha., SASA MANTIKI YA UNACHOKISEMA IKO WAPI?

Kama kawaida yako UNAPOTOSHA kwa MAKSUDI, KISIASA na KIRAFIKI.

NANI ASIYEJUA ULIKUWA KAMATI MOJA NA KANGI NA WENGINE ULIWATUMIA SANA KWA MASLAHI BINAFSI ?? WATANZANIA WANAKUMBUKA URAFIKI WENU ULE NA KWA MASLAHI YENU BINAFSI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Interest,
Mwigulu huwa hana hoja mpaka Zitto Kabwe atoe mawazo yake. Nataka nimuambie kuwa pamoja na PhD yake ya "kuokoteza" hawezi kuifikia intellectualism ya Zitto na mvuto na uwezo wa kujenga hoja na uthubutu wa Zitto Kabwe. Leave Zitto Kabwe alone, he is not your class.

Halafu sahau kabisa kupata uteuzi kwa Jiwe
 
Mwigulu huwa hana hoja mpaka Zitto Kabwe atoe mawazo yake. Nataka nimuambie kuwa pamoja na PhD yake ya "kuokoteza" hawezi kuifikia intellectualism ya Zitto na mvuto na uwezo wa kujenga hoja na uthubutu wa Zitto Kabwe. Leave Zitto Kabwe alone, he is not your class.

Halafu sahau kabisa kupata uteuzi kwa Jiwe


Kama Zito Kabwe ni ,,intellectual“ basi hauelewi maana ya hilo neno!
 
Interest,
Simbachawene effect. Yani kila kada ana ndoto za kurudi ulajini. Kwa mfano mkataba wa Stiglers ulijadiliwa lini na bunge? Kwanini manunuzi ya ndege hayapelekwi bungeni badala yake tunashuhudia tu tukiambiwa ndege fulani itatua wakati fulani? Mwigulu funga domo lako!
 
Kwanza wewe upo kwenye blacklist ya CCM kama ulikuwa hujijui....hapa unajangaikia ka ubunge kako huko kwenu wasikate jina ...ukamtosa ndugu yako wa damu kabisa kisa tumbo...looh
Kweli binadamu Sisi ni watu wa ajabu kabisa...yaani nduguyo anapigwa marisasi kibao mchana mchana hajasema kitu kisa TUMBO aka njaa...

Wewe hufai kabisa...kaa kimya!!
 
Mwigulu ni mnafiki ! Anadhani akim- attack Zitto basi atarudishwa kwenye Uwaziri! Alijiona kuwa yeye ndo yeye!
Zitto ni level nyingine!
Mwigulu kaa utulie,kubali tu kuwa zama zako za kubebwa na JK zilishapita!
 
Hawa kina Kangi waliposafiri kusaini Mkataba nje ya Nchi walienda kwa kibali cha Ikulu au walisafiri bila ya kibali?

Nmekumbuka kwa sasa Taifa lipo bussy na issue ya Hamida
 
Back
Top Bottom