Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema hayo Mei 23, 2026 wakati akizungumza na wananchi katika Viwanja vya Kichangani kwenye ziara yake ya kikazi ya siku mbili.
"Tunagombanishwa mno. Watu wanapoteza muda hata wa kutafakari kila jambo, kwamba hili limetokeaje.
Unakaa hivi, unasikia
sister katekwa. Unakaa hivi, si padri katekwa. Unakaa hivi, nimeona mwingine jana tena... nimeona pale... nimeona mtandaoni pale eti katekwa. Mnaangalia mtu kaumizwa, anapingu.
Hii ni ajenda maalum. Hii ni michezo. Hii ni michezo.
Na hii michezo haijaanza jana. Hii ni michezo haijaanza jana kwa Tanzania, tuamke! Hizi ni ajenda za watu wenye akili wanaolitafuta taifa letu. Ni ajenda za watu wenye akili, hii sio mpuzi mpuzi tu hivi."