Mwigulu, huu ni uzembe mwingine wa jeshi la polisi

First Born

JF-Expert Member
Jul 11, 2011
5,310
1,473
Juzi tarehe 23 majira ya SAA nne asubuhi gari la polisi la Tandahimba liligonga gari la mpita njia Fulani maeneo ya lidumbe NEWALA mkoani Mtwara...

Gari la polisi lilikuwa lilikuwa linajaribu kuliovertake gari lingine kimakosa hadi kusababisha ajali mbaya sana lililosababisha gari la polisi kuharibika vibaya sana na kwa taarifa isiyo rasmi inasemekana moja ya majeruhi hao ambao ni askari amefariki akiwa hospitali ya NDANDA.

Kibaya zaidi ni kwamba gari la polisi halikuwa kwenye doria ya aina yoyote bali lilikwenda Newala kuchukua beer za moja wa maaskari hao mwenye baa yake Tandahimba....
Picha hapa chini inaonyesha jinsi gari hilo la serikali lilivyoharibika vibaya na jinsi pombe ilivyozagaa.

Huu si mchezo wa Mara moja ila ni kawaida kabisa ila wanasema mwisho wa ubaya huwa ni aibu.
IMG-20161223-WA0011.jpg
 
Lazima watumbuliwe kwa sababu Polisi hawana huruma kwa raia. Wanatesa wanabambikia kesi wanapiga raia saa ingine hata bila sababu. WATUMBULIWE
 
Lazima watumbuliwe kwa sababu Polisi hawana huruma kwa raia. Wanatesa wanabambikia kesi wanapiga raia saa ingine hata bila sababu. WATUMBULIWE
Unadhani kuna atakaetumbuliwa hapa? Maana hali inaonesha shwari kabisa, mambo haya hata redio ya hapa wilayani hawajatangaza... Utasema hakuna kilichotokea
 
Uendeshaji wao huwa ni mbaya sana, sijui kwanini aise? juzi ijumaa kanikosa kunigonga mmoja na gari yao Mungu tu alisaidia. Kwa kifupi wapo juu ya sheria hawa jamaa.
 
Nyoosha vizuri tuhuma zako maana umetueleza makosa lakini hujaeleza kama hatua za kinidhamu na kisheria hazijachukuliwa kwa watuhumiwa.
Mzee hali imekuwa shwari sana, Hamna hata dalili za hatua zozote kuchukuliwa
 
Back
Top Bottom