Mwigulu awataka TRA wasiombe kumbukumbu za miaka 10 hadi 15 iliyopita

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,001
9,866
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kutodai kumbukumbu za miaka mingi iliyopita huwa ni kero kwa wafanyabiashara

Amesema kawaida wafanyabiashara wakishamalizana na serikali hawana utaratibu wa kutunza kumbukumbu bali huwekeza nguvu nyingi katika kukuza biashara. Hivyo si sahihi kuomba kumbukumbu za miaka hiyo

Aidha, watanzania hawana kawaida ya kutunza kumbukumbu, suala hilo ndio limewaingiza wengi kwenye hatia ya kudaiwa kodi kubwa. Ametolea mfano kwa kuwaambia waandishi kama kuna yeyote kati yao mwenye ‘salary slip’ ya 2005

Amewataka wazingatie weledi katika kukusanya kodi kama alivyoagiza Rais Samia katika hotuba yake alipokuwa amewaapisha mawaziri na manaibu waziri Ikulu Dodoma
 
Duh Haya mambo yangekuwa yanafuata utaratibu ambao wadau (stakeholders wote) wanashirikishwa kuweka mifumo bora haya yasingetokea...

Kinachotokea sasa kila anayekuja anakuja na mawazo / mifumo yake bila kushirikisha wadau (wafanya biashara, watoza kodi na wahusika wote)
 
Dr Nchemba, waziri mpya wa fedha nenda kachape kazi kweli kweli watanzania walio wengi wanakutegemea na wanajua makusanyo yatapanda kutoka Trillion 1.3 ya sasa hadi Trillion 2 kwa mwezi, hii itatuhakikishia sisi watanzania miradi yetu mikubwa ya kimkakati kuendelezwa na kumalizwa kabisa.

Watanzania tunataka SGR , BWAWA LA NYERERE, UMEME KILA KIJIJI, HUDUMA ZA AFYA KUBORESHWA, BARABARA ZA LAMI KILA KONA, tusipoona haya hatutakuelewa.

Dr Nchemba usiende kuingia kwenye mtego wa wafanyabiashara wakwepa kodi wanaotaka uwafutie kodi zote alafu hizo kodi uwarundikie watanzania masikini mama ntilie na machinga kama ilivyokuwa zamani unakuta mfugaji au mkulima analipa kodi 10 ili amfikishe Ng'ombe wake mnadani, hatutarajii hili kutokea.
Dr Nchemba umejionea mwenyewe ulivyotukanwa na kuchambwa sana baada ya uteuzi wako na wakwepa kodi ( Chadema) wasiolitakia mema taifa hili kwao hata miradi yote ikikwama ni sawa tu, kwa hiyo hao siyo wenzako, hata siku moja usije kusikiliza ushauri wao. Hao ni nyoka kwa taifa hili.

Dr Nchemba kwa miaka mitano iliyopita hatujaona waziri wetu wa fedha akizunguka kuombaomba Ulaya ,kwa hiyo hatutarajii kukuona kila siku upo uwanja wa ndege unaenda kutembeza bakuri.

Dr Nchemba kwa miaka mitano iliyopita tumeambiwa Tanzania ni tajiri na watanzania tunaweza , hatutarajii waziri wetu mpya uanze kuimba Tanzania ni masikini na hatujiwezi kwa lolote ,ukifanya hivyo watanzania hatutakuelewa
 
TRA wanalaumiwa...

Mara oooh piga ua tunataka 2 Trilion per month...tuna imani utaweza

Mara usiwaulize wafanyabiashara kumbukumbu

Mara hatutaki watumishi wazembe..

Mara msidai kodi kwa nguvu tumieni akili.

Mara rafiki zangu wa TRA wawaache Wafanyabishara wafanye Bishara ya haki, wasiwanyanyase Wafanyabiashara, ninataka kodi kwa ajili ya kuhudumia Watanzania lakini sio kuwanyanyasa Wafanyabishara, wakusanye kodi kwa kuzingatia Sheria

Ninahisi Wahenga hawakukosea waliposema mwanasiasa akikwambia Usiku Mwema...toka nje uhakikishe.
 
TRA wanalaumiwa...

Mara oooh piga ua tunataka 2 Trilion per month...tuna imani utaweza

Mara usiwaulize wafanyabiashara kumbukumbu

Mara hatutaki watumishi wazembe..

Mara msidai kodi kwa nguvu tumieni akili.


Ninahisi Wahenga hawakukosea waliposema mwanasiasa akikwambia Usiku Mwema...toka nje uhakikishe.
 
Hii nchi ukikusanya effectively kwenye sekta tatu muhimu inatosha kuendesha bajeti ya nchi na kusaza, mfano bandari, madini, mafuta na gesi. Haya mambo ya kukusanya kodi kwenye kila eneo ndo inasababisha bei za bidhaa muhimu kupanda bei kila kukicha hali inayopelekea watu wengi kushindwa kumudu maisha ya kawaida kabisa na kupelekea mzunguko wa pesa na maisha ya kijamii kusinyaa......
 
TRA ni jipu bado

Hata wenyewe ukiwaomba kumbukumbu zako na wao za miezi 6 iliyopita hawawezi kukupa

Usipokua vizuri kwenye kutunza kumbukumbu ukajisemea nilishalipa records zitakua kwenye system ya TRA watakusumbua na kukuingiza gharama tena bila kujali
 
Dr Nchemba, waziri mpya wa fedha nenda kachape kazi kweli kweli watanzania walio wengi wanakutegemea na wanajua makusanyo yatapanda kutoka Trillion 1.3 ya sasa hadi Trillion 2 kwa mwezi, hii itatuhakikishia sisi watanzania miradi yetu mikubwa ya kimkakati kuendelezwa na kumalizwa kabisa.

Watanzania tunataka SGR , BWAWA LA NYERERE, UMEME KILA KIJIJI, HUDUMA ZA AFYA KUBORESHWA, BARABARA ZA LAMI KILA KONA, tusipoona haya hatutakuelewa.

Dr Nchemba usiende kuingia kwenye mtego wa wafanyabiashara wakwepa kodi wanaotaka uwafutie kodi zote alafu hizo kodi uwarundikie watanzania masikini mama ntilie na machinga kama ilivyokuwa zamani unakuta mfugaji au mkulima analipa kodi 10 ili amfikishe Ng'ombe wake mnadani, hatutarajii hili kutokea.
Dr Nchemba umejionea mwenyewe ulivyotukanwa na kuchambwa sana baada ya uteuzi wako na wakwepa kodi ( Chadema) wasiolitakia mema taifa hili kwao hata miradi yote ikikwama ni sawa tu, kwa hiyo hao siyo wenzako, hata siku moja usije kusikiliza ushauri wao. Hao ni nyoka kwa taifa hili.

Dr Nchemba kwa miaka mitano iliyopita hatujaona waziri wetu wa fedha akizunguka kuombaomba Ulaya ,kwa hiyo hatutarajii kukuona kila siku upo uwanja wa ndege unaenda kutembeza bakuri.

Dr Nchemba kwa miaka mitano iliyopita tumeambiwa Tanzania ni tajiri na watanzania tunaweza , hatutarajii waziri wetu mpya uanze kuimba Tanzania ni masikini na hatujiwezi kwa lolote ,ukifanya hivyo watanzania hatutakuelewa
Umekuwa kama Vuvuzela sasa!!
 
Watufutie madeni
Wengine tunashindwa anzisha biashara sababu ya TRA wanatudai
 
Na sie tuliopiganisha fedha za Miradi zilipoingia wakachukua na kuzihamishia BOT hadi tupeleke proposal tulizoombea hizo fedha nke nasi watutolee tamko tuanze kufufua NGO zetu
 
Kidoooooooooogooo!!!!!!!
Weeee ulisikia wapiiiii......
Naanza kuwa na matumaini kwa sasa
 
Sizani kama ni TRA pekee.

TRA wanapewa maagizo.

Mfano kile kitengo kilichoanzishwa cha hazina ambapo wafanyabiashara walikaguliwa hesabu zao kuanzia miaka ya nyuma sana .

Walikuwa wanakagua VAT mahsusi.

Hapa Somo ni wafanyabiasha kuwa wakweli na waminifu wakati wote waache kukwepa kulipa kodi stahiki.
 
Waziri angemalazia kuwataka wafanyabiashara kutunza kumbukumbu. Mataifa yaliyoendelea kumbukhmbu muhimu ndio maana kuna idara za masijala. 2005 karibu tu hapo mtu hata za 2016 hana sababu haikuwekwa sheria nzuri ya kumbukumbu
Hata mm nilishangaa hiyo statement yake ya kutohitaji kumbukumbu. Biashara gani itaendeshwa bila kumbukumbu? Bila kumbukumbu hizo itakuwaje sales volume na kodi iliyolipwa? Maajabu sana.
 
Back
Top Bottom