Lyambalyetu
JF-Expert Member
- Apr 6, 2021
- 261
- 235
Weekend hii Dr. Mwigulu amekumbuka kwenda kutoa shukrani jimboni kwake na kama kawaida kaendelea kuongea misamiati ya KiNyiramba huku akiwaona wasikilizaji wake kama hawana uelewa wowote ule.
Pamoja na kukwepa kugusia mambo ya kodi ya miamala lakini agenda kubwa ilikuwa ni kujiimarisha jimboni kwa kuongea hadaa nyingi za kujionesha yeye ndiye kila kitu jimboni wakati kwa miaka yake hii 11 hamna jambo amelifanya jimboni hata Taifani linalompa sifa kuwa yeye ni kiongozi mzuri.
Dr. Mwigulu uzuri wake ni ule wa kujibizana mitandaoni na kutetea hoja zisizo za maana ili kujikomba kwa viongozi. Hili,linaanza kuonekana vema baada ya kuonekana mapungufu makubwa yaliyopo katika Bajeti ya Mwaka huu ambayo inasmekana bajeti ya kujenga barabara ni shilingi milioni 500 tu.
Pamoja na kuanza ukwepa kujiita mamba aliyepo kwenye kina kirefu Dr. Mwigulu ameonge maneno mengi yanayoashiria kutamani kuongoza jimbo kwa miaka 20 ijayo. Hii ni pamoja na kuanzisha mkakati wa kuhamisha makao makuu ya Wilaya kutoka Kiomboi na kuyaleta mahali alipojenga nyumba yake barabara ya kuelekea Shinyanga na Tabora.
Pamoja na kukwepa kugusia mambo ya kodi ya miamala lakini agenda kubwa ilikuwa ni kujiimarisha jimboni kwa kuongea hadaa nyingi za kujionesha yeye ndiye kila kitu jimboni wakati kwa miaka yake hii 11 hamna jambo amelifanya jimboni hata Taifani linalompa sifa kuwa yeye ni kiongozi mzuri.
Dr. Mwigulu uzuri wake ni ule wa kujibizana mitandaoni na kutetea hoja zisizo za maana ili kujikomba kwa viongozi. Hili,linaanza kuonekana vema baada ya kuonekana mapungufu makubwa yaliyopo katika Bajeti ya Mwaka huu ambayo inasmekana bajeti ya kujenga barabara ni shilingi milioni 500 tu.
Pamoja na kuanza ukwepa kujiita mamba aliyepo kwenye kina kirefu Dr. Mwigulu ameonge maneno mengi yanayoashiria kutamani kuongoza jimbo kwa miaka 20 ijayo. Hii ni pamoja na kuanzisha mkakati wa kuhamisha makao makuu ya Wilaya kutoka Kiomboi na kuyaleta mahali alipojenga nyumba yake barabara ya kuelekea Shinyanga na Tabora.