Mwezi wa saba sasa unaingia shule hazijafungwa toka Januari 17

HOPEfull

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
1,716
2,057
Salama jamani.

Huu mwaka 2022 kiboko naona walimu watakuwa wamechoka sio kwa hali hii tunayoenda nayo.

Nahic hata wanafunzi nao watakuwa hoi bin taabani.

Toka January hakuna kupumzika mpaka leo. Hapa kati mwezi wa nne kidogo kulikuwa na vimapumziko vya hapa na pale lkn kifupi ngoma imekuwa ngumu mwaka huu.

Na inaelekea hii ngoma itadunda hadi mwezi wa saba mwishoni naona walimu watakuwa hoi.

Kupumzika ni muhimu ili kujenga afya ya mwili na akili.

Basi niwaombe walimu kitu ..Kuna kipindi waziri mmoja alitoa tamko kuwa wakati wa likizo wanafunzi wapumzike pamoja na walimu.

Kusiwepo na masomo ya ziada watoto waende nyumbani kupumzika ili kulinda afya zao, vile viratiba mnavyojiwekea walimu wakati wa likizo vinatakiwa vife ili kuwezesha wanafunzi na ninyi wenyewe mpumzike.

Kuna viratiba vya usafi kwa wanafunzi pia kuna viratiba vya masomo kwa baadhi ya madarasa.

Sijui inakuwaje wakati wa likizo lakini bado unawaona wanafunzi wanaenda shuleni na mafagio wanaenda kufagia.Sijui maana ya kupumzika hapo.Maana ya likizo ni kuwa hutakiwi hata kuliona eneo lako unalofanya kazi au kusoma.Yaani unakuwa 'free mind' hata dhararu wakati mwingine hazitakiwi,likizo ni likizo jamani.

Nenda kapumzike ufikirie na mambo mengine. Pumzisha akili kidogo na yale mambo ya kuamka asubuhi kurudi jioni au usiku.

Sasa mwaka huu inaenda robo tatu mwaka shule hazifungwa ni hatari kwa afya. Ni muhimu kupumzika wapendwa.

Kuna baadhi ya shule unakuta wanafunzi wanaingia asubuhi saa moja wanatoka saa 11 jioni, wengine saa 10 wengine saa 9.Sijui kama kuna wa mpaka saa 12.

Na sijui kama wanaelewa au hilo nawaachia wenyewe.
 
Wewe ni mzazi au mlezi au nani ambae hujui ratiba ya kufunga shule ya mtoto wako....shule zinafungwa mwisho wa mwezi huu na watoto watakuwa likizo August yote....
 
Kwani Mkurugenzi hufahamu uwepo wa zoezi la Sensa ya watu na makazi mwaka huu!

Walishajiandaa mapema kisaikolojia. Ni hofu zako tu. Ila wahusika wenyewe wanapambana kama kawaida tu huko mashuleni.
 
Mda wa kazi ni saa 1 Hadi 3:30 jikoni,siku za kazi jumatatu Hadi ijumaa,hayo mengine ni ujinga wa......
 

Serikali Mapema Ilitoa Ufafanuzi Kuwa Mwaka Huu Kutokana Na Ratiba Ya Sensa, Ratiba Zitakuwa Tofauti Kidogo Huko Shuleni, Vyuoni

Julai Mwishoni Watafunga Shule Kwaajili Ya Sensa
Shule Zitafunguliwa Mwezi Wa Tisa Halafu Baadaye Watafunga Week Moja
Baadaye Desemba Tena


Hii Inafanyika Kutoa Nafasi Kwa Zoezi La Sensa
 
Salama jamani.

Huu mwaka 2022 kiboko naona walimu watakuwa wamechoka sio kwa hali hii tunayoenda nayo.

Nahic hata wanafunzi nao watakuwa hoi bin taabani.

Toka January hakuna kupumzika mpaka leo. Hapa kati mwezi wa nne kidogo kulikuwa na vimapumziko vya hapa na pale lkn kifupi ngoma imekuwa ngumu mwaka huu.

Na inaelekea hii ngoma itadunda hadi mwezi wa saba mwishoni naona walimu watakuwa hoi.

Kupumzika ni muhimu ili kujenga afya ya mwili na akili.

Basi niwaombe walimu kitu ..Kuna kipindi waziri mmoja alitoa tamko kuwa wakati wa likizo wanafunzi wapumzike pamoja na walimu.

Kusiwepo na masomo ya ziada watoto waende nyumbani kupumzika ili kulinda afya zao, vile viratiba mnavyojiwekea walimu wakati wa likizo vinatakiwa vife ili kuwezesha wanafunzi na ninyi wenyewe mpumzike.

Kuna viratiba vya usafi kwa wanafunzi pia kuna viratiba vya masomo kwa baadhi ya madarasa.

Sijui inakuwaje wakati wa likizo lakini bado unawaona wanafunzi wanaenda shuleni na mafagio wanaenda kufagia.Sijui maana ya kupumzika hapo.Maana ya likizo ni kuwa hutakiwi hata kuliona eneo lako unalofanya kazi au kusoma.Yaani unakuwa 'free mind' hata dhararu wakati mwingine hazitakiwi,likizo ni likizo jamani.

Nenda kapumzike ufikirie na mambo mengine. Pumzisha akili kidogo na yale mambo ya kuamka asubuhi kurudi jioni au usiku.

Sasa mwaka huu inaenda robo tatu mwaka shule hazifungwa ni hatari kwa afya. Ni muhimu kupumzika wapendwa.

Kuna baadhi ya shule unakuta wanafunzi wanaingia asubuhi saa moja wanatoka saa 11 jioni, wengine saa 10 wengine saa 9.Sijui kama kuna wa mpaka saa 12.

Na sijui kama wanaelewa au hilo nawaachia wenyewe.
Umenena Mkuu.
kwakweli ratiba za masomo kwa wanafunzi mwaka huu zimebana sana kutokana na zoezi la SENSA, hivyo wenye dhamana ya Elimu/ Waziri wa Elimu anapaswa atoe maelekezo kwa ajili ya kulinda afya ya akili kwa watoto haswa wanafunzi wa darasa la 7 ambao kimsingi walipaswa wafanye mitihani yao mwezi wa 9 na sasa kupelekwa mwezi wa 10, kwa hili hakuna shida, ila mwezi wa nane uwe mwezi wa mapumziko kweli kusiwe na tution.
 
Wewe ni mzazi au mlezi au nani ambae hujui ratiba ya kufunga shule ya mtoto wako....shule zinafungwa mwisho wa mwezi huu na watoto watakuwa likizo August yote....
Swala ni kupumzika kufuatana na muda muafaka, Kama utapitiliza muda ambao ulitakiwa kuwa kwenye mapumziko hiyo inaleta negative effect kwa mwalimu kuweza ku deliver ipasavyo na mwanafunzi kuweza kuelewa. Ndicho mtoa mada anachojaribu kueleza hapa.
 
Back
Top Bottom