Mwezi mmoja ni wa dalali, madalali hii tabia mmeitoa wapi?

Huo utoto sifanyi, kuna dalali nilimpa kazi nikatia wese kwa boda boda yake siku 2 anizungushe kucheki nyumba.

Nilifanikiwa kupata mjengo kwa 150k, nikamshikisha hela nusu landlord nikamwambia siku nakuja hamia nitamalizia nusu. Hio siku nawasili kukatokea zali kumbe nyumba ile jamaa alipokea hela mara 2...ikabidi anifaulishe tu kwenye nyumba ya 250k kwa kodi ya 200k nikaongezea hela kidogo nikaingia.

Ishu ikaja kwa dalali baada ya kujua nimelipia tayari akadai nimpe hela ya mwezi mzima nikawaza nampaje mtu 150k usawa huu? Nilichofanya nikamshikisha 50k kisha nikamsokota anicheki baada ya siku 10 hivi nimalizie hela. Zilipofika akaanza sumbua nikamtia block tu maana hakukuwa na namna.
nilishafanya hivi hata mimi,

sema mimi nilipo pata nyumba nikaipenda nikajitia sijaipenda tukasepa

nikampa buku 5 ya usumbufu,akapita hivi na mimi vile

usiku nikarudi kwa maza house nimeshajikamilisha nikamtia kodi yake yote

Akanipa funguo nikasepa zangu,nikajaga nikahamia

Baada ya siku mbili tu nkaskia usiku nagongewa mlango na maza house

Kutoka nnje namkuta maza na dalali,kikao cha dharura kikaitishwa

Dalali anadai anataka hela yake ya mwezi,mimi nasema sina hata sh 10

Maza house yupo upande wa dalali...nikaja nikakata mzizi wa fitna nikamwambia bi mkubwa

Naomba nirudishiwe kodi yangu nihame....Ah weeeeee kusikia hivyo Kikao kikaishia angani

Niliambiwa ebu we D nenda ntakuita..sikuitwa mpaka na kesho kutwa.
 
Yaani madalali wa siku hizi eti akikutafutia nyumba anakwambia umpe mwezi mmoja wake

Mfano appartment ya laki 1 na 50 kwa mwezi anataka umpe laki 1 na 50 kama malipo...hapo kukutembeza kwenye nyumba ni elfu 20

Yaani mfano unatafuta nyumba ya kodi ya laki 2 jiandae kuweka laki mbili ya dalali juu na elfu 20 ya kukutembeza kwenye nyumba


Hawa ndo madalali bwana jee hii ni sawa??hapana huu ni unyonyaji anaepaswa kumlipa dalali ni mwenye nyumba sio mteja....

Nisameheni sana madalali ila ndo ukweli huo
Mnawadekeza. mwambie masharti yako mapema atakuelewa. Mimi huwa sitoi ile hela ya kunipeleka kwenye nyumba, namwambia mapema kabisa. na ile commission nampangia
 
nilishafanya hivi hata mimi,

sema mimi nilipo pata nyumba nikaipenda nikajitia sijaipenda tukasepa

nikampa buku 5 ya usumbufu,akapita hivi na mimi vile

usiku nikarudi kwa maza house nimeshajikamilisha nikamtia kodi yake yote

Akanipa funguo nikasepa zangu,nikajaga nikahamia

Baada ya siku mbili tu nkaskia usiku nagongewa mlango na maza house

Kutoka nnje namkuta maza na dalali,kikao cha dharura kikaitishwa

Dalali anadai anataka hela yake ya mwezi,mimi nasema sina hata sh 10

Maza house yupo upande wa dalali...nikaja nikakata mzizi wa fitna nikamwambia bi mkubwa

Naomba nirudishiwe kodi yangu nihame....Ah weeeeee kusikia hivyo Kikao kikaishia angani

Niliambiwa ebu we D nenda ntakuita..sikuitwa mpaka na kesho kutwa.
Good plan
 
Me nadhani ofisi za serikali za mitaa zingechangamkia hii fursa. Kila mwenye nyumba ya kupangisha angetakiwa kuripoti ofisi ya Kata na vielelezo kamili vya nyumba yake, na wateja nao wasingehangaika wangekua wanakwenda moja kwa moja kwa mtendaji kuuliza kama kuna nyumba inapangishwa. Yangekuwepo malipo kidogo mfano 10% kwa ajili ya ofisi
 
Sijawahi na sitawahi mpa dalali ela ya mwezi aisee wakijaga wanachezea maneno anapewa robo ya kodi tena akilegea tu ndoapewi kabisa
kwa sauti hiyo ya madeko

dalali ataekumbuka kudai hela yake

ana moyo mgumu sana
 
Mbona hiii haijaanza leo Ni kitu Cha mda mrefu tu mkuuu... Ulitaka Dalali ale wapi...aua ulitaka kumlipa Nini?
 
Me kwanza kabla ya kutafuta nyumba namwambia nahitaji nyumba ya aina gani na maeneo gani,ndo anakula pesa ya kutembea na haizidi buku 5.maana unamwambia unataka nyumba ya laki 150 yeye anakupeleka nyumba za milioni kwa mwezi,pesa yangu hali.
 
Me nadhani ofisi za serikali za mitaa zingechangamkia hii fursa. Kila mwenye nyumba ya kupangisha angetakiwa kuripoti ofisi ya Kata na vielelezo kamili vya nyumba yake, na wateja nao wasingehangaika wangekua wanakwenda moja kwa moja kwa mtendaji kuuliza kama kuna nyumba inapangishwa. Yangekuwepo malipo kidogo mfano 10% kwa ajili ya ofisi
Hii ingekuwa nzuri sana
 
Kwa nchi za wenzetu , udalali ni kazi official kama kazi nyingine inayotambulika , husajiliwa na kutoa huduma kwa usawa kabisa , bila kumuumiza mwenye mali.

Madalali ambao ni matapeli na wahovyo sana ni hawa wa nyumba , viwanja /mashamba na mazao ya kilimo.

Madalali wa mazao ya kilimo ni wanyonyaji sana kwa wakulima. Hupanga bei wao.


Wanakwenda shambani kupanga bei wao as if wamelima wao , mnunuzi anapokuja wanamdaka sana juu kwa juu. Mkulima ni vigumu sana kumwona tajiri , wao ndo wao tu.

Kuna mahali nilinunua kiwanja, baadae nikaja kusikia pesa aliyopiga dalali ni ndefu sana.

Madalali hula pesa ya bure.

Ni watu wa hovyo sana hawa , matapeli wakubwa.

Pls share utapeli wa madalali.
Wengi wao washirikina wakutupwa.
 
Sasa napata jibu.
Dalali kaleta mtu na makubaliano yamefikiwa aje kulipa kesho kutwa. Lakini hakuacha kuleta watu kuja kuangalia nyumba. Kumbe kuna ya kuwaonyesha. Mjini akili sii manguvu.
 
Back
Top Bottom