Juzi nilipokuwa napitia malengo niliyojiwekea mwaka huu nikagundua kuna vitu viwili nilitarajia kuvifanya mwaka huu. Nilitarajia kuwa na shamba la migomba, mpaka jioni ya juzi nilikuwa sijaweza.Nilitarajia kuwa na shamba la nyuki la kisasa, nimekosa location nzuri.
Ili kuondoa nuksi, leo nimewaomba vijana wangu waoteshe migomba minne mchana wa leo, na nimenunua mizinga mitano ya kisasa ili iwe chachu ya kutimiza ndoto zangu mwakani, kwa hiyo tayari nimeanza mwendo wa kutimiza ndoto zangu.
Zaidi sana namshukuru Mungu alivyonilinda na kunijalia afya kwa mwaka huu, niwashukuru wanajamvi wenzangu kwa kushirikiana vema. Tumshukuru Mungu kwa yote, tuwe tumefanikiwa au hatukufanikiwa, maadamu hatukulala, yote ni heri.
Ili kuondoa nuksi, leo nimewaomba vijana wangu waoteshe migomba minne mchana wa leo, na nimenunua mizinga mitano ya kisasa ili iwe chachu ya kutimiza ndoto zangu mwakani, kwa hiyo tayari nimeanza mwendo wa kutimiza ndoto zangu.
Zaidi sana namshukuru Mungu alivyonilinda na kunijalia afya kwa mwaka huu, niwashukuru wanajamvi wenzangu kwa kushirikiana vema. Tumshukuru Mungu kwa yote, tuwe tumefanikiwa au hatukufanikiwa, maadamu hatukulala, yote ni heri.