Je, hizo kesi alizofuta zilikuwa na uhalali wowote?!Labda ameanza kuwa katili kwa kuwa kaona hamna shukrani. Kawafutia kesi kina Mdude mkaanza kumtukana ndio maana kawaacha vijana wake waseme nyie ni magaidi
Kama zilikuwa na uhalali, kwanini azifute?! Na kwavile kesi ya Mdude ilitolewa uamuzi na mahakama, ina maana Rais alitumia madaraka yake vibaya kuingilia uhuru wa mahakama na kuitaka mahakama ifute kesi iliyokuwa na uhalali kisheria?
Na kama hiyo kesi haikuwa na uhalali wowote, basi hapo hapakuwa na sababu yoyote ya kuwataka watu washukuru kwa sababu, tangia hapo kesi yenyewe haikutakiwa kuwepo!!