Hali ya kisiasa Njombe imeanza kuharibika baada ya jana mwenyekiti wa tawi la Manga kata ya Mahongole(Njombe kaskazini) kukamatwa na kuwekwa kizuizini bila kuwa na nguo mwilini. Kitendo hicho kilifanywa na mwenyekiti wa CCM kijiji cha Manga. Alipigwa kama mbwa na kuwekwa ndani siku nzima hadi pale viongozi wa CHADEMA wilaya ya Njombe walipofika na kufanya mipango ya kumwokoa.
Sababu ya kuwekwa ndani ilikuwa ni kitendo cha kufanya maandalizi ya mkutano wa CHADEMA ambapo ulipangwa kufanywa tarehe 12.8.2012. Baada ya kuokolewa ndani ya Lupango kwenye ofisi ya kijiji viongozi wa CHADEMA waliamua kumpeleka moja kwa moja hospitalini ambako amelazwa hadi sasa.
Leo CHADEMA tayari kimefungua kesi katika mahakama ya wilaya ya Njombe kwa makosa makubwa mawili ya udhalilishaji (defamation) ambayo ni Kuwekwa ndani kwa muda mrefu bila uwezo wa kisheria kufanya hivyo na kosa la pili ni kosa la udhalilishaji (libel). Katika makosa hayo mshitakiwa anatakiwa kulipa 50 milioni.
Pia chama kimemfungulia kesi mwenyekiti huyo wa CCM kesi jinai (criminal) kutokana na kitendo chake cha kushusha bendera ya CHADEMA na kuzichana kinyume cha sheria. Njombe kaskazini ni moja ya majimbo ambayo yanaongozwa na wanasiasa wa aina yake duniani (majah).
Sababu ya kuwekwa ndani ilikuwa ni kitendo cha kufanya maandalizi ya mkutano wa CHADEMA ambapo ulipangwa kufanywa tarehe 12.8.2012. Baada ya kuokolewa ndani ya Lupango kwenye ofisi ya kijiji viongozi wa CHADEMA waliamua kumpeleka moja kwa moja hospitalini ambako amelazwa hadi sasa.
Leo CHADEMA tayari kimefungua kesi katika mahakama ya wilaya ya Njombe kwa makosa makubwa mawili ya udhalilishaji (defamation) ambayo ni Kuwekwa ndani kwa muda mrefu bila uwezo wa kisheria kufanya hivyo na kosa la pili ni kosa la udhalilishaji (libel). Katika makosa hayo mshitakiwa anatakiwa kulipa 50 milioni.
Pia chama kimemfungulia kesi mwenyekiti huyo wa CCM kesi jinai (criminal) kutokana na kitendo chake cha kushusha bendera ya CHADEMA na kuzichana kinyume cha sheria. Njombe kaskazini ni moja ya majimbo ambayo yanaongozwa na wanasiasa wa aina yake duniani (majah).