Kuuli ameyasema hayo wakati wa mahojiano na Mwandishi wa habari aliyetaka kusikia kauli yake baada ya Katibu Mkuu wa TFF, kidao Wilfred kumwandikia barua kumtaka ajieleze wapi ametoa mamlaka ya kusitisha uchaguzi wa timu ya Simba. Kuuli alisitisha uchaguzi wa Simba hadi watakaporekebisha kasoro za mchakato wa uchaguzi ikiwa ni pamoja na gharama za uchukuaji fomu ambazo haziendani na zile zilizoainishwa kwenye Katiba.