Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
cdm ikifika 2015 najiua
Nina wasiwasi na akili zako.
Hebu chungulia signature ya Invisible, itakusaidia.
cdm ikifika 2015 najiua
dhibitisha kauli yako ndg.
Mkuu, unauliza swali ambalo mwenyewe ulishalitolea majibu kwamba "amechoshwa na udanganyifu ulioko CHADEMA" Nadhani mimi na wengine wanaotaka kujua zaidi ndio tunaotakiwa tukuulize wewe. Ni udanganyifu upi huo? Hebu tudokeze tupate kujua pia.
Njaa, Nooooma!!!
Kweli jamaa njaa kali, mimi nimeangalia hilo tukio kwenye sumbawanga tv jioni ya leo, (NI KITUO CHA UMMA-MANISPAA) walikuwepo wakuu wilaya watatu, wabunge, wakuu wa idara mbalimbali nimemuona afsa elimu manispaa ya Sumbawanga ndugu Maulidi. mwenyekiti wa ccm mkoa ndg matete katoa utangulizi eti usumbufu wote toka CDM kwa CCM huyo njaa mbaya ndiye chanzo na kuwa wamebomoa ngome ya Chadema sumbawanga kitu ambacho si kweli Chadema iko imara sana Sumbawanga na itaendelea kuwa imara zaidi na huyo jamaa hakuwa na mchango wowote wa kujutia kutoka kwake, baadaye jamaa alikuwa kawekwa nje akaitwa na kukabidhi kadi ya CDM then akapewa nafasi ya kuongea, maongezi yalikuwa kuponda Wabunge wa CDM kwa kutoka nje ya bunge na kumtetea mbunge wa Sumbawanga mjini bw Aisha, katika maelezo yake kajamaa kenyewe ni kazawa ka Moshi kamekiri kenyewe kalihamia Sumbawanga kutafuta posho, biashara zikakashinda na mwaka 2005 kakaingia kwenye siasa uchwara za kinafiki na za maslahi binafsi na baada ya kuona CDM hakuna posho ikawa shida kwake, binafsi ilinishangaza pale wajumbe waliponyenyuka ghafla wakiongozwa na Mkuu wa wilaya ya sumbawanga ndg Mzurikwao na kwenda kumkumbatia huku akipewa pesa,walionekana Meya wa manispaa,bw Aisha na wengine wengi waliokuwepo jamaa kama njaa leo yuko fiti na X mas itakuwa poa kwani kwa haraka tu kajamaa kamevuna sichini ya 50 elfu, zaidi Stela Manyanya alipokaribishwa kuongea alikiri kuwa atatumia nguvu zake zote kuhakikisha CCM inaimarisha Rukwa na kuwa ndo moja kazi ya kuletwa Rukwa!njaa mbaya sana
bw. Geophrey shayo mwenyekiti wa chadema sumbawanga amechoshwa na udanganyifu ulioko chadema ameamua kurudi ccm.
Amepewa kadi ya ccm na eng stella manyanya mkuu wa mkoa wa rukwa..
Kuna nini huko chadema acheni kudanganya wanachama???
Source: Michuzi blog
tunadanganywa nn....acha atembee...atarudi na magoti mikono nyuma..ccm wanahangaika na chadema,hii ni kutokana na kushindwa kutekeleza ahadi za mwenyekit wao..chadema ni taasisi si watu.
matomato anatafuta kufanyiwa kama yule DC!Akitoka mnafiki mmoja wanaingia wanachama wakweli 1000 shida iko wapi,Mkuu wa mkoa kumbe kazi yake kugawa kadi na kuchukua kadi za vyama pinzani? Ameshamaliza kazi zote za kuhamasisha maendeleo mkoani kwake? mbona barabara na kipato cha wananchi bado duni sana si angetumia muda huo kujadili bei ya mazao ya wakulima?
Bw. Geophrey Shayo mwenyekiti wa CHADEMA sumbawanga amechoshwa na udanganyifu ulioko chadema ameamua kurudi ccm.
Amepewa kadi ya ccm na Eng Stella Manyanya mkuu wa mkoa wa rukwa..
Kuna nini huko chadema acheni kudanganya wanachama???
Source: Michuzi blog