Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa mara Vincent Nyerere aizidi kete CCM

otorokoko

JF-Expert Member
Feb 2, 2012
2,437
154
Mwenyekiti wa chadema mkoa wa mara na pia mbunge wa jimbo la musoma mjini amezidi kuiteketeza ccm katika mkoa wa mara katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.Siku ya jana alifanya ziara ya kuwanadi wagombea katika vijiji sita ikiwemo wilaya ya bunda na musoma vijijini,wagombea wa upinzani wamekuwa tishio hali iliyopelekea baadhi ya wanachama wa ccm kukata tamaa ya kupata ushindi katika mitaa yao
 
Team ukawa,wassira ajitathmini mapema kabla ya nguvu ya umma haijamtoa kwa mapambano yasiyo na mwisho
 
Wassira hana chake mitaa chadema inamnyoosha na ubunge ester bulaya anamnyoosha
Ester Bulaya anafahamika Bunda Mjini tu. Hajulikani Bunda vijijini na ana kazi kubwa sana ya kuwafanya wana Bunda wa maeneo mengine ya Bunda wamfahamu,namshauri aende viti maalum kuliko akijirengesha kwenye jimbo either kwa upinzani au kwa chama chake,alitakiwa apate support ya Wasira kuliko anayompinga.

Kamanda hachagui kichaka cha kupigania yeye kichaka chochote anavamia na anashinda vita
Hivi kwenye uchaguzi wa udiwani kata ya Nyasura nani aliibuka kidedea? Vincent haiwezi Bunda - ataishia kipata umati wa watu Bunda Mjini na Tarime tu.
 
Sijawahi kuona ccm wanakodi helicopter wiki mbili Wilaya moja lakini, bado muziki mzito

hata walete helicopter nane kupigwa chini kuko palepale,wananchi wanaangalia sera kama ingekuwa ni kuchagua helicopter si wangekipa dhamana kiwanda cha kutengeneza helicopter kiwaongoze
 
Ester Bulaya anafahamika Bunda Mjini tu. Hajulikani Bunda vijijini na ana kazi kubwa sana ya kuwafanya wana Bunda wa maeneo mengine ya Bunda wamfahamu,namshauri aende viti maalum kuliko akijirengesha kwenye jimbo either kwa upinzani au kwa chama chake,alitakiwa apate support ya Wasira kuliko anayompinga.

Hivi kwenye uchaguzi wa udiwani kata ya Nyasura nani aliibuka kidedea? Vincent haiwezi Bunda - ataishia kipata umati wa watu Bunda Mjini na Tarime tu.

Bunda ni eneo zaidi la vijijini, ni kweli Esther anatakiwa kwenda vijijini, Ila Nyasura hakuna asiyejua nini kilifanyika
 
Ester Bulaya anafahamika Bunda Mjini tu. Hajulikani Bunda vijijini na ana kazi kubwa sana ya kuwafanya wana Bunda wa maeneo mengine ya Bunda wamfahamu,namshauri aende viti maailum kuliko akijirengesha kwenye jimbo either kwa upinzani au kwa chama chake,alitakiwa apate support ya Wasira kuliko anayompinga.

Hivi kwenye uchaguzi wa udiwani kata ya Nyasura nani aliibuka kidedea? Vincent haiwezi Bunda - ataishia kipata umati wa watu Bunda Mjini na Tarime tu.

Ester Bulaya ni mtu mmoja hatari sana ambaye wassira akimsikia huwa anatetemeka kama kapigwa shoti,ester bulaya ananitandikia huyu mtu mapema
 
Huyu jamaa vicenti baba yake anaitwa kiboko lakini hajawahi kutaja jina la baba yake sijui anasumbuliwa na nini.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom