Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Bagamoyo Mathayo Torongei anashikiliwa na Polisi kwa zaidi ya siku 7 bila kupelekwa Mahakamani, kinyume cha sheria

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,643
218,099
FB_IMG_1607279426808.jpg


Hii ndio taarifa iliyozagaa Mkoani Pwani baada ya Jeshi la Polisi Mkoani humo kumkamata kwa style ya kumteka Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Bagamoyo Mh Mathayo Torongei na kumnyima dhamana kwa zaidi ya siku 7 na kugoma kumpeleka Mahakamani , jambo ambalo ni kinyume cha sheria za nchi .

Mpaka sasa haijulikani kosa lake na wala haifahamiki sababu hasa za Polisi kuvunja sheria za nchi kwa kumshikilia bila kumpeleka Mahakamani .
 
Kama kawaida yako mkuu na habari zako,yani unaona kusema tu sababu za yeye kukamatwa ni kama habari yako itakosa mvuto

any way wamekusikia✌💪✌👏
 
Akamatwe tu bila sababu?
Cdm mnapenda kudekaaa
Yaani msichukuliwe hatua Kama mmekosea
Mnaanza kulilalia kwa wananchi
 
Akamatwe tu bila sababu?
Cdm mnapenda kudekaaa
Yaani msichukuliwe hatua Kama mmekosea
Mnaanza kulilalia kwa wananchi
Lissu alipouawa kwa maagizo kutoka juu kwa kutandikwa risasi 38 sababu zake uliambiwa ?
 
Back
Top Bottom