nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
** Why is this CCM now they have to use religious books to prove it's existance? The trouble ain't that there is too many fools, but that the lightning ain't distributed right!!!
Na Nathaniel Limu-Singida.
Mwenyekiti wa CCM Singida vijijini Narumba Hanje, amekitabiria Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwamba hakitaingia Ikulu milele kwa madai kuwa kimepoteza mwelekeo baada ya kuanza kutumia mbinu chafu ambazo hazitawasaidia kufikia lengo lao.
Hanje ametoa utabiri huo wakati akifungua mkutano mkuu wa Jumuiya ya umoja wa vijana (UVCCM) uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa shirika la Pride Singida Mjini.
Alisema CHADEMA sasa kimeacha kuwaeleza wananchi kitawafanyia nini ili waweze kuleta maendeleo endelevu, na badala yaje kueneza fitina, hasira, uadui, uzushi.
Aidha, Hanje amedai kuwa Chama hicho kimeundwa, kiundugunaizesheni na kwamba hakina demokrasi na kuwa na mwonekano wa taasisi binafsi, na kuongeza kuwa kimepoteza muda mwingi kwa kuzunguka na kufanya maandamano ambayo hayana tija kwa wananchi.
Mwenyekiti huyo amedai chama hicho kimeonyesha dhahiri kwamba hakiwatakii mema Watanzania baada ya kuanza kuwadanganya na kuwashawishi wasichangie maendeleo kwa madai kwamba jukumu la kuleta maendeleo ni la serikali pekee.
Sisi hapa mjini, tunachangia mambo mengi hata ya uzoaji wa takataka, sembuse maendeleo, alihoji na kuongeza CHADEMA hawana ubavu tena wa kuchukua nchi, wamepoteza mwelekeo, wamefikia mahali wanaifananisha Tanznaia na Misri.
Hanje alisema CHADEMA ni ya kuogopwa kama ukoma, kwa madai kwamba viongozi wa chama hicho,wanatumia nafasi zao kujaza watu wa ukoo wao katika nafasi mbali mbali za uongozi.
Katika kuujengea nguvu utabiri wake huo, mwenyekiti huyo alisoma Agano jipya kitabu cha Wagalatia 5 mstari mdogo kuanzia 19-21.
Pamoja na mambo mengine, mistari hyo inasema Fitina, wivu, hasira, husuda na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo, nawaambia kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo, hawataurithi ufalme wa Mungu.
Mwenyekiti wa CCM Singida vijijini, Narumba Hanje akisoma Agano jipya kitabu cha Wagalatia mbele ya mkutano mkuu wa UVCCM Singida vijijini juzi.
Na Nathaniel Limu-Singida.
Mwenyekiti wa CCM Singida vijijini Narumba Hanje, amekitabiria Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwamba hakitaingia Ikulu milele kwa madai kuwa kimepoteza mwelekeo baada ya kuanza kutumia mbinu chafu ambazo hazitawasaidia kufikia lengo lao.
Hanje ametoa utabiri huo wakati akifungua mkutano mkuu wa Jumuiya ya umoja wa vijana (UVCCM) uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa shirika la Pride Singida Mjini.
Alisema CHADEMA sasa kimeacha kuwaeleza wananchi kitawafanyia nini ili waweze kuleta maendeleo endelevu, na badala yaje kueneza fitina, hasira, uadui, uzushi.
Aidha, Hanje amedai kuwa Chama hicho kimeundwa, kiundugunaizesheni na kwamba hakina demokrasi na kuwa na mwonekano wa taasisi binafsi, na kuongeza kuwa kimepoteza muda mwingi kwa kuzunguka na kufanya maandamano ambayo hayana tija kwa wananchi.
Mwenyekiti huyo amedai chama hicho kimeonyesha dhahiri kwamba hakiwatakii mema Watanzania baada ya kuanza kuwadanganya na kuwashawishi wasichangie maendeleo kwa madai kwamba jukumu la kuleta maendeleo ni la serikali pekee.
Sisi hapa mjini, tunachangia mambo mengi hata ya uzoaji wa takataka, sembuse maendeleo, alihoji na kuongeza CHADEMA hawana ubavu tena wa kuchukua nchi, wamepoteza mwelekeo, wamefikia mahali wanaifananisha Tanznaia na Misri.
Hanje alisema CHADEMA ni ya kuogopwa kama ukoma, kwa madai kwamba viongozi wa chama hicho,wanatumia nafasi zao kujaza watu wa ukoo wao katika nafasi mbali mbali za uongozi.
Katika kuujengea nguvu utabiri wake huo, mwenyekiti huyo alisoma Agano jipya kitabu cha Wagalatia 5 mstari mdogo kuanzia 19-21.
Pamoja na mambo mengine, mistari hyo inasema Fitina, wivu, hasira, husuda na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo, nawaambia kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo, hawataurithi ufalme wa Mungu.
Mwenyekiti wa CCM Singida vijijini, Narumba Hanje akisoma Agano jipya kitabu cha Wagalatia mbele ya mkutano mkuu wa UVCCM Singida vijijini juzi.