CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 4,984
- 4,083
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao maalum cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kilichokutana Ikulu ya Chamwino, Jijini Dodoma leo Jumatatu tarehe 26 Septemba, 2022.
Rais wa Zanzibar na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe Dkt Hussein Mwinyi akiteta jambo na Makamu Mwenyekiti wa ccm-Tanzania visawani Mhe Dkt Ally Mohamed Shein muda mchache kabla ya kikao kuanza,
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Kanali Mstaafu Ndg Abdulrahaman KINANA akipitia makabrasha mbalimbali kabla ya kikao cha Kamati kuu Maalum,
Katibu wa NEC Itikadi & Uenezi CCM Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka akiteta jambo na Mjumbe Mpya wa Kamati Kuu Ndg Steven Masato Wassira,
Wajumbe wa Kamati kuu wakimkaribisha kwa Wimbo wa Chama Mkt wa Kikao Ukumbini,
#CCM MBELE KWA MBELE