mfalmeselemani
Member
- Sep 30, 2014
- 95
- 47
Na Ghati Chacha
HII sio Chama Cha Mapinduzi(CCM) ninachokijua na kukulia kwa zaidi ya miaka 30. Chama kilichosimama mstari wa mbele katika kuwakomboa wananchi na unyonge wao, Chama kinachosimama mbele kupinga rushwa hadharani.
Naamini na nitaendelea kuamini CCM ni taasisi kubwa na yanayoendelea kufanyika katika Mkoa wa Mara hasa majimbo ya Tarime Mjini na Vijijini ni jambo linalopaswa kukemewa na kila mpenda maendeleo na kukitakia mustakabali Chama katika kuyasisimamia maendeleo ya wananchi.
Yaliyofanywa na washindi wa kura za maoni katika majimbo ya Tarime ni wizi mkubwa na yanapaswa kukemewa kwa nguvu zote kwani haikubaliki na haitakiwi kwa CCM kushiriki kwenye ulanguzi wa kura kama uliofanywa na kina Jackson Kangoye kwa Tarime Mjini.
Kiongozi anayenunua kura hafai hata kupendwa kwani anakuwa ni mtu anayeleta dharau kwa wananchi na anaamini kura yake imetokana na rushwa na sio kitu kingine chochote.
Kwani kilichotokea Tarime ni kuuza utu pasipokuwa na sababu za msingi uliotekelezwa na watendaji kwa ajili ya masilahi binafsi ya watu wachache ambao wanakiharibu Chama kwa jimbo la Tarime Mjini ambalo viongozi wanafanya mambo ya ovyo pasipokuwepo uimara na ubora wa kuleta maendeleo kwa jamii husika.
Hivyo mbunge wa namna hiyo, hafahi na hawezi kuleta maendeleo kwa wananchi kwa kuwa anaamini huu wakati wa kurudisha hela yake na sio kuleta maendeleo jimboni.
HII sio Chama Cha Mapinduzi(CCM) ninachokijua na kukulia kwa zaidi ya miaka 30. Chama kilichosimama mstari wa mbele katika kuwakomboa wananchi na unyonge wao, Chama kinachosimama mbele kupinga rushwa hadharani.
Naamini na nitaendelea kuamini CCM ni taasisi kubwa na yanayoendelea kufanyika katika Mkoa wa Mara hasa majimbo ya Tarime Mjini na Vijijini ni jambo linalopaswa kukemewa na kila mpenda maendeleo na kukitakia mustakabali Chama katika kuyasisimamia maendeleo ya wananchi.
Yaliyofanywa na washindi wa kura za maoni katika majimbo ya Tarime ni wizi mkubwa na yanapaswa kukemewa kwa nguvu zote kwani haikubaliki na haitakiwi kwa CCM kushiriki kwenye ulanguzi wa kura kama uliofanywa na kina Jackson Kangoye kwa Tarime Mjini.
Kiongozi anayenunua kura hafai hata kupendwa kwani anakuwa ni mtu anayeleta dharau kwa wananchi na anaamini kura yake imetokana na rushwa na sio kitu kingine chochote.
Kwani kilichotokea Tarime ni kuuza utu pasipokuwa na sababu za msingi uliotekelezwa na watendaji kwa ajili ya masilahi binafsi ya watu wachache ambao wanakiharibu Chama kwa jimbo la Tarime Mjini ambalo viongozi wanafanya mambo ya ovyo pasipokuwepo uimara na ubora wa kuleta maendeleo kwa jamii husika.
Hivyo mbunge wa namna hiyo, hafahi na hawezi kuleta maendeleo kwa wananchi kwa kuwa anaamini huu wakati wa kurudisha hela yake na sio kuleta maendeleo jimboni.