Mwenyekiti wa CCM kuita gazeti la chama "vigazeti" ni kosa kubwa

Nanukuu

"Wameanza kutuchokoza, Kuandika kwenye vigazeti kuwa Samia hata gombea, nani kasema."

Hapa nadhani mwenyekiti ameteleza maana gazeti lililoandika habari hii ni gazeti la Uhuru linalomilikiwa na Chama cha Mapinduzi. Kuliita gazeti hili kigazeti ni kosa kubwa sana.

Ila kama ndiyo ameamua hivyo sawa.
Kwani hujui kuwa Uhuru ni kijigazeti? Umashatembelea newsroom yake ukajionea? In fact kwa sasa Tanzania inaonekana kama hamna gazeti tena bali ni vijigazet tu.

Ila mama samia anapenda sana vijembe vya uswahili ambavyo haiendani na hadhi yake kama kiongozi wa nchi. Hilo tamko la vijigazeti dhidi yake binafsi siyo presidential material.
 
Nanukuu

"Wameanza kutuchokoza, Kuandika kwenye vigazeti kuwa Samia hata gombea, nani kasema."

Hapa nadhani mwenyekiti ameteleza maana gazeti lililoandika habari hii ni gazeti la Uhuru linalomilikiwa na Chama cha Mapinduzi. Kuliita gazeti hili kigazeti ni kosa kubwa sana.

Ila kama ndiyo ameamua hivyo sawa.
Amelewa madaraka
 
N
Sioni kosa.

Kigazeti ni gazeti dogo.

Udogo huenda kwa umri tangu kuanzishwa, idadi ya nakala zinazochapishwa na kuuzwa, upana wa uhitaji.

Kwa vyote tajwa hapo juu, hako ni kagazeti.
Na yeye kama "mmiliki" wa hako kagazeti anakaacha ka nini? Si akaondoe tu kaache kukitia chama hasara?
 
Back
Top Bottom