Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA aliyekamatwa Zanzibar, Hashimu Issa Juma apelekwa Kisutu

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,343
217,378
Mwenyekiti_wa_Baraza_la_Wazee_%40ChademaTz_%23Bazecha_Mzee_Hashim_Issa_Juma_amechukuliwa_nyumb...jpg


Hii ndio Taarifa mpya kutoka Chadema kwa sasa, ambapo watu wasiofahamika wakiwa na bunduki wamemchukua Mzee Hashimu Issa nyumbani kwake Unguja na kuondoka naye, tena bila kusema wanampeleka wapi.

Taarifa zaidi zitaendelea kuwajia kwa kadri zitakavyotufikia.

====

UPDATES

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kumshikilia mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chadema (Bazecha), Hashimu Issa Juma kwa tuhuma za uchochezi wa kujenga chuki kati ya Serikali na wananchi.

Issa alikamatwa Oktoba 3,2021 mjini Unguja, Zanzibar kisha kushikiliwa kwa muda kabla ya kusafirishwa jana Jumatatu Oktoba 4,2021 kuletwa Dar es Salaam kwa mahojiano zaidi.

"Uchunguzi wa shauri hili unaendelea na ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani haraka iwezekanavyo," amesema Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum Dar es Salaam,Jumanne Muliro katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.

Juma ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya Chadema anadaiwa kutenda kosa hilo Oktoba Mosi,2021 wakati wa mkutano wake na wanahabari uliofanyika katika ofisi za makao makuu ya Chadema Kinondoni.

=====

Mwenyekiti wa baraza la Wazee Chadema afikishwa Mahakamani​

WhatsApp-Image-2021-10-07-at-3.27.00-PM-660x400.jpeg
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee CHADEMA Hashim Juma Issa (63), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka mawili ikiwemo kuchapisha taarifa za uchochezi kwa lengo la kumdhalilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro.

Akisoma mashtaka hayo, Wakili wa Serikali Yusuph Aboud alidai Mshitakiwa huyo alitenda makosa hayo October 1 mwaka huu mtaa wa Ufipa, Kinondoni, Dar es Salaam ambapo katika shitaka la kwanza ilidaiwa akiwa eneo hilo alichapisha taarifa ya uongo kwa njia ya kompyuta na kusambaza katika mtandao wa YouTube kwa lengo la kumchafua na kumdhalilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Simon Sirro.
WhatsApp-Image-2021-10-07-at-3.27.01-PM-1-950x713.jpeg

Ilidaiwa alichapisha kuwa ‘IGP Sirro ni gaidi namba moja hapa nchini Tanzania na fisadi’ na katika shitaka la pili ilidaiwa katika tarehe na eneo hilo, alichapisha taarifa ya uchochezi kwa lengo la kutengeneza chuki kwa Wananchi dhidi ya IGP Sirro kuwa ‘IGP Sirro ni gaidi namba moja hapa nchini Tanzania na fisadi’.
WhatsApp-Image-2021-10-07-at-3.27.01-PM-950x713.jpeg

Baada ya kusomewa mashitaka hayo upande wa mashitaka ulidai upelelezi wa kesi hiyo upo katika hatua za mwisho hivyo wapangiwe tarehe nyingine ya kutajwa na Hakimu alikubali ombi hilo na kuahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 28 mwaka huu huku Mshitakiwa akiachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana likiwemo kuwa na wadhamini wawili wenye vitambulisho vya kura au cha taifa watakaosaini bondi ya Sh.Mil 3 kila mmoja.

Pia, soma: Hashimu Juma, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee CHADEMA[BAZECHA afutiwa mashtaka na DPP
 
View attachment 1961683

Hii ndio Taarifa mpya kutoka Chadema kwa sasa , ambapo watu wasiofahamika wakiwa na bunduki wamemchukua Mzee Hashimu Issa nyumbani kwake Unguja na kuondoka naye , tena bila kusema wanampeleka wapi .

Taarifa zaidi zitaendelea kuwajia kwa kadri zitakavyotufikia .
Ameyataka mwenyewe mzee mzima ndio anashobokea siasa

USSR
 
Hata Lissu akiwa rais watu watatekwa kama kawa, KUNA SYSTEM nyuma ya rais,Ndio maana tunaoijua hii nchi, tunajua Mbowe sio Gaidi ila SYSTEM imefanyabyake, angekuwepo JPM angetupiwa kila lawama...

SAMIA awali hakuijua Vzr SYSTEM..... akataka aendeshe nchi yeye kama yeye, ndipo SYSTEM ikamuambia kina mbowe watamzid kete...

Now Mbowe yupo korokoroni.....
 
hata lissu akiwa rais watu watatekwa kama kawa, KUNA SYSTEM nyuma ya rais,Ndio maana tunaoijua hii nchi, tunajua Mbowe sio Gaidi ila SYSTEM imefanyabyake, angekuwepo JPM angetupiwa kila lawama...

SAMIA awali hakuijua Vzr SYSTEM..... akataka aendeshe nchi yeye kama yeye, ndipo SYSTEM ikamuambia kina mbowe watamzid kete...

now Mbowe yupo korokoroni.....
Kwamba Rais anaburuzwa na watu fulani siyo ?
 
Back
Top Bottom