Mwenyekiti UVCCM, Kheri James aomba radhi kwa watu wote waliokerwa na kauli yake

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899



"Nachukua nafasi hii kuwaomba Radhi Watanzania Wenzangu wote walio kerwa na ujumbe huo,na ninawashukuru viongozi wote wa kisiasa na kiraia walio nikosoa na kunikemea kwa maslahi mapana ya Taifa letu,ninawashukuru sana" Kheri James Mwenyekiti UVCCM Taifa

james.jpg


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James ametengua kauli yake inayosema ‘CCM ndiyo inayoamua maendeleo yaje au yasije na hakuna mwananchi anayeweza kuchukua hatua yoyote dhidi ya chama hicho’.

Akimnadi mgombea wa udiwani Kata ya Bagara, mkoani Manyara, Nicodemus Tlaghasi James alisema CCM haiwezi kupeleka maendeleo kwenye maeneo yanayoongozwa na upinzani.

James alitoa kauli hiyo wiki iliyopita katika mtaa wa Mpya wilayani Babati akisema CCM haiwezi kupeleka maendeleo kwa wananchi waliochagua viongozi wa upinzani badala ya CCM.

Akizungumza leo Julai 30, 2018 na Mwananchi James amesema amefikia uamuzi huo baada ya kupokea simu za kumkemea na kumuonya juu ya kauli hiyo.

“Anayepokea sentensi hiyo, hawezi kujua mwanzo ulisema nini na mwisho ulisema nini, nimeamua kufanya kitu cha kiungwana kwamba ilimradi kilichopokelewa kwenye jamii ni kibaya, tumeamua kuomba radhi bila kujali mwanzoni na mwisho nilisema nini,” amesema James.

Chanzo: Mwananchi
 
Last edited:
"Nachukua nafasi hii kuwaomba Radhi Watanzania Wenzangu wote walio kerwa na ujumbe huo,na ninawashukuru viongozi wote wa kisiasa na kiraia walio nikosoa na kunikemea kwa maslahi mapana ya Taifa letu,ninawashukuru sana" Kheri James Mwenyekiti UVCCM Taifa

View attachment 822683
Hivi naanzaje kumsamehe mtu mjinga na limbukeni kama huyu ? aendelee kuamini kwamba Magufuli atakuwa rais milele , lakini aangalie kilichomkuta Sadifa , Mwenyekiti wa UVCCM aliyekuwa na matusi kuliko yeyote , hakuna marefu yasiyokuwa na ncha
 
Haha ni kawaida yetu Wana ccm kufanyaje. .......hiyo umeongeza chumvi kamanda
 
Edward N Lowasa(rtd PM) alivyokutana na Rais wa URT aliusia viongozi kuchunga kauli zao kwani amani ya nchi hii ni muhimu kuliko chochote kile, na kuna watanzania walipambana mpaka hapa tulipo day and night, wengine wametangulia mbele ya haki na wengine bado wako hai, sifa ya kiongozi ni unyenyekevu kwa wale anaowaongoza, kiongozi akianza kutoa lugha ya kejeli , dharau na iliyojaa kiburi si ishara njema, nawashukuru hao viongozi waliomfahamisha kuwa kwa maneno yale alikuwa amekengeuka si lugha ya kuombea kura hata kidogo, na si kura tu ila si lugha inayotakiwa kutoka kwa kiongozi anaeamini katika utawala wa sheria na uongozi wa kidemokrasia, safari bado ni ndefu, M/Mungu awajaalie viongozi wetu wawe na lugha ya kistaarabu na kiasi katika shughuli zao , every word to them gonna ferry or bury them, they have to put their brain engaged before putting their mouth into gear , merci beaucoup!
 
Hii ni hadithi ya Nyani na Jiwe!

Katika pita pita zake baada ya kushiba mema ya nchi hata kuvimbiwa kwa kula kile ambacho hakukilima au kikipanda akaamua apumzike juu ya Jiwe (mwamba) na hata kuujambia!

Kwa kuwa mwamba ulikuwa umepata joto kutokana na shida ya jua kali, uliamua kumuunguza NYANI matako yake na hata kubabuka!

Nyani akaruka kwa kuungua kule, ...akaondoka zake huku akitoa maneno ya kashfa kwa JIWE, ..."pamoja kwamba umeniunguza, nimekujambia"

Kati ya haya nani ni Nyani na Nani ni Jiwe?

Ameshasema, ameshaleta madhara hawezi kuponyesha nafsi zilizoraruliwa kwa kauli yake!...anaenda zake huku akisema "amekemewa kwa kauli yake"
 
Back
Top Bottom