Mwenyekiti tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) astaafu

mzee kazeeka hadi ubongo, alivyokuwa anatangaza matokeo ya uchaguzi kila akifika kwenye kura za Dr.Slaa anatetemeka mwili mzima.
 
akapumzike kwa amani ila hatakuwa na nafasi katika historia ya baadaye ya nchi yetu ni mbakaji wa demokrasia kwa kuipendelea CCM
 
Mi sitaki hata kumsikia maana nahisi kutapika! Si ndo huyu anayesababisha mpaka sasa hivi watanzania tunapigika kwa kuchakachua matokeo ya uchaguzi, na damu za watanzania zitamlilia milele kwa mashinikizo ya matumbo yao pamoja na walafi wenzie. Astaghafilah
 
Lewis Makame alichakachua kura za wapinzani akidhani alikuwa katika wadhifa wake ili kudumisha utawala wa ccm. Ni matumaini ya wapenda demokrasia ya kweli kwamba ataridhiwa na Mtanzania atakayeimarisha demokrasia ili nchi iweze kupiga hatua za kweli kimaendeleo.
 
Yule Kihongwe mwingine KIRAVU... bado yupo? Nakumbuka lile sauti lake DOVUTWA YAHMI DOVUTWA Kura 4 sawa na asilimia 0.009,MZIRAY PETER KUGA Kura 7 sawa na asilimia 0.018 yaaani Kipindi kile ALINIBOAJE?
na bado tunae mpaka kieleweke..
 
Ni kawaida yao kuombwa waendelee na kazi, mbona hata KATIBU MKUU KIONGOZI alishastaafu zamani, lakini yuko hapo kwa mkataba tu. Ina maana wengine hawawezi kushika nafazi kama hizo ni mpaka wazee tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu.
 
Ukweli utamuhukumu maisha yake maana anajua ujanja alokua anafanya pale Nec
 
Yule Kihongwe mwingine KIRAVU... bado yupo? Nakumbuka lile sauti lake DOVUTWA YAHMI DOVUTWA Kura 4 sawa na asilimia 0.009,MZIRAY PETER KUGA Kura 7 sawa na asilimia 0.018 yaaani Kipindi kile ALINIBOAJE?

TB,ilibidi nimrekodi kabisa,alinibore kupita maelezo na kila ninapokuwa namsikiliza nabaki kucheka tu,natumaini hata familia yake ilikuwa inapata fedheha jinsi Mzee alivyokuwa anang'an'gana kusoma matokeo ya uwongo.
 
Sasa aende kuchakachua familia yake na siku siyo nyingi atatengwa na ukoo wake.Wamezoeana sana na Kiravu inabidi wasitenganishwe sana kwani anaweza kufa
 
hana jipya huyu mzee zaidi ya kutumika kisiasa, huyu naye kachangia kwa namna moja ama nyingine kutufikisha hapo tulipo.
 
Ale zake kona,
Kwanza ameidhalilisha sana taaluma yake kama Jaji,
huyu babu na yule mchakachuaji mwenzie Kiravu nimetokea kuwachukia mpaka ntakapokufa.
Ukiangalia kwa umakini maamuzi ya hawa wazushi wawili yanaweza kuliangamiza kabisa taifa kwa kukubali kwao kuiweka madarakani serikali isiyotokana na matakwa ya wananchi.
 
Wana Jf.Taarifa nilizozipata hivi leo ni kuwa Mwenyekiti Tume ya Taifa ya uchaguzi Jaji Mstaafu Lewis Makame amestaafu kushikilia wadhifa huo.Mwenyekiti huyo amestaafu rasmi tangu tar 14/6 lakini kwa sasa bado haijatangazwa in public kwa kuwa anasubiri kukabidhi ofisi rasmi mara tu bada ya mtu mwengine kuteuliwa kushika wadhifa huo.Taarifa zinasema mwenyekiti huyo ilikua astaafu tangu mwaka nov 2004 lakini aliombwa na aliyekuwa Rais Ben Mkapa aendelee kushikilia nafasi hiyo kwa sababu kulikua na uchaguzi mkuu mwaka unaofuata jimbo ambalo lilihitaji mtu mwenye uzoefu.Mwaka 2009 alitaka kuachia ngazi tena akidai uzee umeshamchukua lakini Rais Kikwete alimuomba tena mzee huyu abaki Nec ili kusimamia uchaguzi mkuu uliopita mwaka jana ambao Rais Kikwete alishinda kwa mbinde.Mzee huyu ni mwenyekiti wa kwanza wa tume ya uchaguzi Tanzania jambo linalomfanya atumike sana kwa ushauri katika uchaguz wa nchi jirani kama Congo, Zimbabwe n.ksource: Chanzo Makini
nilijua tu
 
Afe kabisa asije kufundisha wengine jins ya kuchakachua 2015, nikatumia gun yangu.
 
Unamkumbuka kingunge ngombale mwiru? Aliacha uwaziri maalumu akiwa na miaka mingapi? Tanzania chochote chaweza kutokea
tz wazee hawataki kuacha kazi, na jambo hili ni baya kwan linabana nafas za vijana kupata fursa za ajira zaidi na hivyo kuzuia ustawi wa jamii nzima, watu wale wale, wa aina zile zile, na wa familia zile zile ndizo ztaendelea kupata fursa za ajira. Upumbavu kabisa huu.
 
Wana Jf.Taarifa nilizozipata hivi leo ni kuwa Mwenyekiti Tume ya Taifa ya uchaguzi Jaji Mstaafu Lewis Makame amestaafu kushikilia wadhifa huo.Mwenyekiti huyo amestaafu rasmi tangu tar 14/6 lakini kwa sasa bado haijatangazwa in public kwa kuwa anasubiri kukabidhi ofisi rasmi mara tu bada ya mtu mwengine kuteuliwa kushika wadhifa huo.Taarifa zinasema mwenyekiti huyo ilikua astaafu tangu mwaka nov 2004 lakini aliombwa na aliyekuwa Rais Ben Mkapa aendelee kushikilia nafasi hiyo kwa sababu kulikua na uchaguzi mkuu mwaka unaofuata jimbo ambalo lilihitaji mtu mwenye uzoefu.Mwaka 2009 alitaka kuachia ngazi tena akidai uzee umeshamchukua lakini Rais Kikwete alimuomba tena mzee huyu abaki Nec ili kusimamia uchaguzi mkuu uliopita mwaka jana ambao Rais Kikwete alishinda kwa mbinde.Mzee huyu ni mwenyekiti wa kwanza wa tume ya uchaguzi Tanzania jambo linalomfanya atumike sana kwa ushauri katika uchaguz wa nchi jirani kama Congo, Zimbabwe n.ksource: Chanzo Makini

a ACHA AENDE ZAKE MUHEZA AKANYWE MNAZI KWA MZEE BELEKO. HIYO TUME MPYA ITAKAYOKUJA HATAIWEZA. HAKUNA UCHAKACHUZI. BADO KIRAV4 NAE AONDOKE.
 
akamatwe na kufikishwa mahamani kwa udanganyifu na manipulation ya uchaguzi. Anahusika sana na matatizo ya watanzania
 
Ngoma imestaafu mara nne,
  1. Jaji Mstaafu, Mahakama kuu.
  2. 2004 Akastaafu NEC, Mkapa akamuomba.
  3. 2009 Akastaafu NEC Kikwete akamuomba.
  4. 2011 Kastaafu NEC haijatangazwa!
Siyo bure, kuna jambo hapo kati ya watu milioni 40; mtu mmoja anastaafu mara nne?
 
Na hilo ni kama tone moja la maji katika bahari! kuwa viongozi wengi kwenye taasisi nyeti za serikali ambao hawatakiwi kuwepo kwenye nafasi zao, lakini wanaendelea kuwepo kwa kisingizio cha uzoefu/utaalamu/sifa/na upuuzi mwingine.
Kuna idara moja pale UDSM mkuu wa kitivo alikuwa hataki kuajiri ikafika kipindi kitivo kiko hoi bin taabani bado mzee wa watu kakomaa! bajeti ikija anabana na mwisho wa mwaka anarudisha hela utawala kama salio (na ile hela wanagawana). Mzee wa watu katoka, watu wameshtuka kuwa kitivo/chuo hakina walimu wa kutosha. Ndo haya ya akina makame na serikali yetu.
Vijana tupo tupeni nafasi tunaweza tena efficiency karibu 100% lakini wazee wetu wanatafuta kusurvive na siyo kufanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.
 
Back
Top Bottom