Kishongo
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 932
- 64
Mimi nina maswali yafuatayo ambayo ningependa nimuulize
1. Ningependa kujua kuhusu hao vijana wake wa kazi mashushushu wanaompa taarifa mbali mbali anazokuwa anadai ni mabomu analipuwa, kwa taarifa za hivi karibuni kama ile aliyotutangazia kwenye mkutano wa hadhara kuwa Mstaafu wa EAC ameuawa na polisi na maiti yake iko Muhimbili na ikaja kugundulika kuwa ni taarifa ya uwongo, je anatuhakikishia vipi kuwa yale mabomu yake ya nyuma yalikuwa ni ukweli?
Pili vijana wake walioko TRA hivi karibuni walimpa tena taarifa za uwongo kuhusu gari iliyokuwa huko Tunduma, je ina maana yeye kila anachoambiwa anakichukulia kuwa ni kweli kabla ya kikifanyia kazi? Na kama kweli ana vijana mashushushu walio mahiri kwanini anatuletea mambo ya uzushi?
3. Ikiwa yeye kama kiongozi anaamini kila uzushi anaousikia mjini, je anatuhakikishiaje kuwa atakapokuwa kiongozi hatavictimize watu kutokana na taarifa za redio mbao na uzushi?
4. Kwanini hakemei wafuasi na wanachama wake wanaotumia matusi kumfanyia kampeni? Ina maana ameridhishwa au yeye ameidhinisha utovu wa nidhamu kwa wanachama wake?
5. Hili ni swali langu la mwisho, kwa kuwa Chadema imetumia resource nyingi kufanya kampeni za urais na kutelekeza kampeni za ubunge, je akishinda ataundaje serikali bila kuwa na wabunge wa kutosha kutoka kwenye chama chake? Na kwa kuwa chama chake kitakuwa na wabunge wachache sana ambao hawataweza kupitisha miswada yoyote bungeni, je hizo ahadi zake za kutekeleza mambo ndani ya siku 100 atazitekelezaje?
Hayo ni maswali yangu machache tu mwenyekiti naomba unifikishie maana mimi sitakuwepo kwa kuwa bado niko njiani!
Msafiri.
Source: MJENGWA BLOG
1. Ningependa kujua kuhusu hao vijana wake wa kazi mashushushu wanaompa taarifa mbali mbali anazokuwa anadai ni mabomu analipuwa, kwa taarifa za hivi karibuni kama ile aliyotutangazia kwenye mkutano wa hadhara kuwa Mstaafu wa EAC ameuawa na polisi na maiti yake iko Muhimbili na ikaja kugundulika kuwa ni taarifa ya uwongo, je anatuhakikishia vipi kuwa yale mabomu yake ya nyuma yalikuwa ni ukweli?
Pili vijana wake walioko TRA hivi karibuni walimpa tena taarifa za uwongo kuhusu gari iliyokuwa huko Tunduma, je ina maana yeye kila anachoambiwa anakichukulia kuwa ni kweli kabla ya kikifanyia kazi? Na kama kweli ana vijana mashushushu walio mahiri kwanini anatuletea mambo ya uzushi?
3. Ikiwa yeye kama kiongozi anaamini kila uzushi anaousikia mjini, je anatuhakikishiaje kuwa atakapokuwa kiongozi hatavictimize watu kutokana na taarifa za redio mbao na uzushi?
4. Kwanini hakemei wafuasi na wanachama wake wanaotumia matusi kumfanyia kampeni? Ina maana ameridhishwa au yeye ameidhinisha utovu wa nidhamu kwa wanachama wake?
5. Hili ni swali langu la mwisho, kwa kuwa Chadema imetumia resource nyingi kufanya kampeni za urais na kutelekeza kampeni za ubunge, je akishinda ataundaje serikali bila kuwa na wabunge wa kutosha kutoka kwenye chama chake? Na kwa kuwa chama chake kitakuwa na wabunge wachache sana ambao hawataweza kupitisha miswada yoyote bungeni, je hizo ahadi zake za kutekeleza mambo ndani ya siku 100 atazitekelezaje?
Hayo ni maswali yangu machache tu mwenyekiti naomba unifikishie maana mimi sitakuwepo kwa kuwa bado niko njiani!
Msafiri.
Source: MJENGWA BLOG