Mwenyekiti, Katibu Mkuu CHADEMA kigugumizi cha nini sakata la Wabunge wa Viti Maalum?

Ajitokeze aseme nini tena wakati Katibu Mkuu kashamaliza kila kitu kwamba ule mchakato mzima ni uhuni mtupu wa NEC wakisaidiana na Ndugai ili kuokoa zile 2 trillion za Mabeberu.
 
Mbowe hawezi kujitokeza kusema chochote juu ya hili kwa sababu alibariki mchakato mzima na aliridhia kilichotendeka hayo ni kwa mujibu wa Mdee alisema wazi kabisa kuwa Mbowe ameridhia sasa unatarajia Mbowe ajitokeza amkaange Mdee?!? haiwezekani.
kitakacho watafuna ni unafiki ulio komaa ndani ya chadema
Wanaccm wana vita personal na Mbowe, ni mwiba mchungu kwao kwa sababu ni kiongozi imara sana na dhamira yao ni kuhakikisha Chadema inafutika sasa wanachukulia advantage kwenye hizi dhoruba zinazokikumba chama ili kufarakanisha kati ya mwenyekiti na wanachama. Lakini ukweli wanachadema tunaujua kuwa Mbowe ni kiongozi imara sana ndio maana tunamuita "MWAMBA". Asante kiongozi wetu kwa busara zako, umemtuma katibu mkuu ametangulia na ni imani yetu kuwa kesho mtatoa uamuzi sahihi kwa ajili ya ustawi wa chama.

Chadema nguvu moja!!!
 
Dah...Nadhani mwenyekiti atakuwa bado anatafakari…….
"Muishi nao kwa akili" 🤣 🤭
 
Huko cdm naamini kauli za Lisu tu hao wengine wakiongozwa na akina Mbowe ni wajasiliamali wa siasa afadhali na Lema
 
Lissu na zitto waanzishe Chama tutawafuata. CDM naona wanafuata maslahi yao tu.
ACT-Wazalendo bado inaweza vaa viatu,hatufuati chama hapa ila watu tunaowaamini watatuvusha,Mbowe naona keshafikia malengo ya biashara yake ya ujasilimali wa siasa
 
Hata mimi nimeshukuru kwakweli yaani CHADEMA wameonesha uhalisia wao mapema kabisa hahaahaahahahahaha hivi huyu mbowe si ndio angekua waziri mkuu huyu huyu mmh kuanzia leo sitawashabikia tena washenzi wakubwa hawa
Hata kampeni za Lisu hakuonekana na inaonekana yeye alipendelea Nyalandu lakini pamoja na hiyo kampeni za Lisu zilifaulu sana given mazingira yaliyokuwepo na nguvu kubwa sana ya dola iliyotumika.Kimsingi huyu bwana amekuwa akivuruga harakati nyingi sana sasa anatakiwa ajue bila Lisu hakuna cdm,kama tulivyosema awali kama Lisu hagombei kura atapga yeye na genge lake tumechoka na uhuni wake
 
Kuhusiana na hii ishu ya wabunge wa Viti Maalum CHADEMA.

Naona watu wengi wanashindwa kuelewa nini kinaendelea juu ya kilichotokea leo, wapo wanaotaka hao wabunge wa viti maalumu waliokwenda kuapishwa leo, wafukuzwe chamani kwa kuwa wamekwenda kinyume na msimamo wa chama kama anavyosema Mnyika (Katibu Mkuu wa chama)

Ila me binafsi naona kama wafuasi wa CHADEMA wanachezewa 'mind game' na viongozi wapo wakuu wote wakiwemo Mnyika na Lissu.

Kwanini basi me nafikiri hivyo?

Juzi tu hapa Lissu pamoja na Zitto waliitisha mkutano na waandishi wa habari, ajabu katika mkutano huo wamezungumzia jambo ambalo linafahamika kwa kila mtu.

Wamezungumzia jambo ambalo walishalizingumzia muda si, mwingi sana.

Sasa mtu unajiuliza nini lengo la hawa jamaa kuwaita wanahabari na kuwaambia kwamba hawatambui matokeo ya uchaguzi huu na hawatashirikiana na serikali iliyopo madarakani hivi sasa?

Si hata mwezi haujaisha wamelisema hili?

Kwanini juzi wameamua kulirudia tena?

Kwa sababu walikuwa wanajua nini kitatokea ndani ya muda mfupi ujao, na wao ni sehemu ya maamuzi hayo ila tu wanawahadaa wafuasi wao ili ionekane kwamba wao wana misimamo isiyoyumba.

Kinachofuata muda si mrefu ni Maalim Seif kujiunga na serikali ya Mwinyi then game over, hakuna cha uchaguzi haukuwa wa kidemokrasia wala haki za binadamu zimevunjwa.

Kazi kwenu mnaoamini.
Labda kuna kaukweli maana unaweza kuta wamepiga hesabu ya faida ya kifedha watakayoipata na pengine wameshafikia compromise na serikali kimya kimya ila sasa wanapima upepeo na kuona gia gani waje kuitumia,maana sikuelewa ile kauli ya Lisu kuomba maridhiano na serikali,ile ilikuwa ni kibali kwa bawacha kuingia serikalini,nataka nione mwisho wa huu mchezo utakuwaje na mimi itanisaidia kufanya maamuzi binafsi kuhusu mambo ya kisiasa
 
Kuwa na mwanamke mpinzani wa aina ya Halima Mdee, Ester Bulaya na Ester Matiko ni fahara kubwa sana kwa chama na nguvu ya harakati.

1. Ni wahamasishaji wazuri.
2. Waliwapa wanawake ujasiri na sababu ya kujivunia.
3. Walitoa picha ya harakati shirikishi.

Kilichowakuta ni nini? Mimi sifahamu.
Kwa Dr.Slaa ilikua rahisi sana kutabiri, alikua na kila sifa ya Yuda Isikarioti, hata sura!
Ila Halima?
Ester Bulaya?

Nataka niamini kuna INTIMIDATION kubwa sana nyuma ya hili zoezi!
Nataka niamini it was against their will.
Ila hizi ni imani tu.

Muda ndio mwalimu mwema!
 
Kwa nini unaona ni hasara kwa CHADEMA na siyo hasara kwa nchi? Upinzani ukiwa imara ni faida kwa wananchi wote. Wapinzani ukiwa ni puppet wa serikali ni hasara kwa nchi
 
Mwaka jana kulivuja sauti ya wabunge wa Chadema Said Kubenea na Anthony Komu wakipanga njama za kumuuwa Boniface Jacob ili hatimae wafanikishe adhima yao ya kumng'oa Freeman Mbowe kwenye uenyekiti wa chama.

Baada ya sauti hizo kuvuja mara moja chama kilitangaza kikao cha dharura cha kamati kuu kuwahoji ili waweze kuchukuliwa hatua kali sana ikiwa pamoja na kufukuzwa Chadema. Matokeo yake baada ya kikao cha kamati kuu hao wabunge wauaji walisamehewa na kutakiwa kuomba radhi tu!!!

Kama hali ni hiyo, wabunge wa viti maalum Chadema si wauaji na wala hawajatishia kumuuwa mtu yoyote ila wanajaribu tu kutumia haki yao ya kikatiba iweje wafukuzwe Chadema? Kweli kuwa mwanamke Chadema ni dhambi kubwa kuliko wapanga mauaji waliosamehewa??

Tusubiri na kuona kesho kikao cha kamati kuu chadema kitaamua nini ,bila shaka Mbowe is going to be tested again na maamuzi tofauti na kufukuza yatamwimalisha ,na maamuzi ya kufukuza hao wanawake itakuwa ni kiss of death kwa Mbowe na Chadema kwa ujumla.
 
Mnahangaika sana, Chadema ni taasisi imara. Alikuwepo Zitto, alipotoka mlifikiri Chadema itakufa. Alikuwepo Dr Slaa, apoondoka mlifikiri Chadema itakufa.
 
Kilichofanyika ni zaidi ya usaliti.Je halima kabla ya kwenda kuapa hakuwasiliana na hata katibu mkuu?
 
Back
Top Bottom