Mwenyekiti Halmashauri Tarime Vijijini anayekabiliwa na kesi ya mauaji aachiwa kwa dhamana

nokwenumuya

JF-Expert Member
Jun 29, 2019
810
2,851
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tarime Vijijini, Simon K pamoja na wenzake wanaokabiliwa na kesi ya mauaji namba PI RM (MURDER) CASE NO. 4/2021 wameachiwa kwa dhamana hapo jana mjini Musoma. Jambo ambalo limewashangaza watu wengi kwani inajulikana wazi kuwa kesi hiyo haina dhamana.

Hata hivyo mke wa Mwenyekiti huyo alikuwa anajisifia kuwa wametumia milioni zaidi ya 400 hivyo lazima mumewe atoke.

Taarifa zilizopatikana ni kuwa Mwenyekiti huyo amebadilishiwa mashitaka kutoka kesi ya kuua kwa kukusudia hadi kuua bila kukusudia na ndio mwanya waliotumia kumpa dhamana.

Jambo hili ni baya mbele za umma kwani ushahidi wa huyu Mwenyekiti kuua uko wazi. Ni murder case na hakuna kesi ya kuua bila kukusudia.

Kwa kuwa huyo Mwenyekiti ni mfanyabiashara na ana pesa basi sasa watu wanaamini uongozi wa sasa unakumbatia watu wenye pesa na kuwa wenye pesa wako juu ya sheria.

Wanaweza kuua na kuhonga na kuepuka mkono wa sheria.

Hii ni ishara mbaya katika uongozi wa awamu ya sita. Na itabaki hivyo kuwa kama unataka haki basi tafuta pesa za kuhonga.
 
Enzi za mwendazake haya yalikuwa yamepungua,Pamoja na mapungufu ya awamu ya 5 lakini kuna machache hatuwezi kumsema vibaya!Hata hili la hawamu hii nayo ni zimwi tu, Lipi jema!?
 
Mtoa mada we ni Nani kwa namna Moja ama nyingine. Katika kesi hii.
Maana kuna tetesi kuwa ni mshindani wako ki biashara.

Lakini pia, jambo likiishakuwa mahakamani , haturuhusiwi kuuingilia muhimili huo.

Ikiwa hauridhiki na mwenendo wa kesi , kuna taratibu.

Ila pia, pale police mnapopeleka kesi zenu ndio shida inapoanziaga. Mnaenda mkiwa na mihemuko. Mnaandika charge zinazojichanganya. Mkipanda mahakamani zote zinapanguliwa na hoja moja.
 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tarime Vijijini, Simon K pamoja na wenzake wanaokabiliwa na kesi ya mauaji namba PI RM (MURDER) CASE NO. 4/2021 wameachiwa kwa dhamana hapo jana mjini Musoma. Jambo ambalo limewashangaza watu wengi kwani inajulikana wazi kuwa kesi hiyo haina dhamana.

Hata hivyo mke wa Mwenyekiti huyo alikuwa anajisifia kuwa wametumia milioni zaidi ya 400 hivyo lazima mumewe atoke.

Taarifa zilizopatikana ni kuwa Mwenyekiti huyo amebadilishiwa mashitaka kutoka kesi ya kuua kwa kukusudia hadi kuua bila kukusudia na ndio mwanya waliotumia kumpa dhamana.

Jambo hili ni baya mbele za umma kwani ushahidi wa huyu Mwenyekiti kuua uko wazi. Ni murder case na hakuna kesi ya kuua bila kukusudia.

Kwa kuwa huyo Mwenyekiti ni mfanyabiashara na ana pesa basi sasa watu wanaamini uongozi wa sasa unakumbatia watu wenye pesa na kuwa wenye pesa wako juu ya sheria.

Wanaweza kuua na kuhonga na kuepuka mkono wa sheria.

Hii ni ishara mbaya katika uongozi wa awamu ya sita. Na itabaki hivyo kuwa kama unataka haki basi tafuta pesa za kuhonga.

Usiishi kwa kukariri, kuwa kesi za mauaji hazina dhamana.

Rejea kesi ya Lulu Michael elizabeth.

Ditopile Mzuzuri.

Chenge Andrew Mtemi.

“Wewe na mke wa marehemu mmetoana wapi na hayo maneno ya 400M)”
 
Back
Top Bottom