Mwenyekiti chama cha walimu aipongeza serikali kwa kuahidi kulipa deni la walimu la milioni 800

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,252
Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Bwana JOSEPH NDALAMA, amepongeza hatua iliyochukuliwa na serikali ya kuahidi kuyalipa madeni ya walimu wanayodai, ambayo yamefikia zaidi ya shilingi milioni 800.

Hata hivyo ameitaka serikali itekeleze ahadi hiyo mapema iwezekanavyo, ili kuinua ari ya walimu katika kutekeleza majukumu yao ya ufundishaji, kwani wanaishi katika mazingira magumu.

Kwa upande wake Katibu wa chama hicho Bwana PETER SIMWANZA, amewaonya walimu hao wasichanganye utetezi wa walimu na mambo ya kisiasa, hali ambayo amesema inaleta mihemko inayochangia uvunjifu wa amani.

Chanzo: ITV
 
Kwa sasa kuna shughuli za uhakiki endelevu hadi 2020. Tulieni mtalipwa after 2020
 
Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Bwana JOSEPH NDALAMA, amepongeza hatua iliyochukuliwa na serikali ya kuahidi kuyalipa madeni ya walimu wanayodai, ambayo yamefikia zaidi ya shilingi milioni 800.

Hata hivyo ameitaka serikali itekeleze ahadi hiyo mapema iwezekanavyo, ili kuinua ari ya walimu katika kutekeleza majukumu yao ya ufundishaji, kwani wanaishi katika mazingira magumu.

Kwa upande wake Katibu wa chama hicho Bwana PETER SIMWANZA, amewaonya walimu hao wasichanganye utetezi wa walimu na mambo ya kisiasa, hali ambayo amesema inaleta mihemko inayochangia uvunjifu wa amani.

Chanzo: ITV
yaani ahadi tu anatoa pongezi?

ajifunze kwa huyu mzee wa 1960S hapa... Mzee awapiga za uso CCM
 
Hiki chama hakina tofauti na UVCCM, kazi yake ni kutetea masilahi ya walimu na siyo kupongeza kulipwa haki za watu kitu ambacho ni wajibu wa serikali, tatizo wamegeuka kuwa wapongezaji kama UVCCM. Chama cha hovyo sana kivunjwe.
 
Hawa nao ndo mana kila siku wanaambiwa hawajielewi, hizo ahadi wameanza kupewa Leo?
 
Back
Top Bottom