Mwenye uzoefu na Online loss report--polisi

JAMBONIA LTD

JF-Expert Member
Jan 22, 2014
576
263
Habari wakuu, nimejaza online loss report kwa ajili ya laini ya simu nimefanya malipo baada ya kutumiwa control number kila nikiingia sehemu ya kuangalia taarifa yako ili nipate kupakua ile loss report naambiwa taarifa yako haijathibitishwa. Kwa utaratibu wa sasa wameeleza kuwa kwa loss report ya laini za simu na vitambulisho ikiwa umetumia NIDA kujisajili basi hakuna haja ya kwenda kituo cha polisi kuthibitisha bali utatumiwa hapo hapo baada ya malipo ila mpaka sasa siku ya 4 leo bado inanambia taarifa yako haijathibitishwa nifanye nini kuipata report hii?
 
kama sikosei inabidi uende polisi na hizo reference no.. wao ndo wanadhibitisha
 
Kama umetumia namba ya NIDA huhitaji kwenda Polisi.

Sema kwenye ku search ripoti yako unakosea. Fuata maelekezo yao.
Tumia ile alama ya 'hyphen' kama inavoonekana upande wa mbele wa NIDA yako
 
wameandika kwa ishu ya laini za simu na vitambulisho hautakiwi kwenda polisi kama zamani
Duh hawa jamaa hawaeleweki. Au labda wanamalizia msiba?

Hebu jisogeze kituo cha polisi cha karibu upate uhakika zaidi. Usisahau kuturejea kwa ajili ya mrejesho tafadhali...
 
Kama umetumia namba ya NIDA huhitaji kwenda Polisi.

Sema kwenye ku search ripoti yako unakosea. Fuata maelekezo yao.
Tumia ile alama ya 'hyphen' kama inavoonekana upande wa mbele wa NIDA yako
Ukikosea hupati majibu inakwambia umekosea ....huwa naweka na hyphen na inanipa majibu kwa kunipa jina langu kamili ila irb na fomu ndio haviji inasema haijathibitishwa
 
Duh hawa jamaa hawaeleweki. Au labda wanamalizia msiba?

Hebu jisogeze kituo cha polisi cha karibu upate uhakika zaidi. Usisahau kuturejea kwa ajili ya mrejesho tafadhali...
Ok, nimepanga kutawaona jamaa wasteshenari kwanza ambao huwa wanawadaunlodia wateja wao kila siku fomu hizi
 
Nilitumia mwezi kufwatilia loss report ya Cheti changu.. kila nikifanya malipo naambiwa yanakubali ila fomu inasema haijadhibitishwa
 
Back
Top Bottom