Mkuu wewe unataka nini zaidi ikiwa Lowassa mwenyewe kakubali mbele ya waandishi wa habari akimjibu Manyerere (tazama video yake) amekiri kwa kujisifia kuwa mradi ule ulikuwa safi kabisa na mitambo ilikuwa state of art ulosifiwa na rais wa Marekani wakati hata hilo kadanganya, unataka nini zaidi?. He confessed on record nakala tunayo.Mkuu vuta subira kidogo tu, hili la RICHMOND liliwekwa kiporo pale sheikh Kaluta kwa sababu maalum, ila nina imani kubwa kuwa LOWASSA atateuliwa na CCM kuipeperusha bendera ya chama, hivyo katika muendelezo wa safari hii ya matumaini RICHMOND itaibuka tu, na ukweli wote utadhihirika!
Hizi sio tuhuma ni KASHFA za kiongozi na hakuna mahala alipopinga kwamba hahusiki na zaidi ya hapo alikuwa waziri mkuu alopitisha mkataba ule wapewe nani..Nukuu kibao katika report ya tume unataka nini zaidi? JK sio mjinga wa Kuachia report ile ilopelekwa kwake kwanza aje airuhusu ipelekwe bungeni wakati inamhusu yeye. Jk alijua fika Lowassa kahusika na alimwambia ajiuzuru mapema kabla halijafika mbali. Alitumia uungwana wake leo mnataka kubadilisha na hata kuwatisha familia yake ati mkiingia madarakani watakiona cha moto jamani, jamani kuweni na utu japo kidogo.