Mwenye uelewa kuhusu Tujijenge Saccos

kambagasa

JF-Expert Member
Aug 18, 2014
2,241
1,749
Ndugu zangu,rafiki yangu alinishauri kujiunga na hii saccos ili nipate mkopo. Leo hii naelekea mwezi mzima tangu niweke akiba sijapata mkopo. Nimepiga simu nyingi sana kwa meneja katika tawi langu imefikia hatua hapokei simu wakati awali alikuwa ananiambia kuna tatizo wanalifanyia kazi makao makuu Dar es salaam
 
Hiyo sio saccoss bhana n microfinance,kws sasa wPo juu ya mawe
Mkuu naomba unifafanulie vizuri niliweka akiba ya laki nne pamoja na gharama za kufungua akaunti ili niingeze mzigo kipindi hiki cha sikukuu. Wako juu ya mawe kivipi?
 
Saccos nyingi zinakufa ama haziendelee kutokana na watu wenye mawazo kama wewe.

1. Kumbuka saccos ni chama cha ushirika ambayo kazi ya zake kuu ni kuweka akiba kwanza na hatua inayofuata ni kukopa

2.Unacho kikopa ni akiba za wanachama walioweka na kwa kuwa ni ushirika basi wanakopeshana

3. Saccos nyingi hukopesha kwa uwiano wa akiba ya mwanachama mara nyingi akiba yako huzidishwa mara tatu ili kupata kiasi cha mkopo kama sikosei

4.Suala la umri wako kwenye chama nacho ni kigezo muhimu sana katika kukopeshwa na mara nyingi lazima wakuchunguze kwa kipindi kisichipongua miezi mitatu angalau kujua tabia yako ya kuweka akiba na nidhamu ya kurudisha deni ambalo ni michango ya wanachama wenzako.

5. Nilichokigundua ni kuwa wabongo wengio wanajiunga kwenye saccos baada ya kuelemewa na madeni na wanakwenda pale wanataka wapige pesa fasta ili wakahahamishe madeni na kufanya hivyo mikopo inashidnikana kurudi na vyama vinayumba.

6.Maafisa mikopo wengi wa hizi saccos hula dili kwa kupitisha mikopo kwa wanachama ambao ni pre mature na kuvuta mkwanja na kulala mbele.

7. Mwisho kama umejiunga na saccos, huumuda ambao haujifikisha hata miezi mitatu jitahidi kwanza kosoma sheria ya vyama vya ushirika, katiba ya chama ulichojiunga nacho na kuelewa kabisa ili ujue haki na wajibu wako, na sio kukimbilia tuu kukopa haraka haraka hata kabla hujajua masharti ya chama, riba n.k, subiri miezi mitatu tena anza kukopa kidogo kidogo kwanza kwa maslahi ya chama chako lakini vilevile kwako wewe binafsi kujijengea ndidhamu ya kujenga uchumi kidogokidogo na wajibu wako wa kurudisha deni kwa muda.
 
Saccos nyingi zinakufa ama haziendelee kutokana na watu wenye mawazo kama wewe.

1. Kumbuka saccos ni chama cha ushirika ambayo kazi ya zake kuu ni kuweka akiba kwanza na hatua inayofuata ni kukopa

2.Unacho kikopa ni akiba za wanachama walioweka na kwa kuwa ni ushirika basi wanakopeshana

3. Saccos nyingi hukopesha kwa uwiano wa akiba ya mwanachama mara nyingi akiba yako huzidishwa mara tatu ili kupata kiasi cha mkopo kama sikosei

4.Suala la umri wako kwenye chama nacho ni kigezo muhimu sana katika kukopeshwa na mara nyingi lazima wakuchunguze kwa kipindi kisichipongua miezi mitatu angalau kujua tabia yako ya kuweka akiba na nidhamu ya kurudisha deni ambalo ni michango ya wanachama wenzako.

5. Nilichokigundua ni kuwa wabongo wengio wanajiunga kwenye saccos baada ya kuelemewa na madeni na wanakwenda pale wanataka wapige pesa fasta ili wakahahamishe madeni na kufanya hivyo mikopo inashidnikana kurudi na vyama vinayumba.

6.Maafisa mikopo wengi wa hizi saccos hula dili kwa kupitisha mikopo kwa wanachama ambao ni pre mature na kuvuta mkwanja na kulala mbele.

7. Mwisho kama umejiunga na saccos, huumuda ambao haujifikisha hata miezi mitatu jitahidi kwanza kosoma sheria ya vyama vya ushirika, katiba ya chama ulichojiunga nacho na kuelewa kabisa ili ujue haki na wajibu wako, na sio kukimbilia tuu kukopa haraka haraka hata kabla hujajua masharti ya chama, riba n.k, subiri miezi mitatu tena anza kukopa kidogo kidogo kwanza kwa maslahi ya chama chako lakini vilevile kwako wewe binafsi kujijengea ndidhamu ya kujenga uchumi kidogokidogo na wajibu wako wa kurudisha deni kwa muda.
Mbona povu mkuu? Wakati wanatafuta wateja mbona waliniambia ukiweka akiba ni siku tatu tu na sio porojo zako hizi. Kama ni mmojawao fanyeni mrudishe akiba yangu maana nimeiomba irudishwe lkn wanadai iko kwenye mchakato wa mkopo
 
Mbona povu mkuu? Wakati wanatafuta wateja mbona waliniambia ukiweka akiba ni siku tatu tu na sio porojo zako hizi. Kama ni mmojawao fanyeni mrudishe akiba yangu maana nimeiomba irudishwe lkn wanadai iko kwenye mchakato wa mkopo
Kajifunze kutofautisha benki na saccos naona huelewi chochote
 
Mbona povu mkuu? Wakati wanatafuta wateja mbona waliniambia ukiweka akiba ni siku tatu tu na sio porojo zako hizi. Kama ni mmojawao fanyeni mrudishe akiba yangu maana nimeiomba irudishwe lkn wanadai iko kwenye mchakato wa mkopo
acha ubishi, unatakiwa umshukuru
 
Ww hyuo aliyefafanua hapo juu amekusaidia sanaaa,sawa?wewe hujaweka fedha saccoss km umeweKa saccoss,fata elimu aliyotoa ndgu yetu,na km n tujijenge umeliwa hao sio saccoss ni microfinance ni vitu viwili tofauti elewa hivyo kwNzA
 
Back
Top Bottom