Mwenye taarifa za TAPELI hili tuwasiliane

vamda

JF-Expert Member
Aug 1, 2012
858
533
Ndugu wana JF na watanzania wengine kuna TAPELI mmoja anayejiita Phinias Aloyce huzunguka mikoa na wilaya mbalimbali na kuwaibia watu kwa njia za udanganyifu akijifanya yeye ni mfanyakazi kutoka kampuni ya Nokia Ltd. Hivi karibuni TAPELI hilo lilipita kwenye shule za msingi na sekondari wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga na kuwatapeli walimu wengi kwa kuwauzia vizuia mionzi feki na kudai kampuni ya Nokia Ltd imeamua kuwakopesha walimu mkopo nafuu wa simu za nokia kwa muda wa miezi sita.

TAPELI hilo hutembea na nyaraka zenye jina la kampuni ya Nokia Ltd. Namba zake za mawasiliano ni: 0784 298085/ 0719 434700/ 0766 103008/ 0784 953914/ 0719 434699 na 0715 298085.

Mtu huyo ni mwongeaji sana, mnene, mweusi, ana kitambi, ana sura ya duara pia anaonekana ni mtu mwenye heshima kupitia mavazi anayovaa. Aliowaibia fedha wanapomfuatilia huwatisha kwa kuwaambia endapo wataripoti kwenye vyombo vya usalama fuatilia wataumia.

TAPELI hilo linatafutwa na polisi kwa jalada namba KHM/RB/3445/2013.

Mwenye taarifa kuhusu TAPELI hilo atoe taarifa kwenye kituo chochote cha polisi akitaja namba ya RB iliyotajwa hapo juu. Au apige simu zifuatazo: 0713 758165/ 0755 831576/ 0784 821973. Tushirikiane ili tuyaangamize MATAPELI haya.
 

Attachments

  • TAPELI.docx
    11.4 KB · Views: 426
Mhh vizuia mionzi,teknolojia mpya hiyo lakini hapo hujaeleza katapeli nini?maana umesema watakopeshwa simu na hiyo ya kuuziwa vizuia ni makubaliano maana hata dar wamachinga au kkoo tunanunua sana vitu feki
 
Kweli waalimu ni mteremko. Nimegundua kwanini zero zinaongezeka.

Anyway! Poleni wahanga.
 
Hujaonesha connection ya maelezo yako na utapeli wake. Fafanua vizuri tujue utapeli wake ukoje.
 
jamani walimu si wanalalamikia masilahi duni? mbona wachezea hela?, au za twisheni...... :heh::heh::heh::heh: :heh::heh: :heh:
 
Wakuu,

Tuache mzaha wale wenye taarifa watoe kesho atalizwa mama yako huko kijijini au shangazi yako acheni utani.
 
Kwi kwi kwi !
Unaposema walimu ni mtelemko una maana
gani Mkuu ? Pole pole jamani.
 
Hujasema katapeli nini?

Maelezo yako yanaonyesha jamaa ni mfanyabiashara ya vizuia mionzi na anawauzia walimu,

Sasa sijakuelewa jamaa ni tapeli vipi?

Fafanua zaidi
 
waalimu jipangeni, maana kuna kesi nyingi tu za utapeli katika mashule, hasa hasa issue za mikopo zimekua zikiwaumiza sana waalimu, kuweni makini japo kidogo
 
Fursa fursa fursa fursa....hizo. Na nyie mjipange na muwe mnajisumbua kurafura maarifa kidogo. Unauziwa kitu hata kujisumbua kutafuta habari kidogo za huyo muuzaji au hiyo bidhaa haujisumbui! Ha!
 
Wakuu,<br />
<br />
Tuache mzaha wale wenye taarifa watoe kesho atalizwa mama yako huko kijijini au shangazi yako acheni utani.

Kwa mujibu wa kichwa cha habari na maelezo yake bado hatujaona huo Utapeli wa huyo jamaa.
 
Labda utapeli wa kuwakopesha hivyo vizuia mionzi bila kuchukua pesa zao...hehehehe
 
Ndugu wana JF na watanzania kw jumla kuna mtu mmoja anayejiita Phinias Aloyce anatafutwa na polisi kwa jalada namba KHM/RB/3445/2013 kutokana na tuhuma za kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu wilayani kahama. Mtu huyo anayejifanya ni mfanyakazi wa kampuni ya Nokia Ltd akiwa na nyaraka zenye jina la kampuni hiyo, hivi karibuni alipita kwenye maofisi mbalimbali zikiwemo shule na kuwaibia watu kwa kuwauzia vizuia mionzi feki. Pia aliandikisha majina na kukusanya fedha nyingi kwa ahadi ya kuwaletea simu kutoka kampuni iliyotajwa lakini mpaka sasa zaidi ya mwezi mmoja umepita hakuna mawasiliano yeyote na simu zake zote amezima. Namba zake za simu ni: 0784 298085/ 0719 434699/ 0766 103008/ 0784 953914/ 0719 434699/ 0715 298085. Mtu huyo ni mwongeaji sana, mnene, mweusi, ana kitambi, ana sura ya duara, umri wake unakisiwa kati ya miaka 45 hadi 55, anaonekana ni mtu wa heshima kupitia mavazi anayovaa. Yeyote anayemfahamu mtu huyo atoe taarifa kwenye kituo chochote cha polisi akitaja RB iliyoandikwa hapo juu ili atiwe mbaroni mapema. Au wasiliana nami kwa namba 0713 758165/ 0755 831576/ 0784 821973.
 

Attachments

  • NOKIA LTD.doc
    565.5 KB · Views: 113
Du! Poleni...lakini pia tunatakiwa kuwa waangalifu, tuache tabia ya kununua vitu mikononi na kwa ahadi wakati maduka yamefurika. Huu ni wakati wa kutumia akili kufikiri badara ya kutaka watu wafikiri kwa ajili yako!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom