Mwenye nyumba anakusanya pesa za kunyonya majitaka kwa wapangaji lakini anatumia pesa hizo kwa matumizi binafsi

Aug 22, 2018
44
50
Nyumba za kupanga,

Imetokea Katika nyumba moja hivi hapa Dar es Salaam, Choo kimejaa halafu Mwenye nyumba kachangisha pesa ili gari ya maji taka ije Kunyonya lakini tamaa ikamuingia mwenye nyumba akala ile pesa yote. Hali hii imetokea mara tatu pesa zinaliwa.

Siku zikaendelea, choo kinazidi kujaa na hali ni mbaya, wapangaji hawana la kufanya.

Mwisho wa siku mpangaji mmoja amegoma kutoa pesa kwa ajili ya suala hilo kwani pesa ishaliwa mara tatu ikabidi amwambie mwenye nyumba kuwa ukitaka pesa yangu kwa suala hilo tafuta pesa mwenyewe itagari ya majitaka ije isqfishe baada ya hapo nitatoa pesa.

Mwenye nyumba anaona kuwa mpangaji wake amekuwa mkaidi, anaamua kuwaita wapangaji wengine anawashawishi watoe pesa kisha Mke wa yule aliyekataa kutoa pesa kwa mara ya nne anapiga simu kwa mmewe ili pesa itolewe, Mwanaume anakataa na kutoa lake la moyoni akisema kwamba endapo gari itakuja nitatoa pesa kinyume na hapo ni ubabaishaji.

Mwenye nyumba ni Mjumbe wa nyumba kumi hapo mtaani, sasa nini kifanyike ili huyo mwenye nyumba afanye usafi wa Choo?

Ukisema uende serikali za mtaa, yeye pia ni mwakilishi mtaani hapo. Wapangaji wana watoto wadogo ambao wanaweza kuathirika kiafya.

Wapangaji washitaki wapi ili kuondoa usumbufu huo?

Karibuni
 
Hameni kwani lazima mkae Magomeni nyumba zilizokuwa za NHC hizo zimechakaa jamani
 
Dawa ni kuhama TU,

Biashara yenyewe ya nyumba na hii Corona, imedoda mno.

Mambo yameyumba, watu wamerudi vijijini
Nyumba kibao ziko wazi .

Hameni wote Akili imkae sawa sawa.

ONYESHENI MSIMAMO
 
Nyumba za kupanga,

Imetokea Katika nyumba moja hivi hapa Dar es Salaam, Choo kimejaa halafu Mwenye nyumba kachangisha pesa ili gari ya maji taka ije Kunyonya lakini tamaa ikamuingia mwenye nyumba akala ile pesa yote. Hali hii imetokea mara tatu pesa zinaliwa.

Siku zikaendelea, choo kinazidi kujaa na hali ni mbaya, wapangaji hawana la kufanya.


Mwisho wa siku mpangaji mmoja amegoma kutoa pesa kwa ajili ya suala hilo kwani pesa ishaliwa mara tatu ikabidi amwambie mwenye nyumba kuwa ukitaka pesa yangu kwa suala hilo tafuta pesa mwenyewe itagari ya majitaka ije isqfishe baada ya hapo nitatoa pesa. Mwenye nyumba anaona kuwa mpangaji wake amekuwa mkaidi, anaamua kuwaita wapangaji wengine anawashawishi watoe pesa kisha Mke wa yule aliyekataa kutoa pesa kwa mara ya nne anapiga simu kwa mmewe ili pesa itolewe, Mwanaume anakataa na kutoa lake la moyoni akisema kwamba endapo gari itakuja nitatoa pesa kinyume na hapo ni ubabaishaji.

Mwenye nyumba ni Mjumbe wa nyumba kumi hapo mtaani, sasa nini kifanyike ili huyo mwenye nyumba afanye usafi wa Choo?

Ukisema uende serikali za mtaa, yeye pia ni mwakilishi mtaani hapo. Wapangaji wana watoto wadogo ambao wanaweza kuathirika kiafya.

Wapangaji washitaki wapi ili kuondoa usumbufu huo?

Karibuni
Mpeni kipigo cha mbwa koko
 
Acheni ujinga kwani mmewekewa gundi kwenye hiyo nyumba? Maana hata nyie mnaoishi humo ni wapuuzi tu kama upuuzi mwingine
 
Watanzania wengi ni waoga sana. Inakuwaje mtu akuchangishe kitu hicho hicho zaidi ya mara moja!?
 
Mara tatu anakula... ..!


Kwani mkataba wenu wa pango umebakiza miaka kumi na ngapi.....! Halafu mmiliki mwenye Nyumba wa aina hiyo hata nyumba zao haziwangi nzuri kivileeeeee.
 
Nyie wapangaji wote ni wajinga Sana,kwa Nini msiite gari,mkachangishana wenyewe na mkalipa? Mpaka mumkabidhi faza house? Bora azile tu maana wapangaji wote nyie hamnazo kabisa.
 
Back
Top Bottom