Mwenye mawazo:Itawezekana vipi katiba kuweka mahakama ya kadhi bila kuona yaikutayo bakwata leo?

Nicholas

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
25,261
7,195
Najaribu fikiri ni vipi Katiba inaweza kuweka Mahakama ya kadhi bila ,kuicha ktk lawama ambazo serikali na Bakwata wanazipata Leo?

Pamoja na ukweli kuwa hata wakristu nao wanaweza weka Amri 10 ktk mahakama yao,na wakatoliki nao watapitisha sheria zao za kanisa.Pia kutaka serikali igharamie na kuiweka mahakama ya kadhin ni unyonyaji na contradcition ktk Katiba ya nchi.Kuwa na sheria mbili ambazo mara nyingi zitagongana.

Tunajua ni mpango wa wachumia tumbo ambao wanadhani watapata kitengo cha kutuliza njaa,na baadaye watakaokosa wataanza tangaza kutoitambua km leo tuanvyo Bakwata.

Wenye mawazo mbadala watusaidie.Ni vipi serikali itaweka mahakama ya kadhi bila kuingilia uislam?Ni vipi nchi ikaendeshwa kwa sheria tofauti ktk jambo moja na zote zikawa na mamlaka sawa?Km si mamlaka sawa basi sheria za nchi zitatawala ili taifa lisiwe la Kiislam.Sasa itakuwa vipi tofauti na waislam kujianzishia mahakama yao?kama hawajaikubali bakwata ni vipi wataikubalia mahakama ya kadhi?
 
Thread yako nzuri kweli,ila umeuliza maswali ambayo kumbe ulitaka ufundishwe kwanza,ufupi kuna tofauti kubwa sana baina ya mwislamu na uislamu! bakwata ni mwislamu na mahakama ya kadhi ni uislamu,ktk uislamu kila jambo sheria ipo kama benk,afya nk.
 
Ukitaka kujua zaidi vp mahakama ya kadhi haiathiri uendeshaji na utekelezaji wa sheria za nchi pata taarifa toka Kenya, Uganda, Afrika ya kusini au Zanzibar. Pia hata waulize mawaziri wakongwe kama Wassira na wenzake akina George Kahama waliofanya kazi na nyerere kwani waliikuta ikitumiwa na mkoloni mpaka pale nyerere alipoamua kuifuta kwa sababu anazozijua yeye.
 
Hivi suala hili linahitaji mjadala bado? Mahakama ya kadhi ruksa.... ila waislamu waanzishe hata kwenye familia zao, sio jambo la serikali. Wawalipe makadhi wao kwa raha zao. Watunge sheria zao kwa raha zao, bila kuingilia sheria za nchi. Wakristo vilevile, mathalan wakatoliki, unadhani hawana sheria? Inaitwa Canon Law. Hii ni sheria mama ya kanisa lao. Waseme pia tuweke kwenye katiba ya nchi? Kwani nchi ni ya ukristo, usabato, uislamu.
Nadhani hapa tutashindwana. Ninahakika kwetu bara waislamu wasahau suala hili kwenye katiba ya Nchi. Labda huko kwao, wakakatane mikono na miguu na pua... si ndo tunayoona wenzao walio na mahakam ya kadhi?
 
Thread yako nzuri kweli,ila umeuliza maswali ambayo kumbe ulitaka ufundishwe kwanza,ufupi kuna tofauti kubwa sana baina ya mwislamu na uislamu! bakwata ni mwislamu na mahakama ya kadhi ni uislamu,ktk uislamu kila jambo sheria ipo kama benk,afya nk.

Kuuliza swali ni kutaka jibu..na km unalo huna haja ya kuanza jiwekea mipaka kwa kutaka kuanza sema ooh sijui hujui, sijui najua..go strainght to your views.

Lakini hata mahakama nayo inakuwa mwislam,sheria ndio uislam.Same kwa bakwata km taasisi unaweza iita muislam ila misingi ya uislam inayoifuata ndio uislam.


Tukirudi ktk msingi ni kwamba,km si innitiative ya waislam jambo hili litawezaje kuwa la kiislam?
 
Ukitaka kujua zaidi vp mahakama ya kadhi haiathiri uendeshaji na utekelezaji wa sheria za nchi pata taarifa toka Kenya, Uganda, Afrika ya kusini au Zanzibar. Pia hata waulize mawaziri wakongwe kama Wassira na wenzake akina George Kahama waliofanya kazi na nyerere kwani waliikuta ikitumiwa na mkoloni mpaka pale nyerere alipoamua kuifuta kwa sababu anazozijua yeye.

Wassira ni mweupe na mfuata upepo,yupo tayari kufuata lolote kwa vile ataonea aibu mfumo islam wa JK(Anayeabudiwa na kila gamba-wanamtaja kuliko Mwenyezi Mungu).

Mkoloni hakuw ana issue na mahakama hiyo kwa vile haikumhusu yeye na watu wake...sisi watanzania wa leo inatuhusu sana ktk mahusiano yetu.Ingekuwa waislama wamewekwa ktk mkoa wao na kuishi km wao pengine ingeweza fanyika.Ila hili la kukopeshana,kuoana nusunusu, na wasio waislam,kuchinja, mirathi ya ndoa mchanganyiko, watu kukacha dini na kuingia ingine...haitokuwa issue rahisi au ya waislam pekee.

Hizo nchi zilikuw ana shida sana,ni nchi za ukabila na udini....kwa hiyo kaburu hakuona shida wapa waislam hilo.kwani hata hivyo ni jamii za kihidni na kiarabu ambazo zilikuwa juu ya waafrica ila chini ya za mzungu kwa hiyo sharia haikuwahusu sana.Waganda tayai idd amini alijenga msingi wa migawanyo na haikuwa rahisi kwa rais mwingine kuitoa, kenya nao walikuwa na majimbo km Lamu, mombasa,malindi etc yalikuwa tayari si Kenya, na Kenya haijawahi fanya zoezi la kuunganisha nchi km TZ.
 
Hivi suala hili linahitaji mjadala bado? Mahakama ya kadhi ruksa.... ila waislamu waanzishe hata kwenye familia zao, sio jambo la serikali. Wawalipe makadhi wao kwa raha zao. Watunge sheria zao kwa raha zao, bila kuingilia sheria za nchi. Wakristo vilevile, mathalan wakatoliki, unadhani hawana sheria? Inaitwa Canon Law. Hii ni sheria mama ya kanisa lao. Waseme pia tuweke kwenye katiba ya nchi? Kwani nchi ni ya ukristo, usabato, uislamu.
Nadhani hapa tutashindwana. Ninahakika kwetu bara waislamu wasahau suala hili kwenye katiba ya Nchi. Labda huko kwao, wakakatane mikono na miguu na pua... si ndo tunayoona wenzao walio na mahakam ya kadhi?

Ndio najaribu fikiria watu wakikataa ruksa yako hiii..je watawezaje Lalamika kuwa serikali imeingialia mambo yao..sababu katiba itakuwa na namna fulani ya kutambua baadhi ya taratibu zao,ila kuna sehemu haitotambua kwa vile ni kinyume na haki za binadamu,kinyume na mila za watu,kinyume na dini zingine..hapo ndipo nataka utatuzi wao.kwani tayari katiba itakuwa na mgogoro na waislam km bakwata leo na serikali.
 
Ukitaka kujua zaidi vp mahakama ya kadhi haiathiri uendeshaji na utekelezaji wa sheria za nchi pata taarifa toka Kenya, Uganda, Afrika ya kusini au Zanzibar. Pia hata waulize mawaziri wakongwe kama Wassira na wenzake akina George Kahama waliofanya kazi na nyerere kwani waliikuta ikitumiwa na mkoloni mpaka pale nyerere alipoamua kuifuta kwa sababu anazozijua yeye.

Nyerere hakuifuta. Serikali ndio ilifuta. Kadhi ana uhusiano na Ugaidi
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom