gwakipanga
JF-Expert Member
- Dec 1, 2011
- 795
- 636
Nilikuwa natembea njiani, ghafla nikamuana mtu ninaemjua, mkononi kashika panga na chepe, kwajinsi nilivyomuona kama amekuwa chizi. Kwajinsi tulivyo angaliana akakunja sura na kutoa ishara kama nirudi nilikotoka, nageuka nyuma naona paka wawili weusi wamekaa sawa sawa kisha wamekenua meno, nikashikwa na mang'amung'amu ile napiga kelele sauti haitoki kama nimekabwa na jinamizi. Mwenye kujua tafsiri ya hii ndoto msaada tafadhali, mkuu mshana Jr ukichangia itapendeza zaidi. Nawasilisha.