ulimi waupanga
JF-Expert Member
- Aug 31, 2014
- 470
- 1,160
Wakuu habari? Naomba nichangie uzoefu wangu nilioushuhudia mwenyewe kwa macho yangu.
Kwenye imani ya Kikristo kuna sehemu imeandikwa" Mtu akifariki haoni, hasikii wala hajui chochote kinachoendelea Duniani" na pia kuna maelezo kwamba unapofariki roho yako inakwenda kwa Mungu moja kwa moja.
Shida yangu ni kwamba, kwenye jamii yetu ya Kihaya kuna kitu wanaita( nchweke) hii ni hali inampata mtu anakuwa kama kapandwa na mashetani lakini inakuwa ni roho ya mtu x aliyeshafariki tayari ambapo mtu huyo anaanza kuongea kwa sauti na rafudhi ya marehemu akikemea au kutoa taarifa ya jambo Fulani.
Nimekuwa nikisikia tu watu wakisimulia hili jambo lakini nikawa naichukulia kama ngano za kiafrika lakini mwaka Jana mwezi wa 12 Babu yetu kipenzi Mzee Cypriani alitutoka. Kama tamaduni zetu zilivyo tulijumuika wote kwenda kijijini kwenye msiba wa Babu hisipokuwa baba Mkubwa ambaye ndo mtoto Mkubwa wa babu alishindwa kufika kwa wakati akipanga kufika mwezi wa kwanza maana kajichimbia machimboni Msumbiji.
Siku ya Mazishi ilipofika tukatoka Malaloni(Makaburini) kumstiri Mzee ile tunafika tu ndani tukiwa kundi kubwa la watu na nyimbo za maombolezo zikitawala gafla Shangazi akadondoka akawa kama amepata kifafa Mara babu Mdogo na baba Mdogo nao wakaanza kama kuweuka. Watu wakaanza kutawanyika ovyoovyo maana ilikuwa ni taflani gafla. Wazee wa ukoo wakakusanyika wakaanza kuchoma majani machanga ya migomba na kuwawekea puani wale waliokabwa na kitu kisichojulikana huku wakiomba kilichowakaba kiongee.
Mara gafla wote watatu wakaanza kuongea kwa pamoja, sauti moja ya babu tuliyetoka kumzika mda huo huo. Akaanza kuwauliza wazee wa ukoo kwamba kwanini wamekubali kumzika bila mtoto wake Mkubwa kufika? Wakajitetea hapo na akawambia siyo kweli kwamba baba Mkubwa hana nauli Bali yuko bize tu na machimbo yake, akasema kabla baba Mkubwa hajafika nyumbani iyo tarehe aliopanga kuja atakuwa ameshamtembelea huko huko msumbiji aliko.
Niachane na iyo stori maana ni ndefu kidogo lakini swali langu ni kitu gani kinatokea kwa watu kama hawa kuweza kupanda juu ya vichwa vya wengine wakati wamekufa tayari? Je roho zao zinakuwa na kitu gani cha kipekee mpaka wawe na uwezo huu maana wengi ni wazee ndo wanaweza kufanya hili.
Kwenye imani ya Kikristo kuna sehemu imeandikwa" Mtu akifariki haoni, hasikii wala hajui chochote kinachoendelea Duniani" na pia kuna maelezo kwamba unapofariki roho yako inakwenda kwa Mungu moja kwa moja.
Shida yangu ni kwamba, kwenye jamii yetu ya Kihaya kuna kitu wanaita( nchweke) hii ni hali inampata mtu anakuwa kama kapandwa na mashetani lakini inakuwa ni roho ya mtu x aliyeshafariki tayari ambapo mtu huyo anaanza kuongea kwa sauti na rafudhi ya marehemu akikemea au kutoa taarifa ya jambo Fulani.
Nimekuwa nikisikia tu watu wakisimulia hili jambo lakini nikawa naichukulia kama ngano za kiafrika lakini mwaka Jana mwezi wa 12 Babu yetu kipenzi Mzee Cypriani alitutoka. Kama tamaduni zetu zilivyo tulijumuika wote kwenda kijijini kwenye msiba wa Babu hisipokuwa baba Mkubwa ambaye ndo mtoto Mkubwa wa babu alishindwa kufika kwa wakati akipanga kufika mwezi wa kwanza maana kajichimbia machimboni Msumbiji.
Siku ya Mazishi ilipofika tukatoka Malaloni(Makaburini) kumstiri Mzee ile tunafika tu ndani tukiwa kundi kubwa la watu na nyimbo za maombolezo zikitawala gafla Shangazi akadondoka akawa kama amepata kifafa Mara babu Mdogo na baba Mdogo nao wakaanza kama kuweuka. Watu wakaanza kutawanyika ovyoovyo maana ilikuwa ni taflani gafla. Wazee wa ukoo wakakusanyika wakaanza kuchoma majani machanga ya migomba na kuwawekea puani wale waliokabwa na kitu kisichojulikana huku wakiomba kilichowakaba kiongee.
Mara gafla wote watatu wakaanza kuongea kwa pamoja, sauti moja ya babu tuliyetoka kumzika mda huo huo. Akaanza kuwauliza wazee wa ukoo kwamba kwanini wamekubali kumzika bila mtoto wake Mkubwa kufika? Wakajitetea hapo na akawambia siyo kweli kwamba baba Mkubwa hana nauli Bali yuko bize tu na machimbo yake, akasema kabla baba Mkubwa hajafika nyumbani iyo tarehe aliopanga kuja atakuwa ameshamtembelea huko huko msumbiji aliko.
Niachane na iyo stori maana ni ndefu kidogo lakini swali langu ni kitu gani kinatokea kwa watu kama hawa kuweza kupanda juu ya vichwa vya wengine wakati wamekufa tayari? Je roho zao zinakuwa na kitu gani cha kipekee mpaka wawe na uwezo huu maana wengi ni wazee ndo wanaweza kufanya hili.