maforce
JF-Expert Member
- Mar 18, 2017
- 660
- 615
Unataka Mungu akutokee ili iweje? Kamaunasoma biblia utaona kuna watu wengi ambao waliishi kabla yetu ila Mungu(Yesu) aliwatokea watu wachache waliokuwa na kazi maalumu kutoka kwake mfano Musa, Yohana, Ibrahimu, na wengine wengi lakini hawakuomba awatokee. Pia kuna wakati wana waisraeli waliomba kama unachotaka wewe lakini alipowatokea hawakutamani tena kumuona Kutoka 19:10-25 na Kutoka 20:18-19. Kwa watumishi wa Mungu wanaweza kuyaelewa haya maneno zaidi maana kuna wakati Mungu anasema na mtumishi wake juu ya jambo ambalo wamekosea watu wengine hadi mtumishi unaiona hasira ya Mungu na hofu inakukuta kiasi kwamba unaanza kumwambia Mungu unisamehe. Tuache mambo ya kitoto maana kuna vitu ukiviomba wewe mwenyewe unaweza ukajiuliza hivi kweli nilichomba kina maana katika maisha yangu?Kama unaongeaga na Mungu basi mwambie anitokee na mimi