chamng'asi
JF-Expert Member
- Apr 23, 2012
- 211
- 385
Niko mbioni kununua hii gari kwaajili ya familia... Nimependa muonekano wake na pia injini ni ndogo cc 650 nitaimudu. Hofu yangu sijui chchte kuhusu hii gari. Msaada tafadhali kwa wajuvi wa mambo...
Mkuu nashukuru sanaNi nzuri kwa ulaji wa mafuta ila kinahitaji service mara kwa mara kwa familia hapana hakifai ni gari ya mizunguko midogo kwa hapa Town mimi ninayo ipo ktk hali nzuri kama unahitaji nicheki nikuhuzie
Nimewahi kulimiliki. Matumizi ya mafuta ni madogo sana. Tatizo haliwezi kupanda milima hususani kwenye njia za vumbi. Pia njia zenye mbavu za mbwa inarukaruka balaa
Sawa kiongozi nimekupata mkuu.....Sio nzuri kwa familia...aidha wewe na mwanao mmoja.
Cc 650.
Oooh sawa ndg shukurani kwa elimuNunua gari yenye kuanzia cc 1200 mpaka 1,500 ulaji unafanana umesema unataka Family Car hako kagari kakibeba watu wanne walioshiba kupanda mlima shida.
Sister anayo hio gari anapokaa kuna milima kikiwa kinawatu wanne walioshiba mpaka washuke ndo kipande mlima. Ila nunua mkuu roho ya paka hiyo gari.
Mkuu asante mno.... Sina swali tena umemalizaUmesema uko mbioni kununua hilo gari kwa ajili ya familia?
Kubeba familia na engine ya cc650? Haina nguvu ya kutosha. Kuwa na gari isiyo na nguvu ya kutosha kwa matumizi unayohitaji sio salama mkuu.
Pia kama unabeba familia manake engine itakuwa inafanya kazi kwa nguvu kubwa (high rpm) muda mrefu hivyo kuichosha haraka.
Nafasi ndani ni ndogo kwa matumizi ya familia. Udogo wa gari unamaanisha itokeapo ajali kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kupata majeraha.
Maana ya Kei car kwa wajapani ni city car. Inafaa kwa safari za mjini kwenye foleni kubwa na limited parking space.
Hahahahaaa umeenda mbali aiseeKei jina tu linatisha
Duh aisee kweli mkuu....Yani baba, mama na watoto mnajazana kwenye suzuki kei.. Si mtakua mnapumuliana sana.. Labda ukifanye cha kuwapeleka watoto shule