Mwenendo wa kiasi cha makusanyo na matumizi yenye viashiria vya Rushwa, Udanganyifu na Ubadhirifu kwa miaka mitatu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
Katika uchambuzi wa ripoti za CAG za mwaka 2019/20, WAJIBU imeainisha maeneo yenye viashiria vya rushwa, udanganyifu na ubadhirifu wa fedha za umma. Kiasi ambacho aidha hakikukusanywa au kimetumika na Serikali pasipo kupata tija yoyote kimeongezeka kutoka TZS 232.52 bilioni mwaka 2018/19 hadi TZS 1,770.84 bilioni mwaka 2019/20.

Mamlaka ya Serikali zaMitaa ndizo zimekuwa na ongezeko kubwa zaidi kutoka TZS 103.93 bilioni mwaka 2018/19 hadi TZS 863.85 bilioni kwa mwaka 2019/20 kama inavyoonekana katika Jedwali Na. 3.

Kati ya makusanyo na matumizi ambayo yanaviashiria vya rushwa, udanganyifu na ubadhirifu kwa mwaka 2019/20, Mamlaka ya Serikali za Mitaa ilikuwa na TZS 863.85 bilioni sawa na asilimia 49 ya TZS 1,770.84 bilioni ambapo kasoro nyingi zilionekana katika eneo la ununuzi wa umma na usimamizi wa mikataba.
1.PNG
 
Maneno mengi na blabla kibao, tuanze kwanza na VOTE ya Ikulu kwanini haikaguliwi na CAG na wakati ni fedha za umma? Pia kwanini mshahara wa Rais haukatwi kodi? tofauti na hapo kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake
 
Maneno mengi na blabla kibao, tuanze kwanza na VOTE ya Ikulu kwanini haikaguliwi na CAG na wakati ni fedha za umma? Pia kwanini mshahara wa Rais haukatwi kodi? tofauti na hapo kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake
Kwani CAG huwa hakagui hiyo miamala? Nadhani kuna sheria inasamehe mshahara wa Rais kulipishwa kodi. Niliwahi kusikia hivyo mahali fulani.
Ni Rais peke yake au hata Makamo na PM?
 
Kwani CAG huwa hakagui hiyo miamala? Nadhani kuna sheria inasamehe mshahara wa Rais kulipishwa kodi. Niliwahi kusikia hivyo mahali fulani.
Ni Rais peke yake au hata Makamo na PM?
Kuanzia PM, kama ni wazalendo mbona mishahara yao hawataki ikatwe kodi?
 
Back
Top Bottom