Mwendokasi yaua mtu Ardhi-Kivukoni, chanzo kuchat wakati akivuka barabara

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Wana JF.

Leo nimeshuhudia kifo cha ajabu mno. Ilikuwa hivi, MTU mmoja akiwa anatokea maeneo ya postal/ mjini alipofika kwa ofisi ya mwanasheria mkuu alivuka barabara ya kwanza inayotoka na kwenda Kivukoni.

Ghafla bila kuangalia huku akiwa anongea na simu ndipo mwendokasi ikampiga na kumzungusha chini ya uvungu na kukanyagwa na tyre lingine LA mbele, kakanyangwa shingo.

Wakati huo dreva tunamwambia rudi nyuma umekanyaga mtu, yeye akakosa nguvu kabisa arudisha kumbukumbu kurudi nyuma tayari damu nyingi zinachuruzika na mtu ajitingishi.

Mpaka sasa polisi ndio wanafika kuuchukua mwili.

Funzo: Usivuke barabara wakati unaongea na simu, kusikiliza mziki na headphone.
 
Duuu aloo sijawahi shuhudia kifo, ila nikivuta picha lazima upate motoo.

Kama ipo kama ilivyo, basi marehemu alikosea.
Marehemu ndiye kajiingiza, hata hivyo haya magari NAyO vimeo sana kwenye breki sio ya kuyaamini hata kama huko kwenye zebra, jamaa kabla ya kumgonga alimpigia honi lakini ndio hivyo sikio LA kufa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom