Mwema Vjana wako wanadai unawatuma!!!

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
May 9, 2007
3,832
2,790
Kila kona sasa hivi hapa Dar es Salaam ukikutana na mtu ukagusia milipuko ya bomu Arusha hakika wengi wanailaani CCM na UCHAFU WAKE wa tangu enzi na enzi!! Kitu cha kujiuliza ni kwamba bado CCM wanadhani wananchi bado ni mbumbumbu wa siasa kama enzi za TANU na ASP. Yale anayoongea Nape hakika amekishushia hadhi Chama cha CCM.

Nimekutana na Askari mmoja wa FFU nikamtania japo simfahamu kabisa nikamwambia "Wazee sasa hivi mko enzi za ukoloni Afrika Kusini, alinielewa nilichokuwa nataka kugusia. Jibu lake likawa hivi. "Ndg yangu yote hayo ni matokeo ya hofu ya kunyang'anywa madaraka. Hawa wakubwa wanahofia kwamba ikiwa Chadema kitachukua nchi wao wataishia kushitakiwa hivyo wanafanya kila linalowezekana kuhakikisha wanabaki madarakani, sisi tunatumwa kutekeleza mambo yao. Akasema ukiangalia ya Mwangosi na sasa hivi huko Arusha huwezi shangaa. Mlipuaji analiwa fedha nyingi ukiangalia hata donge nono walilotangaza la milioni mia moja ni danganya toto kwani wanajua watapindisha ushahidi.

Sasa kutokana na mambo kadhaa ambayo Polisi wamehusika tunategemea busara za IGP Said Mwema ajitathimini kama anafaa katika nafasi hiyo. Tulichokichoka ni zile tambwe za tutahakikisha tunawakamata watuhumiwa kokote waliko hata ndani na nje ya Tanzania, haya sasa tumeyachoka. Tumeyachoka kwasababu raia amegeuka ni bidhaa ya kugombewa na wanasiasa na mwanasiasa akizidia bidhaa inamwagwa chini yaani kuuawa.

Mr IGP I don't think we need you anymore, could you please step aside???
 
Unaota nini Mwema ajitathimini kwa lipi wakati yuko kwenye genge la viongozi wanaotoa maelekezo ya kuuwa wananchi kutokana na shahidi zilizo patikana hakika Mwema, Kikwete na Kinana ni wahusika wakuu wengine wanatumwa tuu
 
Nchi hii hakuna kiongozi ndani ya serikali <2005>anaeweza ku step down kwani akiachia madaraka tu serikali yote inaporomoka,walio juu wote lao ni moja na kama mmoja ataharibu siri hizo basi ajali ama kupigwa risasi kwa kufananishwa na jambazi ndiyo kitakachofatia,wamekula yamini kuwa wataikabidhi serikali hii kwa kiongozi mwingine yoyote yule ndani ya ccm<2015> and not otherwise,kwa maana hyo haya yote yanayotokea kuanzia wiziri mkuu,mkuu wa police,jeshi,jaji mkuu na hata amri jeshi mkuu wanayajua vizuri sana,wakifatiwa na viongozi wa chama na serikali wale wa juu kabisa,huku chini hakuna anaejua haya yanayotokea kwani hata conections zenyewe tu za tabu ndiyo maana wengi hasa wana ccm wanalaumu sana hawa vijana waliopewa madaraka kipindi hiki
 
Jakaya Mrisho Kikwete, hivi huoni kuwa Nchimbi na Mwema (shemejio) wameshakuharibia sifa kwa wananchi vya kutosha na bado unaendelea kuwalea!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!. Kiongozi yeyote anaelea mauaji wa raia wake, yeye nae ni muuaji tu. Ninakushauri kwa utume wa Mungu waondoe madarakani hao watu. Hawafai hata chembe kwa kipimo chochote kile.
 
Wanajidanganya tu make hakuna mamlaka popote pale iliyo juu kama alipokaa Muumba na hakujatokea mateso kama waliyopata kufanyiwa wana wa Mungu pale Misri ...ipo siku hawa watesi wanaoua,kutesa na kumwaga damu hukumu yao inakuja
 
Msajili wa vyama haoni ni hatari hiki chama kipya cha CCP kinamiliki silaha?
Pia kiunganishwe na ccm
Yaani CCM + CCP = MVURUGO WA AMANI.
 
Hali ya kungangania madaraka ikikolea na itakapofikia wakati kuua ili ubaki madarakani ni jambo la kawaida ipo siku Nape na Mwigulu watashika bunduki wenyewe ila kwa sasa wanaishikia nyuma ya Polisi. Nape na Mwigulu ni watu wa kushughulikiwa ipasavyo
 
Bado ndo tenda imetangazwa ya kumtafuta mshauri mwelekezi atakayesaidia ku-design namna nzuri ya ku-step DOWN!
Bila mwekezaji/ akili ya nje, kujiuzulu hatuna!
 
Je ni kiongozi chama kipi alisema watahakikisha nchi haitatawalika? je ni kiongozi wa chama kipi alisema wanahakikisha arusha watashinda kwa gharama yoyote? hiyo ni "circumstantial evidence" kuwa mauaji yote ya arusha yanapangwa na chadema ili watu waichukie serikali yao. Kumbuka kesi ya kupanga njama za mauaji iko mahakamani.
 
Kila kona sasa hivi hapa Dar es Salaam ukikutana na mtu ukagusia milipuko ya bomu Arusha hakika wengi wanailaani CCM na UCHAFU WAKE wa tangu enzi na enzi!! Kitu cha kujiuliza ni kwamba bado CCM wanadhani wananchi bado ni mbumbumbu wa siasa kama enzi za TANU na ASP. Yale anayoongea Nape hakika amekishushia hadhi Chama cha CCM.

Nimekutana na Askari mmoja wa FFU nikamtania japo simfahamu kabisa nikamwambia "Wazee sasa hivi mko enzi za ukoloni Afrika Kusini, alinielewa nilichokuwa nataka kugusia. Jibu lake likawa hivi. "Ndg yangu yote hayo ni matokeo ya hofu ya kunyang'anywa madaraka. Hawa wakubwa wanahofia kwamba ikiwa Chadema kitachukua nchi wao wataishia kushitakiwa hivyo wanafanya kila linalowezekana kuhakikisha wanabaki madarakani, sisi tunatumwa kutekeleza mambo yao. Akasema ukiangalia ya Mwangosi na sasa hivi huko Arusha huwezi shangaa. Mlipuaji analiwa fedha nyingi ukiangalia hata donge nono walilotangaza la milioni mia moja ni danganya toto kwani wanajua watapindisha ushahidi.

Sasa kutokana na mambo kadhaa ambayo Polisi wamehusika tunategemea busara za IGP Said Mwema ajitathimini kama anafaa katika nafasi hiyo. Tulichokichoka ni zile tambwe za tutahakikisha tunawakamata watuhumiwa kokote waliko hata ndani na nje ya Tanzania, haya sasa tumeyachoka. Tumeyachoka kwasababu raia amegeuka ni bidhaa ya kugombewa na wanasiasa na mwanasiasa akizidia bidhaa inamwagwa chini yaani kuuawa.

Mr IGP I don't think we need you anymore, could you please step aside???

rais kikwete aliwahi kusema anataka afanye jambo ambalo kwa hilo atakumbukwa daima, tumsikilizie kimya kingi mshindo mkuu, anaweza kuleta suluhu ya haya na tukamweka katika kumbukumbu za vizazi vyetu daima
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom