Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,314
- 33,108
Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Saidi Mwema.
[FONT=ArialMT, sans-serif]Jeshi la Polisi nchini, limetangaza mkakati wake wa kukomesha vitendo vya baadhi ya askari wake kujihusisha na vitendo vya rushwa kwa kuwazaidia kiasi cha fedha walichokataa kupokea.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mpango huo ulitangazwa na mkuu wake, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Saidi Mwema juzi wakati akizungumza na vikosi kazi katika Ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi, mjini hapa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Jeshi la polisi sasa rushwa basi, tunataka kuaminiana na wananchi wetu Tanzania nzima kati ya Januari na Machi kama kuna askari aliyekataa rushwa ya kiasi chochote kwa ushahidi, atalipwa kiasi hicho, hata kama ni milioni 10 alisisitiza.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema, hatua hiyo ndiyo njia pekee itakayosaidia kumaliza tatizo la rushwa ndani ya jeshi hilo ambalo limekuwa likilalamikiwa na kutuhumiwa kuwa linajihusisha na vitendo hivyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliwataka askari watakaoendelea kujihushisha na vitendo vya kuomba na kupokea rushwa wajiondoe mapema katika jeshi hilo, vinginevyo watakabiliwa na hatua kali za kisheria.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kula rushwa ili uuze haki ya mtu ni dhambi, una mdhalilisha mtu gharama ya mtu anayekupatia rushwa inataka umdhulumu mwingine haki jambo ambalo ni la hatari sana kwa maendeleo ya nchi, alisistiza Mwema.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliwaagiza makamanda wa mikoa nchini wapokee, kuyapitie na kumpatia majina ya askari waliokataa kupokea rushwa kati ya Januari hadi Machi 2, mwaka huu hata kama ni Sh milioni 10,000 jeshi hilo limpatie mara moja.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Vilevile aliwatahadharisha wagombea na wapiga kura watakaoshiriki kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu wasijihusishe na rushwa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema yeyote atakayepuuzia agizo hilo atakumbana na mkono mrefu wa Serikali kwa madai kuwa safari hii polisi kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kukomesha tabia hiyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mwema yupo katika ziara ya siku tano mkoani hapa ikiwa ni ya kwanza kuifanya tangu ateuliwe na Rais Jakaya Kikwete kuliongoza Jeshi la Polisi.[/FONT]
CHANZO: NIPASHE