samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
serikali inaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo vinavyotokana na ajali za usafiri wa vyombo vya majini endapo itaanzisha utaratibu wa kulazimisha vyombo vyote vya usafiri wa majini viwe na life jackets zitakazovaliwa na abiria wakati wa safari kama ambavyo abiria wanaosafiri kwa kutumia mabasi wanavyolazimika kufunga mikanda wakati wa safari. Utaratibu huu wa sasa unaotumika wa kufungia life jackets chache stoo na kusubiri ajali itokee ndipo watu waanza kugombania maboya machache yaliyopo utaendelea kugharimu maisha ya wananchi wengi. Serikali sasa inapaswa kusimama kidete na kuhakikisha vyombo vyote vinavyosafiri majini vinakuwa na life jackets za kutosha na kuhakikisha abiria wote wana hamasishwa kuvaa life jackets kabla ya kuanza safari.
Nawasilisha.
Nawasilisha.