Mwanza: Yaliyojiri kwenye kuaga mwili wa Hayati Magufuli Uwanja wa CCM Kirumba

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,797
11,959
Kutoka katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza tayari viongozi wa kiserikali na Chama cha Mapinduzi pamoja na wananchi wa Mkoa wa Mwanza na mikoa jirani wameshaanza kuingia kwenye uwanja huu tayari kumuaga mpendwa wetu Dk John Magufuli.

Mageti ya uwanja wa CCM Kirumba yamefunguliwa toka saa 12 alfajiri na wananchi ni wengi sana ambao wako nje ya uwanja wakiendelea kuingia kwenye uwanja huu.

Mikoa zaidi ya mitano ya Mwanza, Shinyanga, Geita, Tabora na Mara yote wananchi wake kwa uwingi wao wanaendelea kuingia kwenye uwanja huu.

Mwili wa aliyekua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli aliyefariki Machi 17 mwaka huu utaagwa kwenye uwanja huu kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwake Chato, Geita kwa ajili ya mazishi.

=====
1616570481814.png
1616570506510.png
1616570522144.png
1616570539156.png
1616570582316.png
IMG_20210324_091559_308.jpg

MWANZA: Mwili wa Hayati Dkt. John Magufuli umeshawasili Mwanza ambapo idadi kubwa ya Wananchi wameonekana wakiwa wamejipanga barabarani na wengine wakisindikiza mwili wakati ukipelekwa Uwanja wa CCM Kirumba.

Dkt. Magufuli alifariki dunia Machi 17, 2021 na anatarajiwa kuzikwa Machi 26 Chato Mkoani Geita.

Baada ya mwili wa Hayati Rais Magufuli kuwasili jijini Mwanza, utapelekwa nyumbani kwa mjane wake, Mama Janeth Magufuli, maeneo ya Busisi, kupitia katika daraja la Kigongo-Busisi.

Jeneza lenye mwili wa Hayati Rais Magufuli litasimamishwa Busisi kwa dakika 10, kwa ajili ya kutolewa heshima za mwisho.

Baada ya mwili huo kutolewa heshima za mwisho mjini Busisi, utapelekwa Wilayani Sengerema, Geita Mjini hadi Katoro wilayani Chato, Mkoa wa Geita.

 
Kila uzi wa Magu ukifunguliwa umo tu!!!hv hakuna nyuzi zingine ukaenda huko......
kila uzi umo
Kama unapata maumivu makali hivi ya moyo kwa sababu ya mimi kuchangia nyuzi za huyo magufuli, si ufe tu mkuu!!

Kwani habari ya mjini kwa sasa ni nini? Mbona umejipa cheo kigumu hivi cha kunifuatilia? Na siendi kokote sasa! 😇

Nikiona tu uzi wa kumhusu magufuli na ccm, nakuja faster! Sababu si unaifahamu mzee mzima ras jeff kapita ?
 
Kama unapata maumivu makali hivi ya moyo kwa sababu ya mimi kuchangia nyuzi za huyo magufuli, si usife tu mkuu!!

Kwani habari ya mjini kwa sasa ni nini? Mbona umejipa cheo kigumu hivi cha kunifuatilia? Na siendi kokote! Nikiona tu uzi wa kumhusu magufuli na ccm, nakuja faster! Sababu si unaifahamu mzee mzima ras jeff kapita ?
Ok haina noma popote nikikukuta unaponda na mimi nakutandika
 
Kesho!! Ni keshokutwa boss
Duh! Pole nyingi sana ziwafikie familia ya marehemu. Na hasa mke na watoto. Wanapitia kipindi kigumu sana kwa kuomboleza kwa muda wote huu.

Na bado kuna kipindi kingine cha miaka kadhaa ya maombolezo, kabla ya kusahau na kukubali matokeo.

NB: Hizo pole zangu nilizo toa hapo juu haziwahusu MATAGA, wanasiasa wanafiki, wachumia tumbo na waimba mapambio. Ni pole za familia tu ya Mh. Hayati Rais John Pombe Joseph Magufuli.
 
Back
Top Bottom