Mwanza: Wanaodaiwa kusafirisha dhahabu wapandishwa kizimbani, wasomewa makosa 7

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,888
Mwanza. Watu 12 wakiwemo askari polisi wanane watapandishwa kizimbani muda wowote leo Ijumaa Januari 11, 2019 katika mahakama ya hakimu mkazi Mwanza.

Wamefikishwa mahakamani hapo leo na wanasubiri kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayowakabili.

Watu hao wanadaiwa kuhusika na tukio la kusafirisha shehena ya dhahabu kilo 323.6 na fedha taslimu Sh305 milioni kutoka mkoani Mwanza kuelekea Geita.

Wanashikiliwa na polisi tangu tukio hilo lilipotokea Januari 5, 2019.

Askari watakaopandishwa kizimbani leo walitajw ana Rais John Magufuli siku mbili zilizopita kuwa wanadaiwa kuhusika katika tukio hilo, kuwasaidia wahusika kufanikisha kusafirisha shehena hiyo.

Chanzo: Mwananchi

=====

WALIODAIWA KUTOROSHA DHAHABU WAFIKISHWA MAHAKAMANI: Watuhumiwa 12 wa utoroshaji wa Dhahabu waliokamatwa hivi karibuni wamefikishwa mahakamani alasiri hii wakiwemo askari wanane (8) waliokamata dhahabu hiyo.

Watuhumiwa hao wamefikishwa katika Mahakamani ya Hakimu mkazi wa Mkoa wa Mwanza huku wakikabiliwa na makosa Saba (7).
 
Mahakamani ni formality tu!
Kesi alishaiamua rais.
Huyu hakimu wa kupingana na jiwe atatokea wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao askari ngoja wakione cha mtema kuni,baadhi ya askari mwanza ni majambazi ukitaka kuona hilo ww kamatwa hata umechekewa kdg usiku uone wanavyo sachi mifuko yote na kuondoka na kila kitu..


Safi sana mheshimiwa raisi wetu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,hakika ww ni raisi wa wanyonge!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ala
Watu kusota rumande na hata kabla mahakama haijasema lolote tayari ameshageuka rais wa wanyonge?

Yani waziri alishapewa order tayari kwamba ile dhahabu itatusaidia kupata fedha za kigeni kabla hata watu hawajaingia kwenye mlango wa mahakama.

Nachoona hiyo mahakama wala haina sababu, rais angeachiwa tu amalizie kuhukumu!
Hao askari ngoja wakione cha mtema kuni,baadhi ya askari mwanza ni majambazi ukitaka kuona hilo ww kamatwa hata umechekewa kdg usiku uone wanavyo sachi mifuko yote na kuondoka na kila kitu..


Safi sana mheshimiwa raisi wetu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,hakika ww ni raisi wa wanyonge!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ala
Watu kusota rumande na hata kabla mahakama haijasema lolote tayari ameshageuka rais wa wanyonge?

Yani waziri alishapewa order tayari kwamba ile dhahabu itatusaidia kupata fedha za kigeni kabla hata watu hawajaingia kwenye mlango wa mahakama.

Nachoona hiyo mahakama wala haina sababu, rais angeachiwa tu amalizie kuhukumu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ww ni mkazi wa Mwanza au ulishawahi kufika mwanza?

Baadhi ya askari police mwanza wanafanya kazi zao kama walivyo vibaka,wakikukamata ni mwendo wa jeki huku una pigwa sachi ya maana ukicheza wanaondoka hadi ma suruali unabaki na boksa.

Mengine ngoja tuiachie mahakama ila itabidi nikacheki sura zao maana kuna mmoja huyo akiondoka na wallet yangu bila kujari kuwa wallet inabeba vingi ikiwemo vitambulisho.


JPM hakika ww ni mtenda haki bila kujari cheo cha mtu,asante raisi wangu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanza nimekaa sana, wewe ulipigwa tero ukiwa wapi?
Mkuu ww ni mkazi wa Mwanza au ulishawahi kufika mwanza?

Baadhi ya askari police mwanza wanafanya kazi zao kama walivyo vibaka,wakikukamata ni mwendo wa jeki huku una pigwa sachi ya maana ukicheza wanaondoka hadi ma suruali unabaki na boksa.

Mengine ngoja tuiachie mahakama ila itabidi nikacheki sura zao maana kuna mmoja huyo akiondoka na wallet yangu bila kujari kuwa wallet inabeba vingi ikiwemo vitambulisho.


JPM hakika ww ni mtenda haki bila kujari cheo cha mtu,asante raisi wangu!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanza nimekaa sana, wewe ulipigwa tero ukiwa wapi?


Sent using Jamii Forums mobile app
Mwaka jana mda kama saa tatu usiku napita zangu karibu na rock city mall sina hili wala lile nastuakia napigwa jeki,sitatulia vzr nipo kwenye tenga,askari kama wawili wana sachi mifuko eti sijui wanatafuta bangi,utadhani waliambiwa mm ndo muuzaji halafu watu kibao wana sachiwa lakn badala watafute bangi wanaondoka na vyote vilivyo kwenye mifuko ya suruali.


Noma sana ila niliongea na kujitambulisha kwa mkubwa wao ndo nikaachiwa ila sikupata vitu vyangu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanza. Watu 12 wakiwemo askari polisi wanane watapandishwa kizimbani muda wowote leo Ijumaa Januari 11, 2019 katika mahakama ya hakimu mkazi Mwanza.

Wamefikishwa mahakamani hapo leo na wanasubiri kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayowakabili.

Watu hao wanadaiwa kuhusika na tukio la kusafirisha shehena ya dhahabu kilo 323.6 na fedha taslimu Sh305 milioni kutoka mkoani Mwanza kuelekea Geita.

Wanashikiliwa na polisi tangu tukio hilo lilipotokea Januari 5, 2019.

Askari watakaopandishwa kizimbani leo walitajw ana Rais John Magufuli siku mbili zilizopita kuwa wanadaiwa kuhusika katika tukio hilo, kuwasaidia wahusika kufanikisha kusafirisha shehena hiyo.

Chanzo: Mwananchi

=====

WALIODAIWA KUTOROSHA DHAHABU WAFIKISHWA MAHAKAMANI: Watuhumiwa 12 wa utoroshaji wa Dhahabu waliokamatwa hivi karibuni wamefikishwa mahakamani alasiri hii wakiwemo askari wanane (8) waliokamata dhahabu hiyo.

Watuhumiwa hao wamefikishwa katika Mahakamani ya Hakimu mkazi wa Mkoa wa Mwanza huku wakikabiliwa na makosa Saba (7).
Polisi wetu wamekuwa kero sana kwa kweli,huku mtaani kwetu wameua mtu katika mazingira ya kutatanisha,lakini mpata leo sioni kinachoendelea,ni kulindana tu mtindo mzima.Ni kama wanajiona wako untouchable hivii.Jeshi la Polisi linahitaji complete overhaul kama ilivyofanywa na IGP mstaafu Philemon Mgaya na mkuu wa TISS then Bwana Kitine mwaka 1975.Cosmetic changes zinazofanyika sasa hazitatusaidia kamwe.
 
Kwanini hukuviomba?
Sio kama nawatetea polisi, hapa naomba nieleweke! Nazijua vyema tabia zao.
Ila amini usiamini wapo askari wastaarabu na waelewa sana!
Kwenye hilo sakata la dhahabu nina kila sababu ya kuamini kuwa hao jamaa wanaonewa!
Mwaka jana mda kama saa tatu usiku napita zangu karibu na rock city mall sina hili wala lile nastuakia napigwa jeki,sitatulia vzr nipo kwenye tenga,askari kama wawili wana sachi mifuko eti sijui wanatafuta bangi,utadhani waliambiwa mm ndo muuzaji halafu watu kibao wana sachiwa lakn badala watafute bangi wanaondoka na vyote vilivyo kwenye mifuko ya suruali.


Noma sana ila niliongea na kujitambulisha kwa mkubwa wao ndo nikaachiwa ila sikupata vitu vyangu!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanini hukuviomba?
Sio kama nawatetea polisi, hapa naomba nieleweke! Nazijua vyema tabia zao.
Ila amini usiamini wapo askari wastaarabu na waelewa sana!
Kwenye hilo sakata la dhahabu nina kila sababu ya kuamini kuwa hao jamaa wanaonewa!

Sent using Jamii Forums mobile app
Ww pia ni askari na ndo maana kuongea na ww tukaelewana ni ngumu ,ujue ya kuwa nyie askari japo siyo wote huwa mnaona ya kuwa nyie ni untouchable mpo huru kufanya chochote bila kuwajibishwa.

Kwahy ww huwezi kuona ouvu wa askari wenzako,hapo ni kesi ya nyani kumpelekea tumbili!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom