Mwanza: Walimu wadaiwa kuhamishwa kwa nguvu

Mmawia

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
121,947
95,237
Walimu wahamishwa kwa nguvu Mwanza
-
Halmshauri ya Jiji la Mwanza imewahamisha kwa nguvu kwenye nyumba walizokuwa wanakaa walimu wanne wa shule za sekondari Mlimani, Mapango na Pamba za Jiji hilo ili kupisha ukarabati unaotekelezwa na Serikali.

Zoezi la kuwaondoa walimu hao kwenye nyumba hizo limefanyika baada ya kukataa kuhama kwa hiari na kudai hawajalipwa fedha za kufunga mizigo.

Zoezi hilo limefanyika kwa kusimamiwa na askari mgambo.

Akisimamia zoezi hilo jana kwa niaba Mkurugenzi wa Jiji, Kiomoni Kibamba, Ofisa Mtendaji wa kata ya pamba, Jonas Mugisha amesema walimu hao wameondolewa kwa nguvu baada ya kukaidi amri ya kuhama kwa hiari kupisha ukarabati wa nyumba hizo.

Amesema walimu hao walipewa barua iliyokuwa ikiwataka kuhama kwenye nyumba hizo ili ziweze kukarabatiwa pamoja na shule hiyo kwani serikali imetowa Sh milioni 540.

Mmoja wa walimu hao, Abel Dendwa akizungumza kwa niaba ya walimu hao amesema inasikitisha kuona mfanyakazi wa umma anafanyiwa vitendo vya unyanyasaji nakwamba ni vema serikali ikaingilia kati suala hilo ili haki iweze kutendeka ikiwamo ya kulipwa fedha zao za kufunga mizigo.

Mtanzania
 
Nyumba ilipokuwa mbovu mlisema ooh tunaishi nyumba za mkoloni,nyumba zimejaa mapopo na kunguni walimu hatuthaminiwi...hela imekuja ya ukarabati sasa ,kutoka hamtaki kupisha ukarabati, kufunga Tu mizigo yako yenyewe uhame Kwa mda na penyewe mpak ulipwe ....... Kimsingi Tu mlitakiwa mtolewe Kwa bakora za kutosha ....
 
Nyumba ilipokuwa mbovu mlisema ooh tunaishi nyumba za mkoloni,nyumba zimejaa mapopo na kunguni walimu hatuthaminiwi...hela imekuja ya ukarabati sasa ,kutoka hamtaki kupisha ukarabati, kufunga Tu mizigo yako yenyewe uhame Kwa mda na penyewe mpak ulipwe ....... Kimsingi Tu mlitakiwa mtolewe Kwa bakora za kutosha ....
Sawa siloo,ila sii sawa,ama nawe no miongoni mwa majina ya isisii.
 
Walimu wahamishwa kwa nguvu Mwanza
-
Halmshauri ya Jiji la Mwanza imewahamisha kwa nguvu kwenye nyumba walizokuwa wanakaa walimu wanne wa shule za sekondari Mlimani, Mapango na Pamba za Jiji hilo ili kupisha ukarabati unaotekelezwa na Serikali.

Zoezi la kuwaondoa walimu hao kwenye nyumba hizo limefanyika baada ya kukataa kuhama kwa hiari na kudai hawajalipwa fedha za kufunga mizigo.

Zoezi hilo limefanyika kwa kusimamiwa na askari mgambo.

Akisimamia zoezi hilo jana kwa niaba Mkurugenzi wa Jiji, Kiomoni Kibamba, Ofisa Mtendaji wa kata ya pamba, Jonas Mugisha amesema walimu hao wameondolewa kwa nguvu baada ya kukaidi amri ya kuhama kwa hiari kupisha ukarabati wa nyumba hizo.

Amesema walimu hao walipewa barua iliyokuwa ikiwataka kuhama kwenye nyumba hizo ili ziweze kukarabatiwa pamoja na shule hiyo kwani serikali imetowa Sh milioni 540.

Mmoja wa walimu hao, Abel Dendwa akizungumza kwa niaba ya walimu hao amesema inasikitisha kuona mfanyakazi wa umma anafanyiwa vitendo vya unyanyasaji nakwamba ni vema serikali ikaingilia kati suala hilo ili haki iweze kutendeka ikiwamo ya kulipwa fedha zao za kufunga mizigo.

Mtanzania

Kwahiyo walimu walitaka nyumba zikarabatiwe wakiwa ndani humo humo?
Au wanahofia wakiziacha kupisha ukarabati hawatapewa tena nyumba hizo?

Kwa namna yoyote ile wao walitakiwa kupisha ukarabati, kulia lia ni kutafuta huruma kwani watumishi ni wao tu? Mbona wengine wamepanga na maisha yanaenda vizuri bila shida?
 
Kwahiyo walimu walitaka nyumba zikarabatiwe wakiwa ndani humo humo?
Au wanahofia wakiziacha kupisha ukarabati hawatapewa tena nyumba hizo?

Kwa namna yoyote ile wao walitakiwa kupisha ukarabati, kulia lia ni kutafuta huruma kwani watumishi ni wao tu? Mbona wengine wamepanga na maisha yanaenda vizuri bila shida?
Kwani umeambiwa kuwa wana kaa bure?inawezekana wewe siyo mtumishi hivyo vigezo vya kupewa nyumba huvijui.
 
Kwahiyo walimu walitaka nyumba zikarabatiwe wakiwa ndani humo humo?
Au wanahofia wakiziacha kupisha ukarabati hawatapewa tena nyumba hizo?

Kwa namna yoyote ile wao walitakiwa kupisha ukarabati, kulia lia ni kutafuta huruma kwani watumishi ni wao tu? Mbona wengine wamepanga na maisha yanaenda vizuri bila shida?
Wao walifanikisha ushindi wa kisayansi tu,wakarudishiwa akili wakati maslahi ya siku ile yalishakwisha,wengine kazi zao ni kuimba mapambio vipato vinaingia,hivyo lazime wastuke.
 
Back
Top Bottom